mirindimo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 819
- 1,320
Maeneo ya morocco hotel kuna vurugu kubwa ss hivi inasemekana kuna wanajeshi 3 wamepiga mwananchi na kumuua na wananchi wakaanza kumshambulia mwanajeshi huyo alievalia kiraia huku wenzake wakikimbia na kumwacha akila kichapo! Alijaribu kukimbilia ktk daladala likaharibiwa vibaya kwa mawe na wananchi hao wengi wakiwa ni vijana! Dalala hilo liko mbele ya daladala tulilo sisi ,mpaka tunavuka eneo la tukio hakuna askari yoyote aliefika na hatujui hatma ya kijana huyo aliejitambulisha kua yeye ni mwanajeshi