Charles Ignatio
Senior Member
- Oct 9, 2010
- 133
- 52
Mimi nashindwa kuelewa huu ni utamaduni gani ambao wanasiasa wamejiwekea, wa kunywa maji wakati wakitoa hotuba mbalimbali, mimi naweza kuwa nyuma na wala sina sayansi iliyopo lakini msingi wake siuelewi mfano mzuri ni Rais wa Nchi JK anapenda sana kunywa maji na kukatisha hotuba mara kwa mara, Je ni kwamba kuongea ni kazi nzito sana au? na kama kuongea kwa muda mrefu ndio kunawafanya watu hawa kunywa maji sana, hapa sitakubali kwani mbona watu wanaohubiri makanisani na majukwaani kwa muda mrefu kama Mzee wa upako hawanywi maji ovyo ovyo? Hilo pia halitoshi Mr. Budget Mkulo alionekana akikatisha sana hotuba yake, Kwa zaidi ya mara 5 na kuelekeza tension yake kwenye glasi ya maji, duu mpaka ilinishangaza, sasa wadau naomba mnipe ufafanunuzi wa siri iliyomo kwenye hiyo glasi ya maji, au yale huwa sio maji.?? Au yanaongeza konfidensi? Mbona walimu wanaofundisha zaidi ya madarasa matano hawaruhusiwi kunywa chochote wakati wanafundisha? au wanaadress kitu chochote