Tenga: Jezi ni mali ya mchezaji si TFF

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Tenga: Jezi mali ya mchezaji Taifa Stars

Habari Zinazoshabihiana
• .... Jezi za 'Kikwete' zakabidhiwa TFF 04.01.2007 [Soma]
• Athuman Idd atafune jongoo kwa meno - Tenga 19.01.2007 [Soma]
• Tenga awapasha wachezaji Stars 13.09.2007 [Soma]

*Ampa tano Cannavaro kumvulia jezi Eto'o.

Na Erasto Stanslaus

RAIS wa Shiriksho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amempongeza beki wa timu ya Taifa 'Taifa Stars', Nadir Haroub 'Canavaro' kubadilishana jezi na mchezaji wa kimataifa wa Kameruni, Samuel Eto'o katika mchezo wa marudiano wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika 2010 uliofanyika mjini Younde, Kameruni.

Baada ya mchezo huo kumalizika 'Cannavaro' alifuatwa na Eto'o anayecheza klabu ya Barcelona ya Hispania akitaka wabadilishane jezi baada ya pambano hilo kumalizika ambapo Stars ilichapwa mabao 2-1 yaliyofungwa na mchezaji huyo.

Tukio hilo limeibua mjadala baada ya Ofisa Habari wa TFF, Florian Kaijage akikaririwa na vyombo vya habari akisema 'Cannavaro' atakatwa sh. 20,000 kwa kitendo cha kubadilishana jezi na Eto'o.

Mchezaji mwingine iliyeingia katika mzozo huo ni Jerry Tegete ambaye alibadilishana jezi na mchezaji Jean Makoun wa Kameruni anayevaa 11. Tegete alivaa jezi nambari 10 katika mchezo huo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Tenga alikata mzizi wa fitina na kutoa ufafanuzi wa kina kuhusiana na sakata hilo na alimpongeza beki huyo akisema amefanya kitendo cha kishujaa kutoa jezi ya Taifa bila kujali kama atadaiwa au la.

"Canavaro amefanya kitendo cha kishujaa kwani sasa tunakwenda na wakati kwani angekataa kutoa jezi kwa kuhofia kudaiwa ulimwengu usingetuelewa na kutoa jezi ni kuitangaza nchi," alisema Tenga.

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya Taifa, alisema kuanzia sasa TFF imepitisha uamuzi kila mchezaji wa Stars ataondoka na jezi aliyovaa siku ya mchezo bila kujali alicheza uwanjani au la baada ya pambano kumalizika na itakuwa mali yake.

Tenga alisema kimsingi waliokuwa wakimdai 'Cannavaro' jezi hiyo walikuwa wakitimiza wajibu waliojipangia kati ya uongozi wa Stars na wachezaji lakini alionya kuwa walishindwa kuangalia mazingira halisi ya tukio husika.

Baadhi ya wadau wa mpira wa miguu wameuponda uongozi wa TFF kutokana na kitendo hicho hicho na walikuwa tayari kuwalipia gharama za jezi hizo 'Cannavaro' na Tegete.
 
Hawa TFF nao mmh...

Tunashukuru kwa kufahamu ya ckwamba mliyokuwa mnaongea mwanzo ni aibu tupu...ati mwamdai mchezaji Jersey yake mwenyewe!!!

Bora mmefumbuka macho na kufahamu ya kwamba Dunia inabadilika.
 
Kauli ya leo toka kwa Leodger Chilla Tenga “kila mchezaji wa Stars, atakuwa anaondoka na jezi atakayoitumia kwenye kila mchezo hata kama atakuwa ni mchezaji wa akiba.”
 
Hivi hawa jamaa wa TFF wanamaanisha nini?? kaijage ni msemaje wa yale leodger na Mwakalebela wanayo amua hii kauli ni kweli au kajitoa kimasomaso kufuta aibu???
 
Thamani ya publicity tutakayoipta as nchi kwa mtu kama Etoo kuvaa jezi ya nchi yetu ipo juu sana ukilinganisha na hiyo elfu ishirini. I understand hii yote ni umaskini lakini basi ni vyema umaskini wetu ukawa na kikomo na kuishia kwenye mali tu na si fikra.
 
TFF wameona aibu wanajikosha baada ya wadau kuwazomewa na kushtukia kuwa watachunguzwa TAKUKURU) kwa ubadhirifu wa pesa za wafadhili pamoja na vifaa vya michezo vinavyotolewa na wadau mbalimbali wa michezo na wenye mapenzi mema na taifa stars

ama yawezekana wafadhili wamewakoromea kuhusu vifaa vyote wanavyotoa au wametaka.
 
Alafu jamaa hapo TFF nasikia wamejaza wenyewe tu kutoka kule kanda ya KASKAZINI MAGHARIBI na wadau wamewashtukia kwa hilo na wanasafishana wenyewe kwani hiyo ni AIBU yao
 
Hivi jezi hizo inakuwa sawa na mashuka ya gesti?


Kwa sisi tuliocheza mipira zamani wakati hari ya uchumi bado ni mbaya tunafahamu haya,kwamba jezi ni zaidi ya hayo mashuka ya gesti.
Unavua jezi unapotolewa kumpisha mwenzio aingie na jezi uliyo vaa wewe wakati huo huo.
Ndio maana zamani sio ajabu kukuta timu nzima ina ugonjwa wa UTANGO TANGO
 
TFF wameona aibu wanajikosha baada ya wadau kuwazomewa na kushtukia kuwa watachunguzwa TAKUKURU) kwa ubadhirifu wa pesa za wafadhili pamoja na vifaa vya michezo vinavyotolewa na wadau mbalimbali wa michezo na wenye mapenzi mema na taifa stars

ama yawezekana wafadhili wamewakoromea kuhusu vifaa vyote wanavyotoa au wametaka.
Hapo umesema
 
taifastars01-2-300x228.jpg

KWA kitendo cha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) cha kumshupalia beki mahiri wa Taifa Stars, Nadir Haroub `Cannavaro’ airudishe jeshi ya Taifa Stars aliyompaia Samuel Eto’o Fils, nathubutu kusema shirikisho hili linatupeleka pabaya.

Bila aibu, viongozi wa TFF wanadiriki kuuambia umma wa Watanzania kwamba, lazima Nadir airudishe jezi au awe tayari kukatwa sh 20,000 za Tanzania kufikia jezi hiyo.

Nashukuru kwamba, kabla ya mshangao wao haujafika mbali, wadau wa Zanzibar wamechangishana na kupata fedha sh 110,000 kumlipia Nadir.

Hali kadhalika, wadhamini wakuu wa Taifa Stars, Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) wanaotoa kila mwaka kitita cha sh bilioni moja, nao wamekerwa, wamejitolea kulipa sh 20,000 anayodaiwa beki huyo aliyeifanyia nchi mambo makubwa, kiasi cha Eto’o kumfuata beki huyo wa Yanga na kumsihi ampatie jezi yake ya Taifa Stars mara baada ya mchezo wa marudiano huko Yaounde, Cameroon.

Katika mchezo huo wa kampeni za awali za kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010, Cameroon ilishinda kwa mbinde 2-1, huku ikibanwa mbavu katika mchezo wa kwanza jijini Dar es Salaam kwa timu hizo kushindwa kufungana.

Eto’o, Mwanasoka Bora wa Afrika mara tatu aliyewahi pia kushika nafasi ya tatu kwa ubora duniani, alikiri kwamba, pamoja na kujituma kwa Stars, Nadir aliiokoa kutokana na kucheza soka halisi ya kimataifa na kumnyima pumzi nyota huyo anayeichezea Barcelona ya Hispania.

Kwa hakika, mpenda michezo yeyote angekiona kitendo cha Eto’o cha `kumvulia kofia’ Nadir na hata kuomba ukumbusho wa nyota huyo mwenye asili ya Zanzibar, kuwa cha kishujaa kwa nyota wa Kitanzania na sifa kwa nchi pia.

Mchezaji kama Eto’o kuikumbatia jezi ya Tanzania, halikuwa jambo dogo hata kidogo.

Lakini kwa mshangao wa wengi, TFF ambayo kwa sasa haitumii hata senti moja kuiandaa Stars, zaidi ya kupokea misaada kutoka SBL, Benki ya NMB na wadau wengine, imekuja juu kuidai jezi ya sh 20,000.

Itakumbukwa kwamba, inadai jezi hiyo siku chache baada ya kuvuna zaidi ya sh milioni 500 katika mchezo na Stars, lakini ikijua haijaingia gharama za kutisha kuiandaa timu, ikiwanyonya wachezaji kwa kuwapoza sh milioni moja moja tu.

Inashangaza kwa TFF kukosa shukrani kwa mashujaa wake wanaopigana kufa au kupona kuiletea sifa nchi. Na kweli, kwa kuwabana Cameroon katika mchezo wa kwanza, hadhi ya Taifa Stars na Tanzania kwa ujumla ilipaa ajabu.

Hivi TFF inataka kutuambia nini, kwamba fedha zote za wafadhili zinashindwa kununua jezi?

Au imeamua kuishi kwa ujima wa kuwa na jezi staili ya `Kauka Nikuvae?’

Mbona jezi hizi zinazotumiwa na Stars si za kuinyima usingizi TFF kiasi hiki? Mbona hazina ubora unaotajwa kulinganisha na jezi za nchi nyingine?

Tena katika hili TFF inabidi izinduke na kuangalia ubora wa jezi, na ikibidi ianze kuandika majina ya wachezaji kwenye jezi zao. Mbona hata klabu zetu zinamudu kufanya hivyo?

Tunadhani wakati umefika wa TFF kuangalia mambo makubwa yenye mwelekeo wa kuinua soka yetu, badala ya kuhangaika ni mambo kama haya ya 20,000, tena mpaka kwenye vyombo vya habari.

Rais wa TFF, Leodegar Tenga na wasaidizi wake bila shaka wanapaswa kukuna vichwa na kuangalia ni jinsi gani wanaweza kuzidi kuiamsha soka ya Tanzania iliyozirai tangu miaka ya 1980.

Kwa wafuatiliaji wazuri wa soka la Tanzania, wanafahamu fika kuwa tangu nchi hii ipate Uhuru wake mwaka 1961, hatujawahi kuwa na mafanikio yeyote zaidi ya angalau kushiriki mara moja fainali za Mataifa ya Ulaya za mwaka 1980.

Baada ya hapo timu yetu ya taifa, Taifa Stars, haijakuwa na lolote la maana na katika klabu, ni mara mbili tatu tu ndiyo tuliweza kujitutumia lakini si kwa kutamba kwa ubingwa katika michuano ya barani Afrika.

Tatizo si wachezaji, bali watu wanaopewa dhamana ya kuongoza soka, ni umbumbumbu wa uongozi wa kisoka ndiyo unaotusumbua.
Ndiyo maana tunaona na kusikia vitu visivyopaswa kuzungumzwa katika zama hizi, kama hili la kudai jezi.

Inashangaza kabisa. Hivi viongozi wa TFF ni viongozi wa soka kweli? Ni wanamichezo halisi kweli?

Kuna kosa gani kwa Cannavaro kumpa jezi Eto’o ambaye pamoja na umahiri wake katika ulimwengu wa soka alifikia hatua ya kukiri kuwa Cannavaro ni kiboko hadi kumpa jezi yake kama ukumbusho?

Kwetu tunadhani kitendo cha Eto’o kukiri kuwa Cannavaro ni kiboko, kilipaswa kuchukuliwa kama kichocheo kwa beki wetu huyo apewe moyo zaidi ili ongoze jitihada.

Na alichofanya Cannavaro ni kitendo cha uanamichezo kabisa, leo anaadhibiwa kwa kosa lipi, au ni umbumbumbu wa watu wa TFF?

Kama TFF inang’ang’ania jezi ya Cannavaro, kitu ambacho katika ulimwengu wa soka ni kidogo sana, inaanza sasa kutupa shaka ya mambo mengi.

Maana wana saikolojia husema, aliye mwangalifu na muadilifu katika mambo madogo, huwa hivyo hata kwa makubwa, kwani makubwa hujengwa na madogo. Kinyume cha hivyo ni dalili ya kuwepo matatizo.

Chanzo:
logo.gif
 
The Tanzania Football Federation (TFF) has reversed its decision to impose a financial penalty on a player who swapped jerseys with Samuel Eto'o.

Defender Nadir Haroub gave away his jersey to the Cameroon star after the teams' recent World Cup qualifier in Yaounde.

Tanzania lost a hard-fought encounter 2-1 and the local media praised Haroub and said his performance was the reason Eto'o was keen to swap jerseys with him.

But the TFF bigwigs were clearly not amused by the gesture and told Haroub that part of his allowance would be used to replace the jersey.

The team's management insisted that Taifa Stars players were not allowed to give away jerseys as the federation could not afford a new set of jerseys for each match.

But following criticism from the media and fans alike, the TFF has backtracked and said the player would not be punished.

"It's obvious he couldn't say no to Eto'o," said TFF president Leodegar Tenga.

"It was a wise decision to give his jersey to such a famous player. This will make our country known," he added.

A fund-raising drive was already underway with fans donating money to help Haroub meet the cost of replacing the jersey.
 
Kwa sisi tuliocheza mipira zamani wakati hari ya uchumi bado ni mbaya tunafahamu haya,kwamba jezi ni zaidi ya hayo mashuka ya gesti.
Unavua jezi unapotolewa kumpisha mwenzio aingie na jezi uliyo vaa wewe wakati huo huo.
Ndio maana zamani sio ajabu kukuta timu nzima ina ugonjwa wa UTANGO TANGO


...Mkuu, Hujatulia! nimecheka!!!!!
 
Kwa sisi tuliocheza mipira zamani wakati hari ya uchumi bado ni mbaya tunafahamu haya,kwamba jezi ni zaidi ya hayo mashuka ya gesti.
Unavua jezi unapotolewa kumpisha mwenzio aingie na jezi uliyo vaa wewe wakati huo huo.
Ndio maana zamani sio ajabu kukuta timu nzima ina ugonjwa wa UTANGO TANGO
....Yawezekana Kaijage anataka kutudisha....
 
Is shame to collect the jersey and reuse especially for the big game like that with Cameroun. If possible all the players should have changed tha jerseys with those of indomitable lions the image of african football. Is better to come back and pay rather than letting a golden chance of exchanging with Etoo to pass away. In one way or another you have advertised Tz outside there.
 
ukweli ni huu, walichotakiwa kufanya TFF ni kuitisha mkutano na waandishi wa habari kisha watueleze ni sababu ipi iliyopelekea timu kushindwa kufuzu kwa mara ya pili katika mashindano ya africa then kwa nini timu imeshindwa kwenda FNB south africa 2010, but walichokiona wao ni kuwa wakija na gea ya jezi wabongo hawatawauliza kwa nini timu haina maendeleo...na kama mlivyoona waandishi woote wakakimbilia ishu ya jezi na kusahau ile ya muhimu
 
Back
Top Bottom