Temeke, Dar: Ili upige muziki kwenye sherehe/shughuli utapaswa kulipia elfu 50 ya kibali

Wanachomaanisha ni kuwa wamepandisha gharama za hizi shughuli.Yaani kama MC alikuwa analipwa TZS 25,000/= akienda kweye shughuli ya mnyonge kama vile kipaimara sasa itabidi alipwe TZS 75,000/= ili yeye aweke mfukoni 25,000/= na 50,000/= alipie kodi.Tafsiri yake ni kwamba wanyonge hawataweza kuwafanyia wapendwa wao sherehe tena!
Hiki ndicho kitakacho tokea

Na chakushangaza zaidi mbona hao wapishi na wapiga picha wakati mwingine malipo yao huwa hayazidi hizo tozo walizoziweka au walikuwa wanzungumzia watu gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni sawa kabisa! Unakuta sherehe kwa mfano ya harusi au sendoff watu mnachangishwa kila kichwa elfu hamsini mpaka laki moja,!

Unakuta sherehe moja tu ina gharimu mpaka milioni 10.

Unakuta kwenye bajeti ya sherehe eti
Mapambo milion 1.5
Ukumbi milion 1.2
Mc na music milioni 1.8
Picha na video milioni 1.6
Vinywaji milioni 1.7
Chakuala milion 4

Na hizi ni sherehe tu za uswahilini bado za ushuani ndio balaa

Unakuta mtu ana maisha magumu lakini akipewa kadi ya mchango anajipinda mpaka ipatikane, tena wanakuwekea masharti kabisa single 80,000 double 150,000.


Tena hili suala lilialamikiwa sana humu kwama ifike hatua hawa watu walipe kodi.

Walipe tu kodi aisee.
Hebu oneni jamani
 
Sherehe zatakiwa kulipiwa kodi au Mc na wapishi wa masherehe watakiwa kulipa kodi?
... nina kashughuli kangu ambako MC amekubali kunifanyia bei ya kishikaji elfu 25. Lakini anatakiwa alipie elfu 50 kodi. Kodi itakuwa imelipw na mimi mwenye shughuli au MC?
 
Sherehe nyumbani na kodi wapi na wapi
Wataanza hadi unyago na ngoma za mashetani
Kwa hiyo nyumbani chakula umejinunulia mwenyewe sokoni

Kuku umewatoa banda kwako la kuku ufanye kasherehe ka mtoto kutoka jando

MC mjomba wa mtoto unaenda dai kodi?

Huo ni uhuni kwa sherehe za krimasi na iddi zinszofanyika majumbani watu wanawake hadi mahema mtafuata kodi?

Watu wakiwa wana sherehe ya kupokea mahari au barua ya uchumba mtaenda? Huo ni udhañimu
 
... nina kashughuli kangu ambako MC amekubali kunifanyia bei ya kishikaji elfu 25. Lakini anatakiwa alipie elfu 50 kodi. Kodi itakuwa imelipw na mimi mwenye shughuli au MC?
Kwani unapoajiriwa ukalipwa chini ya kiwango cha mshahara kinachotakiwa kulipiwa kodi huwa tofauti analipa mwajiri?
Hiyo kodi analipa mc kwa sababu ni kipato kwake, kama hastahili kuilipa basi yatatolewa maelezo.
 
Hii sasa kali. Migambo itakuwa inachungulia madirishani kujua kama ndani kuna sherehe au la!!!!.
Ila katika ufafanuzi mwenye sherehe hajaguswa. Je nikifanya bila kumwalika MC, mpishi nitadakwaje?
Itabidi kukaa na mishale ndani ya nyumba. Nimealika ndugu zangu nyumbani kwa dinner ya kumpongeza mwanangu kupata kipaimara, nione dodoki linachungulia dirishani, mshale wa shingo. Hawa ndio vibaka wenyewe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom