Teofilo Kisanji University

Masanja

JF-Expert Member
Aug 1, 2007
4,819
8,884

Waungwana katika pita pita yangu, nimekutana na hiki Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji University kilichoko Mbeya. I dont know much about it. Mweye details atupe. But naona hakijapata usajili kamilifu ingawa kinaendelea na juhudi za kutoa elimu. Hakika ukiangalia by all standards ni kwamba kina mapungufu mengi. LAKINI je watanzania tufanye nini kusaidia vyuo kama hivi? ambavyo si tuu vina upungufu wa elimu, lakini pia hata uwezo wa kuattract wanafunzi makini unakuwa haupo. Kipi kifanyike? NAJUA wote tuna kiu ya kusaidia elimu hapa nyumbani. Ni vema juhudi kama hizi tusizibeze bali tuwape mawazo ni namna gani wanaweza wakawa nyenzo bora mbadala ya kupigana na umaskini.

By the way kwa mlio nje na mna elimu zenu, naamini huu ndo mwanya muafaka wa kuchangia maendeleo ya taifa letu kwa kussuport by any means, kama kuja kufundisha, kuwalink na universities huko nje, Kuwasaidia na exchange programme kama zipo nk. Nimefarijika kuona Prof. Mbonile wa UD kaenda kufundisha pale, sijui kwa nini, lakini naamini vyuo kama hivi vitafaidika na utalaamu wa wasomi kama hawa.


Link yake ni hii: http://teku.ac.tz/index.php?option=com_frontpage&Itemid=1

Tuwasaidie, tusiwabeze.
 

Mweye details atupe...........But naona hakijapata usajili kamilifu ingawa kinaendelea na juhudi za kutoa elimu. Hakika ukiangalia by all standards ni kwamba kina mapungufu mengi............Nimefarijika kuona Prof. Mbonile wa UD kaenda kufundisha pale, sijui kwa nini, lakini naamini vyuo kama hivi vitafaidika na utalaamu wa wasomi kama hawa.


Tuwasaidie, tusiwabeze.

Masanja,
Asante kwa utambulisho wa chuo, mimi binafsi nilikuwa sijawahi kukisikia hiki chuo. Nimesoma vizuri maelezo yako ila kuna mahali umeniacha angalia hiyo quote hapo juu. Weka bayana ujuvi wako juu ya huu usajili nusu nusu, na mbona unashangaa Prof. kujuunga na hii university?
 
By the way who's Theofilo Kisanji???? Any idea please???? Ni vyema ukawa na uhakika kama kina usajili au la!! but to my views ni ndoto nzuri kwa wahusika kuwa na wazo kama hilo muhimu wanatakiwa kuonyeshwa njia ili waende ktk njia sahihi kuepuka kuwa mahali pa kuwapotosha vijana...Universities commission (Tz) do have any idea on the existence of this University????
 
Masanja,
Asante kwa utambulisho wa chuo, mimi binafsi nilikuwa sijawahi kukisikia hiki chuo. Nimesoma vizuri maelezo yako ila kuna mahali umeniacha angalia hiyo quote hapo juu. Weka bayana ujuvi wako juu ya huu usajili nusu nusu, na mbona unashangaa Prof. kujuunga na hii university?

Hapana ndugu mimi sina ujuvi wowote katika hili. Labda uende kwenye tovuti yao. What I read kilikuwa bado hakijapata full accreditation lakini shule inaendelea kama kawaida. Sasa hapo ndo sijui kama wanaruhusiwa kutoa degree au la. But from my small knowlsge hata Mzumbe imepata accrediation juzi juzi tuu. Kwa hiyo its possible kuwa na wao bado hawajapa. Swala la Profesa kwenda pale, la hasha sishangai ila nimefurahi, maana Mbonile ni Prof. Pale UD na huu ni moyo wa kizalendo kwa Prof. Kama yule ambaye ana potential ya kutengeneza hela ya uhakika na mambo mengine kuamua kwenda kwenye chuo ambacho hakijawa na jina.

I hope umenipata! Again mi sio mjuvi wa lolote!
 
By the way who's Theofilo Kisanji???? Any idea please???? Ni vyema ukawa na uhakika kama kina usajili au la!! but to my views ni ndoto nzuri kwa wahusika kuwa na wazo kama hilo muhimu wanatakiwa kuonyeshwa njia ili waende ktk njia sahihi kuepuka kuwa mahali pa kuwapotosha vijana...Universities commission (Tz) do have any idea on the existence of this University????

Kipanga,

Jina ni kwa heshima ya Marehemu Theofilo Kisanji (1915 - 1982) aliyekuwa Askofu wa kwanza Mwafrika wa Kanisa la Moravian Tanzania.

Nawapongeza sana wamiliki kwa kuanzisha chuo hiki. Kwa kuwa Tanzania tunapenda sana kusoma naamini ni suala la muda tu chuo kitakua na kuimarika.

http://sw.wikipedia.org/wiki/Chuo_Kikuu_Teofilo_Kisanji
 
Mie nadhani makanisa yanayoanzisha vyuo vikuu kabla ya kuanzisha angalau vijisekondari vitano yanakosea. Inabidi kujenga tokea kwenye msingi, na sio kuanzia kwenye paa.

Moravian Church wangepashwa kuanzisha Kisanji High School kabla hawajaanzisha Kisanji University. Wasiokuwa na uwezo wa kuendesha high school watawezaje kuendesha vyuo vikuu? These glorified primary schools are not, and will never be universities, no mater what you call them.
 
Moravian Church wangepashwa kuanzisha Kisanji High School kabla hawajaanzisha Kisanji University. Wasiokuwa na uwezo wa kuendesha high school watawezaje kuendesha vyuo vikuu? These glorified primary schools are not, and will never be universities, no mater what you call them.

Mkuu Augustine Moshi kuhusu sekondary na high schools hawa jmaa wanazo nyingi tu (Lutengano, Kafule, Mbozi etc......) na one of them is one of the oldest school in Tz est 1891 (Rungwe) ambayo ilitaifishwa na serikali Pia wana vyuo vya veta, ualimu,nursing etc.. Na hii hoja yako ya glorified primary school una maanisha majengo, taaluma au? Unaweza kufafanua plz?
 
Mkuu Augustine Moshi kuhusu sekondary na high schools hawa jmaa wanazo nyingi tu (Lutengano, Kafule, Mbozi etc......) na one of them is one of the oldest school in Tz est 1891 (Rungwe) ambayo ilitaifishwa na serikali Pia wana vyuo vya veta, ualimu,nursing etc.. Na hii hoja yako ya glorified primary school una maanisha majengo, taaluma au? Unaweza kufafanua plz?

Atakuwa anaangalia majengo huyo. Anasahau kuwa huu ni mwanzo tu, na chuo kikuu ni vichwa sio majengo.
 
Mapinduzi ya elimu mahali popote yanatafriwa kwa kuwepo kwa hamasa ya wananchi kuanzisha na kusimamia taasisi za elimu. Sasa hivi Tanzania inafanya mapinduzi ya elimu. Nasema mapinduzi kwa sababu huko nyuma msisitizo wa elimu ulikuwa katika kiwango cha elimu ya msingi. Ndivyo wanasiasa wetu walivyokuwa wakitufanya tuamini na hivyo ndivyo kwa kiasi kikubwa tulivyoamini. Mtu akizunguzia elimu wazo la kwanza lilikuwa elimu ya msingi. Ukifika kwenye halmashauri ukakutana na afisaelimu wa wilaya au manispaa, ilikuwa si jambo la kushangaa kuona mazungumzo yote ni kuhusu elimu ya msingi na ngumbaro. Na hata sera yetu ya elimu iliweka bayana kuwa basic education ni primary na elimu ya watu wazima. Elimu katika kiwango cha juu ya hapo ilkuwa anasa. Suala la basic education katika nchi nyingi sasa limekuwa pana zaidi na kujumuisha sekondari, lakini si kwa Tanzania; labda tusubiri mhuisho wa sera ya elimu iliyopo.

Tunafahamu wenzetu walioendelea kidogo kiuchumi na kijamii waliweka msisitizo katika eliu ya juu pia. Nilikuwa nazungumza mkenya mmoja kuhusu Tanzania kutumia wahitimu wa form six kama walimu wa sekondari na kwamba serikali inajitahidi kuwadhamini katika masomo yao ya chuo kikuu. Alinishangaa sana na kuniuliza ni kwa nini serikali iajiri na kuanza kuwasomesha walimu wasio walimu na kwa nini isiajiri wahitimu wa chuo kikuu. Na mimi nikabaki ninamshangaa kwa sababu alikuwa anafikiri Tanzania kuna excess university graduates katika soko la ajira kama walivyo huko Kenya.

Lakini hoja ya ndugu huyo wa Kenya inatukumbusha jambo moja muhimu katika mfumo wetu wa elimu: Tumeshindwa kuingalia elimu kwa upana wake.
-Ni wakati sasa tukajuimusha elimu ya sekondari katika basic education, na itolewe kwa wote.Halmashauri zisimamie elimu katika upana wake, sio elimu ya msingi tu. Nafahamu kuna juhudi za kujenga shule za sekondari katika level ya halmashauri. Hoja yangu hasa ni uendeshaji na usimamiaji wa ubora wa elimu. Tunahitaji katika halmashauri pawepo maafisa mafunzo kazini (siyo wakaguzi) watakaoendesha mafunzo kazini katika level ya sekondari. Msisitizo uwe njia bora za ufundishaji hasa njia shirikishi. Eneo hili halina mwenyewe hasa katika shule zetu za kata.
-Ni wakati sasa walimu wetu wakaandaliwa vizuri: tuache kufikiria kuwaandaa walimu wa grade A. Walimu waandaliwe na vyuo vikuu.
-Ni wakati sasa wa kuwapa moyo wale wanaoanzisha vyuo vikuu. Ni investment kubwa sana kuanzisha chuo kikuu. Na dhahiri chuo kikuu hakiwezi kuwa chuo kikuu kwa siku moja. Tunaelezwa Roma haikujengwa kwa siku moja.
-Ni wakati sasa tukawa na mawazo ya kuwa chuo kikuu si majengo makubwa na ya kifahari. Kinachotakiwa ni kuwa na wataalam wataofundisha, na hiyo ndiyo changamoto. Uzoefu wa nchi nyingine ni kuwa vyuo vidogo vinaanza kwa kuwa na ushirikiano (partnership) na vyuo vikuu vingine. Ushirikiano ninaouzungumzia hapa ni ule wa kutoa shahada, siyo chuo kidogo kumezwa na chuo kikubwa. Kwa maana halisi ya partnership, partners wanakuwa na wajibu na haki sawa katika kuendesha programu. Kwa mtindo huu chuo kipya kinapata uzoefu na walimu kutoka chuo kizoefu.

Tuwapongeze na kuwapa nguvu ndugu zetu wa Kisanji University (na vyuo vikuu vipya vyote). Napenda jiografia ya Mbeya. Mbeya ni jiji linalokuwa kwa kasi. Mahitaji muhimu yote yanapatikana hasa kwa sababu ya hali ya juu ya biashara ya mipakani na Zambia, Malawi na Jamhuri ya Kidemokrasia y Kongo.
 
Mie nadhani makanisa yanayoanzisha vyuo vikuu kabla ya kuanzisha angalau vijisekondari vitano yanakosea. Inabidi kujenga tokea kwenye msingi, na sio kuanzia kwenye paa.

Moravian Church wangepashwa kuanzisha Kisanji High School kabla hawajaanzisha Kisanji University. Wasiokuwa na uwezo wa kuendesha high school watawezaje kuendesha vyuo vikuu? These glorified primary schools are not, and will never be universities, no mater what you call them.

Tatizo lako ni kwasababu wewe huyapendi makanisa? au ni nini?, ni kweli una uhakika kuwa rohoni mwako una kiri kuwa "these glorified primary schools are not and will never be universities?" una maana gani, au una chuki binafsi na wana makanisa wanaojitahidi kuanzisha shule. kwani qualities za university ni nini? unafikiri wangeanzisha university bila kuwa na quality?, wao wametafuta hela mpaka wakajenga chuo matokeo yake wewe unatoa wazo kuwa wangefanya hivi mara hivi, si ungetafuta pesa wewe zako uanzishe shule ya secondary ndo baadae ufanye university? hii tabia ya waislam kuwa na wivu na wakristo wanaoanzisha shule ni chafu sana. pamoja na kwamba, ukweli upo palepale, kune st. st. somebody kibao zinaanzishwa kila siku na zitazidi kuanzishwa. na ninyi changamkieni tenda tusikie kuna shule ya shehe fulani, mara shehe Augustine na kadhalika....quiquiquiiiiii, tehehehtehtehteee.
 
Mie nadhani makanisa yanayoanzisha vyuo vikuu kabla ya kuanzisha angalau vijisekondari vitano yanakosea. Inabidi kujenga tokea kwenye msingi, na sio kuanzia kwenye paa.

Moravian Church wangepashwa kuanzisha Kisanji High School kabla hawajaanzisha Kisanji University. Wasiokuwa na uwezo wa kuendesha high school watawezaje kuendesha vyuo vikuu? These glorified primary schools are not, and will never be universities, no mater what you call them.
Augustine Moshi,

Nasikitika kuwa ulizaliwa ukiwa mtu mzima. Maana ungezaliwa ukiwa kichanga kama wengine wanavyozaliwa sina shaka usingetoa maoni kama uliyoyatoa. Kwa faida yako, nakushauri kabla ya kutoa maoni jaribu kufikiri kwanza na ikibidi kufanya utafiti kidogo kwa kutumia google. Ungekuwa umefanya hivyo ungejua historia ya chuo hicho na hali ya usajili wake.
 
Habar kaka masanja, nimeguswa na swala lako la CHUO KIKUU CHA TEOFILO KISANJI UNIVERSITY: Mimi ni mmjoja wa wahitimu wa chuo hiki ulichokitaja mwaka 2010, napenda kukufahamisha kuwa chuo kilianza na wanafunz 200 ambao had kuitimu kwao walifikia 178 wengine hawakuweza kutokana na sababu mbalimbali, sisi tuliofuata tumehitimu 653 kati ya 715.
ok hii haina maana saana kwako lakin nataka kukuambia kwamba ni chuo kinachotambulika saana Tanzania kuliko unavyofikiri labda kwa kukusaidia jaribu kufuatillia ajira zao. kwa sasa mm nipo SUA nasoma Masters mwaka wa kwanza.
 
Back
Top Bottom