shatisuruali
JF-Expert Member
- Jul 28, 2016
- 888
- 2,636
kwa kuongezea tu kama wadau hapo juu walivyo jaribu kufunguka... Picha hizi unazoziona katika google map hazitoki kwa google wenyewe. Kuna satellite za aina nyingi sana mfano za hali ya hewa (weather satellite) hizi hutumika kwa ajili ya kutabiri na kuonesha hali ya hewa dunia nzima. Kuna zile zinazomilikiwa na jeshi hasa la marekani na mataifa makubwa (millitary satellite) ambazo zipo special kwa ajili ya mambo mengi sana hasa mawasiliano na kupiga picha huku duniani hasa za upelelezi na ulinzi. Picha za dunia hupigwa na satellite za jeshi, hawa huwa wanaamua kipi kifutwe kipi kiachwe katika ramani, mfano kuna sehemu za siri kama makambi ya jeshi, meli zao baharini, silaha za kivita, sehemu za majaribio ya makombora. Wakisha chuja na kutoa kila kitu ambacho raia wa kawaida haruhusiwi kuona ndo huwa wanawauzia makumpuni ya ramani kama google, bing na kadhalika. Ndo maana kuna baadhi ya sehemu nyeti huwezi kuziona google map na inachukua muda kupiga picha, kuziprocess na kuziachilia kwenye public. Hope nimeongeza kitu.