Technolojia iliyotumika hapa

Njunwa Wamavoko

JF-Expert Member
Aug 11, 2012
5,745
2,338
Nina Mdogo wangu yuko chuo(jina nimeifadhi) baada ya kupokea hela ya field,research etc akapiga hesabu kile kiasi extra akakitenga na akatunza ili naye aje kumiliki Samsung S4 na Apple iPad
Basi katika pita pita yake mtaani akakutana na Samsung S4 used na sio clone na jamaa akamwabia kumuuzia 400,000/= basi jamaa akakubali simu ilikuwa katika Good condition kabisa tena ikiwa na charger yake na USB yake...Wakapanga wakutane siku fulani ili waweze kubidhiana hiyo mali basi dogo kailipia na kitu cha kwanza kaja kunitambia kuwa naye kashika S4 basi nikampa pongezi

Kumbe hiyo simu ilikuwa imeibiwa check kimbimbe chake sasa ikatokea simu moja kuna Manzi moja ikawa inamtumia message ikidai inasomea IFM inmfahamu dogo wangu na ingependa wakutane siku....check trick hiyo ya FBI vile kwa kuwa washamjua mwanachuo basi ikabidi waitumie jinsia ya kike itakayojidai mwanachuo ili waweze mkamata huyo dogorasi wangu...Siku waliyokuwa wamepanga ikafika na MANZI Ilimfuata chuo ile anatoka tu nje ya geti la chuo akakutana na hiyo mchuchu wakawa wanasogea ile wanaongea mara wakatokea POLICE wakamuuliza ONESHA SIMU yako simu akanyanganywa akapigwa Pingu akapelekwa Police kujibu mashitaka hiyo simu alitoa wapi...
Thank God aliachiliwa juzi tu hapa baada ya kunyea debe week moja kumbe in short hiyo simu walikuwa wanai-TRACK

:focus::focus: Sasa wataalamu wa simu emu tujezeni jamaani maana Mm smartphone zangu zimeibiwa nyingi tu ila hii technolojia ya ku-track simu sijajua unafanya je au Protocol gani unafuata maana DOGO kanambia leo hii mpaka na-post hii thread kuwa kuna mwingine alinunua Ipad tena dukani iliyo used na yeye amekamata akajitetea alinunua DUKA fulani huko kwao duka wanali-trace alisomeki tena linamilikiwa na mtu mwingine....Dogo mwingine wanasoma wote kaibiwa S3 lkn ameweza kuikamata tena huko Morogoro wakati imepotelea DAR
Sasa wakuu tusaidiane Ili Tuweze Ondokana na hili janga la wezi wa smartPhone....Protocol gani inafutwa I see maana kama sielewi kitu ninachoelezewa

SAMAHANI KWA SIASA NYINGI LKN HOPE NIMETENGENEZA SCENARIO ILI MUWEZE KUNIELEWA
 
kwa apple kuna huduma ya find my phone ambayo ni kama impossible kwa mtu wa kawaida kuweza kui bypass. ukiiba simu kwa kutumia ramani watakuona kila unapoenda.

kwa hizi galaxies huduma hii pia ipo ila sio impossible kui bypass kama unavyojua android ina matundu mengi tu hivyo ni rahisi kuchakachua

huyo dogo atakua hakubadili kitu hivyo ikawa rahisi kwa mwenyewe kuitrack.

_UKWO_IFH-B9JUFoFKlfbm2uBnuvLoWPkKmgrrxegjpuUnf8vGdO65YRPZk54n1Mfuw=h310-rw
 
Mkuu hii kitu ipo namshukuru mungu amenisaidia sana maana jana niipata s4 yangu niliyokuwa nimeibiwa juzi pale Ubungo nilikuwa nashuka tu kwenye dala2 saa 11 alfajiri ili kupanda basi za mikoani jamaa walinizunguka mmoja kajarib kunichomoa wallet kugeuka nyuma sim sina ktk mfuko wa shati nikajua imekwenda nikapanda basi nikaondoka nafika Morogoro km saa 4 hivi nikapata mes ktk sim yangu nyingine niliyobypass no ya sim inayotumika ktk sim yangu ilibidi nishuke pale Morogoro nianze kufuatilia nikajarib kutuma tigopesa nikapata jina la yule bwana nikapanda hewani kumueleza akashangaa kishenzi kadai kuna washikaji wamekuja kwake kuijarib inshort niliinstal app inaitwa eset mobile security hii unasajili line yako tu mtu akitoa yako akaweka ingine sim inajibrock sametime inatuma taarifa ktk no yako uliyobypass pasipo yeye kujua no anayotumia na serial no ya sim yako pia s4 nayo ina program ya sim change alert hivyo ikabidi siku hiyo nirudi dar jana nikakutana naye jamaa kiulafiki kadai mdogo wake aliokota akamuuzia kwa 180000 ilibidi nimtoe 140000 maana alikuwa ni mjeda yuko pale mbagala kambi ya jeshi akanikabidhi sim yangu lkn naona hao vibaka wanawatumia hao wajeda ili wawalinde ktk dili zao
 
kuna mshikaji wangu alinunua ipad huko zenji. kumbe imeibiwa kwa mtangazaji wa cnn. kudadadeki. dogo aliijiwa dodoma. afu alishaileta kwangu niijailbreak sijui nimuwekee vitu gani...
jamaa walimlocate dodoma ghetto anapokaa ambapo hata mimi ukinielekeza sifiki.
mwenye ipad alikuwa mkali kudadadeki chezea wazungu. alidai alipwe fidia la sivyo kesi iende mahakamani. polisi wakambeba dogo mpaka dar. akakaa lockup wiki wakampa laki saba fidia na kurudisha ipad ikawa settled. dogo akaachiwa. hana hamu na vitu used.
 
kuna mshikaji wangu alinunua ipad huko zenji. kumbe imeibiwa kwa mtangazaji wa cnn. kudadadeki. dogo aliijiwa dodoma. afu alishaileta kwangu niijailbreak sijui nimuwekee vitu gani...
jamaa walimlocate dodoma ghetto anapokaa ambapo hata mimi ukinielekeza sifiki.
mwenye ipad alikuwa mkali kudadadeki chezea wazungu. alidai alipwe fidia la sivyo kesi iende mahakamani. polisi wakambeba dogo mpaka dar. akakaa lockup wiki wakampa laki saba fidia na kurudisha ipad ikawa settled. dogo akaachiwa. hana hamu na vitu used.

Nakutafuta kumbe upo huko ... Hebu cam this way bana huoni kibarid cha usubuhi usubuhi???
 
jamani mm nillivamiwa like one month ago. wakaiba vitu vyangu vingi ikiwemo s3 na bb. mm nilipuuzia nikaona itz gone. ilavjananimekutana na askari akanishauri kuna kitengovcha polisi kwa kushirikiana na service provider wa mtandao wanaweza kui trace cm hata kama wanei flash! leo naenda kuanza mchakato nitarudi na feedback eapendwa maana jamaa kanitia moyo sana
 
Mkuu hii kitu ipo namshukuru mungu amenisaidia sana maana jana niipata s4 yangu niliyokuwa nimeibiwa juzi pale Ubungo nilikuwa nashuka tu kwenye dala2 saa 11 alfajiri ili kupanda basi za mikoani jamaa walinizunguka mmoja kajarib kunichomoa wallet kugeuka nyuma sim sina ktk mfuko wa shati nikajua imekwenda nikapanda basi nikaondoka nafika Morogoro km saa 4 hivi nikapata mes ktk sim yangu nyingine niliyobypass no ya sim inayotumika ktk sim yangu ilibidi nishuke pale Morogoro nianze kufuatilia nikajarib kutuma tigopesa nikapata jina la yule bwana nikapanda hewani kumueleza akashangaa kishenzi kadai kuna washikaji wamekuja kwake kuijarib inshort niliinstal app inaitwa eset mobile security hii unasajili line yako tu mtu akitoa yako akaweka ingine sim inajibrock sametime inatuma taarifa ktk no yako uliyobypass pasipo yeye kujua no anayotumia na serial no ya sim yako pia s4 nayo ina program ya sim change alert hivyo ikabidi siku hiyo nirudi dar jana nikakutana naye jamaa kiulafiki kadai mdogo wake aliokota akamuuzia kwa 180000 ilibidi nimtoe 140000 maana alikuwa ni mjeda yuko pale mbagala kambi ya jeshi akanikabidhi sim yangu lkn naona hao vibaka wanawatumia hao wajeda ili wawalinde ktk dili zao

Ngoja nianze na hii maana wale wenzi wa njaa njaa afu watu mnaishi wote lazima niwafume hapa
 
mpenzi niko mwanza. ila now niko kwenye basi nna kijisafari kidooogo... i will be home before xmas. i miss you my dear wife

Miss u too... ukirudi lemme know!!!!!!!! :A S kiss::A S kiss:
 
kwa apple kuna huduma ya find my phone ambayo ni kama impossible kwa mtu wa kawaida kuweza kui bypass. ukiiba simu kwa kutumia ramani watakuona kila unapoenda.

kwa hizi galaxies huduma hii pia ipo ila sio impossible kui bypass kama unavyojua android ina matundu mengi tu hivyo ni rahisi kuchakachua

huyo dogo atakua hakubadili kitu hivyo ikawa rahisi kwa mwenyewe kuitrack.

_UKWO_IFH-B9JUFoFKlfbm2uBnuvLoWPkKmgrrxegjpuUnf8vGdO65YRPZk54n1Mfuw=h310-rw

Mkuu hii kitu ipo namshukuru mungu amenisaidia sana maana jana niipata s4 yangu niliyokuwa nimeibiwa juzi pale Ubungo nilikuwa nashuka tu kwenye dala2 saa 11 alfajiri ili kupanda basi za mikoani jamaa walinizunguka mmoja kajarib kunichomoa wallet kugeuka nyuma sim sina ktk mfuko wa shati nikajua imekwenda nikapanda basi nikaondoka nafika Morogoro km saa 4 hivi nikapata mes ktk sim yangu nyingine niliyobypass no ya sim inayotumika ktk sim yangu ilibidi nishuke pale Morogoro nianze kufuatilia nikajarib kutuma tigopesa nikapata jina la yule bwana nikapanda hewani kumueleza akashangaa kishenzi kadai kuna washikaji wamekuja kwake kuijarib inshort niliinstal app inaitwa eset mobile security hii unasajili line yako tu mtu akitoa yako akaweka ingine sim inajibrock sametime inatuma taarifa ktk no yako uliyobypass pasipo yeye kujua no anayotumia na serial no ya sim yako pia s4 nayo ina program ya sim change alert hivyo ikabidi siku hiyo nirudi dar jana nikakutana naye jamaa kiulafiki kadai mdogo wake aliokota akamuuzia kwa 180000 ilibidi nimtoe 140000 maana alikuwa ni mjeda yuko pale mbagala kambi ya jeshi akanikabidhi sim yangu lkn naona hao vibaka wanawatumia hao wajeda ili wawalinde ktk dili zao

kuna mshikaji wangu alinunua ipad huko zenji. kumbe imeibiwa kwa mtangazaji wa cnn. kudadadeki. dogo aliijiwa dodoma. afu alishaileta kwangu niijailbreak sijui nimuwekee vitu gani...
jamaa walimlocate dodoma ghetto anapokaa ambapo hata mimi ukinielekeza sifiki.
mwenye ipad alikuwa mkali kudadadeki chezea wazungu. alidai alipwe fidia la sivyo kesi iende mahakamani. polisi wakambeba dogo mpaka dar. akakaa lockup wiki wakampa laki saba fidia na kurudisha ipad ikawa settled. dogo akaachiwa. hana hamu na vitu used.

Hivi wakuu ukiiba simu ambayo imewekewa hizo app za kutrace, hafu uka-root/format/factory reset/jail break bado watakunasa tu?
 
mi ninavofahamu kuna application
fulani ambayo ipo ktk hzo simu
application hii inakuwa configured
na namba nyingne ya simu ambayo
ipo ktk simu nyingne, hivyo kama
mtu akiiba simu na akaweka sim
card nyingine basi number ya simu
inatumwa ktk ile simu nyingne
iliyokuwa configured katka
application ile, hivo hata mwizi
abadilishe laini vip number za lain
mpya iliyowekwa katika simu
iliyoibiwa itatumwa kwa mwenye
simu. Hivyo ni rahis kumkamata
mwizi hasa kama hana ufahamu wa
mambo hayo, harafu ukizingatia
sasa hvi kila laini ya simu lazima
isajiriwe hivyo mwizi ni rahisi
kumtambua. Sasa kilichotokea kwa
mdogo wako ni kwamba baada ya
kununua ile simu aliweka lain yake,
application katika simu ikagundua
kuwa kuna new sim card
imewekwa hivyo ika extract
number ya simu ya ile laini na
kuituma kwa mwenye simu na
walivyoipata ile namba wakaitumia
kumpigia na kumlang'ai mdogo
wako kupitia huyo manzi.
 
Kimsingi Police kuna kitengo cha 'Cyber crime', ni kwa bahati mbaya si wengi wanakitumia. Kwa wao wanahitaji 'serial number' ya simu au namba ya sim card yako uliyotumia mara ya mwisho.

Kitendo cha mwizi kuiwasha tu simu wanaweza kujua yuko wapi, na baada ya hapo wanaweza kumtumia mtu mwingine awasiliane naye ili kumkamata.
 
Mbona ziko nyingi sana app za dizaini hii...hata AVast mobile security wanayo na mimi ndo naitumia ambapo hata mtu akiformat simu yako bado unauwezo wa kuitrack kwa kutumia IMEI online, na kuna option nadhani ni kwa pro version hata simu isipokuwa connected online/internet bado inaweza i track kwa sms za kawaida..kuna ingine inaitwa droid lost kama sikosei nlishawahi itumia na zote ziko poa..
 
nilikuwa na sony xperia yangu iiibiwa na sikuipata mpk leo kutokana na siasa za bongo niliweka program inaitwa avg mobile security inachofanya unaweza kuitia alarm non stop kama uko nayo mbali au imeibiwa au unaweza kuialoocte katika tramani lakini muda mwingine huwa inagoma simu inapokuwahaiko connected na internet na pia line ikibadilishwa inakutumia sim card serail nimbwer ya hiyo kadi mpya lakini opia unaweza kuilocl lakini kama chief-mkwawa alovyosema android ni rahisi kuzichakachua nilivyotumiwa simcard serail number kwenye email ikanilzamu niende tigo ili wanitajie namba ya simu iliyokuwemo kwenye hiyo simu wakaniambia hawawezi kufanyahivyo mpk wapate kibali cha upelelezi kutoka kwa mkuu wa polisi mkoa ambae ataandika barua kwa tigo,nikaenda kituo kidogo cha polisi kuchukua rb wakataka hela,nikamalizana nao shughuli ikawa kumpata mkuu wa polisi mkoa wa kimara anindikie barua yaani hawa polisi wadogogwadogo wakawa wanataka laki nzima ili wanikutanishe nae hapo ndipo nilipochoka simu yenyewe lya laki tatu wao wanataka boksi zima na bado kuipata probabilty,basi nilivyoona kusmbuana kumezidi ilibidi niacane nao tu nikailock simu na kuweka ujumbe juu y simu basi sasa hadi leo sijui kama walifanikiwa kuunlock ama vipi????
 
Last edited by a moderator:
Hivi wakuu ukiiba simu ambayo imewekewa hizo app za kutrace, hafu uka-root/format/factory reset/jail break bado watakunasa tu?

apple wanakunasa ila hizi galaxies kama nilivyosema hapo zinachakachulika maana kila kitu unaweza badilisha kuanzia rom, hadi kubadili imei sijui watakushkia wapi
 
jamani mm nillivamiwa like one month ago. wakaiba vitu vyangu vingi ikiwemo s3 na bb. mm nilipuuzia nikaona itz gone. ilavjananimekutana na askari akanishauri kuna kitengovcha polisi kwa kushirikiana na service provider wa mtandao wanaweza kui trace cm hata kama wanei flash! leo naenda kuanza mchakato nitarudi na feedback eapendwa maana jamaa kanitia moyo sana

Kimsingi Police kuna kitengo cha 'Cyber crime', ni kwa bahati mbaya si wengi wanakitumia. Kwa wao wanahitaji 'serial number' ya simu au namba ya sim card yako uliyotumia mara ya mwisho.

Kitendo cha mwizi kuiwasha tu simu wanaweza kujua yuko wapi, na baada ya hapo wanaweza kumtumia mtu mwingine awasiliane naye ili kumkamata.

Sijawahi sikia mtu kafanikiwa through hii kitu. Police yetu bado wako chini sana katika mambo ya Technology. Ila ngoja mkuu hapo atuletee report baadae...
 
Kimsingi Police kuna kitengo cha 'Cyber crime', ni kwa bahati mbaya si wengi wanakitumia. Kwa wao wanahitaji 'serial number' ya simu au namba ya sim card yako uliyotumia mara ya mwisho.

Kitendo cha mwizi kuiwasha tu simu wanaweza kujua yuko wapi, na baada ya hapo wanaweza kumtumia mtu mwingine awasiliane naye ili kumkamata.

Mkuu sio polisi ya tz,mi menyewe yalisha nikuta nikaenda hadi makao makuu ya police kwanza kuipata hiyo barua ya kupeleka kampuni ya simu ni miezi 2,bado huko hadi niliamua niingie front mwenyewe na nikaipata simu yangu.
 
Sijawahi sikia mtu kafanikiwa through hii kitu. Police yetu bado wako chini sana katika mambo ya Technology. Ila ngoja mkuu hapo atuletee report baadae...

Inawezekana wewe hujawahi kuona, mimi nimeshawahi kuona watu watatu wakifanikiwa. Mmoja aliibiwa simu alipovamiwa na majambazi, wa pili aliibiwa simu mbili na vibaka na wa tatu ilikuwa ni ishu ya kutishiwa maisha.
 
Cha msingi ukinunua kitu dai risiti. Itakuokoa maana utapata fedha yako na kuepuka kadhia ya kulala polisi.
Tatizo Watanzania tunapenda mno vya dezo!
 
Mkuu sio polisi ya tz,mi menyewe yalisha nikuta nikaenda hadi makao makuu ya police kwanza kuipata hiyo barua ya kupeleka kampuni ya simu ni miezi 2,bado huko hadi niliamua niingie front mwenyewe na nikaipata simu yangu.

Pengine inawezekana ni kweli ni usumbufu, lakini pia hilo linachangiwa na Police wenyewe kutotoa elimu kwa umma juu ya hilo na ni wapi uingie badala ya kupita kwenye vitengo hata ambavyo havihusiki.

Kingine ni kuwa si vituo vyote vya polisi unaweza kukuta ofisi hii ya 'cyber crime'.
Nakubaliana na wewe inawezekana ulikumbana na huo urasimu lakini so far kwa Watu ninaowafahamu haikuwa tabu.
Hii Nchi nayo wakati mwingine bila "kufahamiana na fulani" hupati huduma inavyostahili.
 
Back
Top Bottom