Elections 2010 Tendwa atabiri viti 100 vya ubunge kwenda upinzan

Jamani Utabiri sii lazima utumie bao, mtu yeyote anaweza kutabiri kisayansi na ikakubalika kutokana na statistical patterns.
Kwa hiyo alichofanya Tendwa ni kutazama Upinzani ulivyojipanga hadi sasa na kuzungumzia ushindani uliopo. Hata JK mwenyewe rais na mgombea anaweza kukiri kwamba safari hii kuna uwezekano mkubwa wa Upinzani kuzoa viti bungeni.

Kwa hiyo hata mtu anayetakiwa kuwa na kuonyesha neutrality kwa mujibu wa kazi yake ni sawa kutabiri?

Utajisikiaje referee wa mechi ya Simba na Yanga kabla ya mechi akisema anatabiri Yanga itafungwa 4-1 ? Wewe kama mpenzi wa Yanga utakuwa na imani na huyu referee ?

Unanikumbusha kuna hadithi moja ya Science Fiction ya Isaac Asimov (Franchise), in some futuristic (then, 1950's future being the 2008 election) United States society watu wameweza, kwa kutumia computer inayoitwa Multivac, kumpata mtu mmoja ambaye input yake ndiyo iko most representative of the whole population, sasa badala ya kila mtu kuhangaika kupiga kura, wanaona inatosha huyu mtu mmoja tu apige kura. Mtu huyu anaitwa Norman Muller.

Inaonekana Tendwa ana Multivac yake huko ofisini kwake, na kashajichagua yeye mwenyewe kuwa Norman Muller wetu, kesho na keshokutwa anaweza kutuambia tuahirishe uchaguzi kwani "patterns and statistics" zote anazo.

Chicago Tribune wenzake walitumia statistics hizo hizo kumtangaza gavana Dewey kumshinda Truman katika uchaguzi wa rais wa Marekani mwaka 1948, ending with the legendary picture of Truman celebrating sarcastically with a paper carrying the headline "Dewey defeats Truman".

E868A_dewey_defeats_truman.jpg
 
Kwa hiyo hata mtu anayetakiwa kuwa na kuonyesha neutrality kwa mujibu wa kazi yake ni sawa kutabiri?

Utajisikiaje referee wa mechi ya Simba na Yanga kabla ya mechi akisema anatabiri Yanga itafungwa 4-1 ? Wewe kama mpenzi wa Yanga utakuwa na imani na huyu referee?
Mkuu wangu refarii ni mchezeshaji mpira ukiwa uwanjani, sii sawa na wadhifa wa Tendwa, lakini kiongozi wa TFF (Tenga) au wa FIFA anaweza kutabiri pamoja na kwamba wao ndio wasimamizi wa mchezo huu. Na hakika sintajisikia vibaya isipokuwa nitawaomba hao Yanga wayasome vizuri mapungufu yetu ili tukiingia Uwanjani iwe maajabu.
 
Mkuu wangu refarii ni mchezeshaji lakini mtu wa TFF (Tenga) au FIFA anaweza kutabiri pamoja na kwamba wao ndio wasimamizi wa michezo. Na hakika sintajisikia chochote kibaya isipokuwa nitawaomba hao Yanga wayasome vizuri zaidi mapungufu yetu ili tukiingia Uwanjani iwe maajabu.

Watu wanatakiwa kuwa na confidence na neutrality ya Tendwa, akishaanza kuweka vi personal observation vyake ana undermine neutrality yake na watu wakikosa imani na neutrality yake watakuwa justified.

Kesho keshokutwa akisema "pingamizi la CHADEMA lina mantiki" CCM wataweza kusema Tendwa ana bias ya upinzani kwa sababu alishasema wapinzani watapata viti mia.

Au akisema "pingamizi la CHADEMA halina mantiki" CHADEMA wanaweza kusema Tendwa ni kada wa CCM ndiyo maana alisema CHADEMA hawawezi kushinda majority.

Kauli hizi zinatengeneza controversy bila sababu.

Ingefaa asikilize ushauri wa Al Capone "You got an all-out prize fight, you wait till the fight's over, one guy's left standing, and that's how you know who won - Alphonse Capone"

Hakuna vi speculation kabla ya prizefight, nchi nyingine zinazojua integrity of office mtu unaweza kutolewa kazini kwa vi speculation kama hivi.
 
Kiranga,
Hivi kweli unataka kunambia Tendwa anatakiwa kuwa neutral kwa sababu ya hofu ya udaku wa watu ati atakuwa napendelea Chadema!. Maamuzi yoyote ya Tendwa kikazi yanatakiwa kufuata sheria na sio utashi wake yeye na pengine kwa kuchukua mtazamo huu ndio maana umeshindwa kuelewa kwamba Tendwa anachotakiwa kufuata ni sheria inavyosema anapokuwa kazini lakini pia kama raia mpiga kura anaweza kuchangia mada yoyote ya kitaifa.
Mangapi kayasema au kuyafanya yakilenga kuwanufaisha CCM tena nje ya sheria lakini hili limetokea la kutabiri na sio kupendelea Chadema imekuwa kavunja sheria ati alitakiwa kuwa neutral..
Hii neutral inapimwa vipi? kwa maneno au kufuata sheria pasipo kupendelea upande mmoja..
 
Kiranga, Hivi kweli unataka kunambia Tendwa anatakiwa kuwa neutral kwa sababu ya hofu ya udaku wa watu. Maamuzi yoyote ya tendwa yanafuata sheria na sio utashi wake na poengine kwa kuchukua mtazamo huu ndio maana umeshindwa kuelewa kwamba Tendwa anachotakiwa kufuata ni sheria anapokuwa kazini lakini pia kama raia mpiga kura anaweza kuchangia mada..Mangapi kayasema au kuyafanya yakilenmga kuwanufaisha CCM tena nje ya sheria lakini limetokea la Chadema imekuwa kavunja sheria ati alitakiwa kuwa neutral..
Hii neutral inapimwa vipi? kwa maneno au kufuata sheria pasipo kupendelea upande mmoja..

Tendwa anatakiwa ku deal na facts, si speculations. Tendwa inaonekana anapenda sana ku deal na speculations, juzi watu wamemuuliza kuhusu pingamizi la CHADEMA, kabla hata pingamizi halijaletwa na kuwa fact, yeye kaanza ku entertain maswali kuhusu pingamizi hewa na hypothetical situiations, ukikutana na mwanasheria kabambe anayejua kazi yake anakupa jibu short and clear "My office does not deal with speculations, let something happen then we can discuss it".

Sasa kwa sababu Tendwa kashaanza ku entertain speculations, tukimuuliza aangalie kwenye crystal ball lake na kutuambia hivyo viti 100 vitatoka wapi na wapi, nani atashinda na nani atashindwa ataweza kutujibu? Kama hataweza kwa nini ajue viti 100 na si viti halisi? Kwa nini 100 na si 90 95 au 97? Au kachagua namba 100 imemvutia kwa sababu ya 1 na sifuri mbili?

Watu kama Tendwa ni wa kuogopwa sana kwa sababu next thing you know, anakuwa na pressure ya kutaka kupatia, "utabiri" wake uwe right, who is to say hatafanya jitihada kwa kutumia influence ya ofisi yake ili utabiri wake uwe sawa ?

Ukiangalia kwa sana unaona utabiri huu unaleta matatizo mengi kuliko unavyotatua.
 
Tendwa should stay out of this prediction business...it's inappropriate for him to do that
 
Tendwa anapotokea mbele ya waandishi wa habari na kuanza kutoa matamshi ambayo yanayohusu matokeo ya mambo kama ya uchaguzi, anakuwa anakosea sana. Anakosea kwasababu, anataka wananchi wenye uelewa mdogo kuamini kuwa utabiri wake una ukweli na hata ikitokea rigging, wasichukue hatua zozote.

Tendwa hana mamlaka ya kutabiri matokeo ya uchaguzi. Kura yake ni moja na haitoshi kusababisha kuwe na viti 100 kwa upinzani wala kwa CCM. Ni vyema akae kimya na kutatua matatizo ya vyama kama ilivyowekwa kwenye Job Description yake. La sivyo, anaweza kujizolea lawama za bure.

Masuala ya uchaguzi ni masuala sensitive sana.

Ni vigumu kwangu kuamini kuwa utabiri wake una base yoyote ya kisayansi. Nadhani amekurupuka na kutamka tu. Na matamshi yake yana madhara makubwa zaidi kwa upinzani kuliko kwa CCM. Ikitokea kuwa CCM wameshindwa kwa viti vingi na hata kupoteza kiti cha urais, na wananchi wakiamini utabiri huo, ni rahisi kwa CCM kuupora ushindi na kujitetea kuwa ushindi wao uliwahi kutabiriwa pia na Msajili wa Vyama vya siasa.
 
mi nawait amwengue kikwete kugombea la sivyo hakuna democrasia mbona chadema walienguliwa bila manoma?hivi masha alidanganya kwenye pingamizi lake eti eeeeh
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom