Mbwa Mpole
Member
- Jul 18, 2012
- 11
- 1
Baada ya kuuawa kwa Mwangosi Tendwa kama kawaida yake alikurupuka na kutoa kauli za utata na zisizo na umakini dhidi ya CHADEMA. Kama Tenwa alikilaumu CHADEMA kwa vurugu aone sasa UVCCM, sijui mpaka afe mtu ndio inaitwa vurugu na kuhatalisha amani. Aidha, nadhani tendwa anasoma magazeti kujua madai ya rushwa inavyodaiwa kutawala katika chaguzi za CCM. Pamoja na haya yote sijamsikia Tendwa bingwa wa kukurupuka akiongea na vyombo vya habari kuhusu rushwa na vurugu katika chaguzi za CCM. Sasa sijui amejifunza na kuacha kukurupuka, au anakiongopa chama tawala ambacho ni mwajili wake, au ndio tuseme ni kweli huwa anawaonea wapinzani kwa kuwashambulia harakaharaka bila hata ya kuchunguza ukweli wa mambo na hali halisi.