Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,023
- 18,563
Jamani tembo si wa kuchezea. Kuna kipindi wanawake fulani walimkuta kasimama barabarani, wakampigia honi, aliifuata gari yao akavunja kioo cha mbele akamchomoa dereva na kumuua. Abiria wengine wakatoka kwenye gari na kukimbilia porini.
Juzi hapa katika mbuga moja Afrika Kusini watalii walishambuliwa na tembo waliyemkuta barabarani. Walipaki pembeni ili apite, na tembo akajifanya anapita, lakini ghafla akaenda nyuma ya gari na kuibetua!