Tegeta wafa na kiu huku wamezungukwa na tanki la dawasco!!!

Am I Crazy?

Member
Jan 12, 2009
10
2
Wakazi wa Tegeta eneo la wazo hill wamelalamika kwa ukosefu wa maji safi huku wakiishi mita chache tu kutoka lilipo tanki kubwa la dawasco. Jana nilikuwa maeneo ya huko, eneo maarufu kama ''mkorosho bangi'' na kushuhudia jinsi wananchi wanavyopata shida ya maji huku tanki kubwa la kusambaza maji likiwa jirani kabisa na makazi yao!!

Baadhi ya wakazi niliozungumza nao walidai kuwa tanki hilo linasambaza maji maeneo ya mbezi, mikocheni na masaki huku wao wakiambulia patupu mbali na kuwa jirani na lilipojengwa tanki hilo.

Waliongezea kusema kuwa walishatuma maombi DAWASCO kuomba kusambaziwa maji, lakini hawakupata jibu lolote la kuridhisha zaidi ya kuona mabomba makubwa yakitandazwa kuelekea mbezi na masaki.

Wananchi wa huku hutegemea maji ya kununua kwa watu binafsi waliochimba visima ambapo hununua ndoo moja kwa shilingi 200!!! ''Tumechoshwa na kununua maji ya chumvi kwa gharama kubwa huku tukiwa karibu kabisa na tenki la maji, tunaomba serikali kupitia dawasco watuunganishie maji ili tuweze kupata maji safi, uwezo wa kulipa bili tunao'' alisema mwananchi mmoja.


Swali kwa Dawasco: Je hii ni sawa?????????
 
Wakazi wa Tegeta eneo la wazo hill wamelalamika kwa ukosefu wa maji safi huku wakiishi mita chache tu kutoka lilipo tanki kubwa la dawasco. Jana nilikuwa maeneo ya huko, eneo maarufu kama ''mkorosho bangi'' na kushuhudia jinsi wananchi wanavyopata shida ya maji huku tanki kubwa la kusambaza maji likiwa jirani kabisa na makazi yao!!

Baadhi ya wakazi niliozungumza nao walidai kuwa tanki hilo linasambaza maji maeneo ya mbezi, mikocheni na masaki huku wao wakiambulia patupu mbali na kuwa jirani na lilipojengwa tanki hilo.

Waliongezea kusema kuwa walishatuma maombi DAWASCO kuomba kusambaziwa maji, lakini hawakupata jibu lolote la kuridhisha zaidi ya kuona mabomba makubwa yakitandazwa kuelekea mbezi na masaki.

Wananchi wa huku hutegemea maji ya kununua kwa watu binafsi waliochimba visima ambapo hununua ndoo moja kwa shilingi 200!!! ''Tumechoshwa na kununua maji ya chumvi kwa gharama kubwa huku tukiwa karibu kabisa na tenki la maji, tunaomba serikali kupitia dawasco watuunganishie maji ili tuweze kupata maji safi, uwezo wa kulipa bili tunao'' alisema mwananchi mmoja.


Swali kwa Dawasco: Je hii ni sawa?????????


Nimeona niweke na picha ya hilo tank ili ambao hawajawahi kuliona wajionee wenyewe!

am-i-crazy--albums-my-photos.html
 
Back
Top Bottom