Mbona number haipatikani?
Ni mt'hani mkubwa,wakati mwengine uzazi huwa faraja kwa mzazi ila hali kama hii mzazi hujikuta akijuta na kujilaumu nafsi yake,kama mumewe alifariki akiwa tayari na ujauzito huo ajaribu kuomba msaada kwa watu hata mashirika mbalimbali kama sivyo basi huyo aliempachika huo ujauzito atafutwe aubebe msalaba wake.
HaipatikaniNa imeandikwa hapo, soma acha uvivu.
Kwa nn husomi ukaelewa unakimbilia kuumbua mtu. Kuwa na busara kidogo.Mkuu habar yako ipo nusu.. huyo mjane hao watoto aliowapata ni wa marehem mume wake kwa maana kwamba alifarik akiwa mjamzito? Au ni wa jamaa tu alijitokeza kumfariji mjane mwishowe faraja ikaleta mimba....
Dah, amshukuru Mungu, wengine tunataka hizo fursa!Ashura Shaibu, aangua kilio hospitali baada ya kujifungua mapacha wanne na akifisha watoto 8, adai yeye ni mjane hataweza kuwalea.
-----------------
Dar es Salaam. Hali ya umaskini pamoja na kufikiria namna ya kuwalea watoto wanane baada ya kujifungua wanne jana imemtoa chozi mkazi wa Yombo, Ashura Shaibu (37).
“Lakini nilipatwa na mshtuko baada ya kujifungua watoto wanne kwani ni jambo ambalo sikulitegemea,” alisema
Ashura alijifungua watoto hao katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke, lakini mzazi huyo hakufurahia tukio hilo kwa kuwa haikuwa matarajio yake ikizingatiwa kwamba familia yake ni maskini.
“Nilifurahi kusikia nimejifungua watoto wanne ingawa mume wangu amekwishafariki na sina mtu wa kunisaidia kwani hata mama yangu anaishi mbali na mimi na wazazi wa mume wangu wamekwishafariki,” alisema Ashura.
Mume wa mama huyo alifariki Desemba mwaka jana wakati akiwa mjamzito.
Alisema hali yake kiuchumi si nzuri kwani kabla ya kupata ujauzito, alikuwa akijishughulisha na biashara ndogo ndogo katika eneo la nyumba yake lakini mimba ilipofikisha miezi minne, alichoka na kushindwa kumudu shughuli zake na biashara.
“Nina maisha magumu, nina watoto wanane, sijui namna nitakavyowalea,” alisema.
Muuguzi katika wodi ya watoto wenye upungufu wa uzito Hadija Kamote anasema mama huyo alijifungua kwa njia ya kawaida ila watoto walionekana kuwa na uzito pungufu.
“Watoto wamezaliwa wa kiume watatu na wa kike mmoja. Wa kwanza ana uzito wa kilo 2 na gramu 300,wa pili ana uzito wa kilo 1 na gramu 900, wa tatu ana uzito wa kilo 1 na gramu 700 na mtoto wa nne ana uzito wa kilo 1 na gramu 300,” alisema Kamote.
Muuguzi Mkuu katika Hospitali ya Temeke Deodata Msoma alisema mama huyo baada ya kujifungua alionekana kukata tamaa na kuanza kulaumu kwanini amepewa watoto hao.
“Ilibidi tufanye kazi ya kumtuliza na kumtia moyo kuwa asikate tamaa na kumuambia wapo watu watakaomsaidia huku tukijaribu kufanya vitu vitakavyo mfurahisha na kurudisha tabasamu usoni kwake,” alisema Deodata. Atakayeguswa kumsaidia Ashura afanye hivyo kwa kutumia namba 0783- 287929.
Chanzo: Mwananchi
itawezekanaje uwe wewe wakati papuchi yako umehamua kuwapa nyenyere?!natamani ingekuwa mimi
Mungu kwa kweli kambariki huyu mama, mme wake atakuwa anafuraha sana huko alipo, it's a shame hajafanikiwa kuwaona.natamani ingekuwa mimi
unataka nilale na kila mtu?itawezekanaje kuwa wewe wakati papuchi yako umehamua kuwapa nyenyere?!
Wasiliana na mtoa madaHaipatikani
Suala la mapacha liko katika mayai, sio mbegu za kupevusha mayai, hivyo mapacha hutokana na mwanamke sio mwanaume, pia ni kitu cha urithi. Kama upande wenu ndugu zako wa kike wana historia ya mapacha na zaidi basi yawezekana nawe ukawa ktk list.unataka nilale na kila mtu?
Mkuu sisi maskini huwa tunaamini watoto ndio utajiri wetu.Ni mjinga kweli, yaani una watoto wa nne lakini bado unazaa? jamani
Yani wewe hata habari hujaisoma umekimbilia kutoa ushauriSasa mjane si atunzwe Na alie mzalisha au Mume alifariki akiwa mja mzito
Kwani ukisoma ukaelewa utapata hasara gani au unaongozwa na ulivyo na roho ya chuki au huna hata mtoto unatamani mimba ungepewa wewe!Sasa mjane si atunzwe Na alie mzalisha au Mume alifariki akiwa mja mzito
Hakuna kitu kama hicho.Mkuu sisi maskini huwa tunaamini watoto ndio utajiri wetu.
Shame?????Mungu kwa kweli kambariki huyu mama, mme wake atakuwa anafuraha sana huko alipo, it's a shame hajafanikiwa kuwaona.