TEC na KKKT: Mkisema ni nongwa, msiposema ni nongwa

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,009
TEC na KKKT: Mkisema ni nongwa; Msiposema ni nongwa.

Makanisa mawili makongwe hapa nchini yamesema kwa uchungu kuhusu vifo vinavyotokana na Corona. Nawapongeza.

Mijadala inayoendelea kuhusu matamko hayo inaonyesha makanisa haya yana dhamana ya kuchukua hatua katika jamii. Yalipokaa kimya watu walihoji. Sasa yamesema, baadhi ya watu (Mzalendo na Mwana harakati huru Musiba) wanahoji kwa nini yaseme.

Bahati mbaya makanisa yamesema baada ya Viongozi wake wengi kufa. Maaskofu, mapadre, wachungaji, watawa, madaktari, wauguzi na watawala wamekufa wengi. Hata angekuwa mmoja, ni wengi.

Mimi natamani yangesema zaidi ya yalivyosema. Ningetamani waseme hata haya ili kuimarisha vita dhidi ya Corona:

1. KKKT imekemea wanaoshangilia pale Viongozi wa serikali wanapougua Corona. Ni sahihi wakemewe. Ningetamani tukemee pia watanzania wanaowashangilia Wana siasa wanaotumia majukwaa kufanya mizaha juu ya Corona na kuonyesha kuwa Corona si lolote. Wananchi WAACHE kabisa kushangilia kifo. Kumshangilia kwa makofi mwanasiasa anayechezea Corona ni sawa na kushangilia pale mtu anapokufa kwa Corona. Tangu Sasa makofi yawe kipimo cha kukosa uzalendo.

2. Baadhi ya hospitali za umma zinakataa kupokea wagonjwa wenye dalili za Corona. Matokeo yake hospitali chache za mashirika na makanisa ndizo zinapokea wagonjwa hao. Hii inasababisha mrundikano wa wagonjwa sehemu moja. Serikali ikemee tabia ya hospitali zinazokataa wagonjwa lakini pia serikali izipe msaada na vifaa zile hospitali zinazopokea wagonjwa. Kubaguana si tabia ya Corona.

3. Pamoja na hotuba za kutahadhalisha, nashauri mabango ya kuelimisha mitaani yawekwe; Viongozi wa mitaa wakague kila nyumba kuona uwepo wa vifaa vya usafi. Mbona kodi tunaenda majumbani kufuatilia?

4. Wataalam wa magonjwa mlipuko wanakiri hatua mojawapo ya kudhibiti maambukizi ni kujitenga au kuzuia muingiliano kwa muda ili upepo mbaya upite. Tukichukua tahadhari zote tukaacha hili, hii vita tutaishinda? Wataalam waongee. Sisi wengine tukae na kusikiliza kama tunavyosikilizwa pale tunapoongelea utaalam wa uwanja wetu.

Tusizuiane kulia.

HATA MMOJA NI WENGI.

1614824155522.jpeg
 
Hapo sirikali misifa ilitaka KUSIFIWA tu kwa namna ilivyopambana na "kolona" tofauti na namna nchi nyingne zilizotumia njia ya "rockdown"!

Na huyo MSIBA ni sabufa tu ila waya umetokea CHATOO!
 
Bora walau kundi hilo limeanza kusema, Yako wapi makundi mengine? Vyama vya wafanyakazi?...
 
Watu wamekuwa na dhihaka, wanaambiwa hawaelewi, nenda huko makanisani ukaone zipo barakoa ngapi.
 
Umegonga nondo hata sioni chakuongeza, nimependa zaidi hapo uliposema mabango yawekwe mitaani hii itaongeza awareness na seriousness kwa watu badala ya hivi sasa unasikia huyu anasema Corona ipo, baadae anaibuka mwingine anasema haipo, tumekuwa taifa la ajabu sana lililokosa kiongozi, tunatawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
 
Umegonga nondo hata sioni chakuongeza, nimependa zaidi hapo uliposema mabango yawekwe mitaani hii itaongeza awareness na seriousness kwa watu badala ya hivi sasa unasikia huyu anasema Corona ipo, baadae anaibuka mwingine anasema haipo, tumekuwa taifa la ajabu sana lililokosa kiongozi, tunatawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
Umesema kweli kbs! Halafu watz wengi ni vilaza! Mtu anakuambia fulani amesema korona haipo! Huwezi kutumia akili yako kujiongoza!!!
 
Kama tulionba Mungu atuepushie mbali janga la COVID, tuelewe pia Mungu anawatumia wanasayansi katika kujibu maombi yetu.
Pia Mungu huwatumia viongozi wa dini kujibu maombi yetu. Sasa Kama viongozi wa dini wako mlango wa kushoto na anachotaka mzee baba maanaake, maombi take ni batili na hayakubariki.
 
Kama tulionba Mungu atuepushie mbali janga la COVID, tuelewe pia Mungu anawatumia wanasayansi katika kujibu maombi yetu.
Tatizo kubwa ni kuwa baada ya kuomba Mungu na janga la corona kupungua tulianza kumpa utukufu mwanadamu mwenzetu badala ya Mungu
 
Mie naona tumtaje mtu anayedumaza vita ya Covid-19, na tuwe wazi bila woga kusema fulani unatupotosha hovyo unasababisha vifo, maneno ya kuzungusha zungusha, watu kushangilia uongo vita hii itatushinda, wenye nafasi kama viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa tunasubiri tamko lenu, ila tabia yenu ya kujifanya hamuoni sasa ona mnavyoangamia!
 
Umegonga nondo hata sioni chakuongeza, nimependa zaidi hapo uliposema mabango yawekwe mitaani hii itaongeza awareness na seriousness kwa watu badala ya hivi sasa unasikia huyu anasema Corona ipo, baadae anaibuka mwingine anasema haipo, tumekuwa taifa la ajabu sana lililokosa kiongozi, tunatawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
Mistake kubwa sana ilifanyika kumkabidhi kijiti jiwe.😤😭
Umegonga nondo hata sioni chakuongeza, nimependa zaidi hapo uliposema mabango yawekwe mitaani hii itaongeza awareness na seriousness kwa watu badala ya hivi sasa unasikia huyu anasema Corona ipo, baadae anaibuka mwingine anasema haipo, tumekuwa taifa la ajabu sana lililokosa kiongozi, tunatawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
Mistake kubwa sana ilifanyika kumkabidhi kijiti jiwe.😤😭
 
wangekuwa wametoa tamko hili ma Askofu wetu hawa wa mtaani - muda huu wangekuwa wanapimwa mkojo, na kucheki kama ni watanzania halisi ama wazamiaji toka Congo na Rwanda/Burundi.
 
Siasa za matukio kila jambo kila mtu anatia siasa yake humo.
 
Mie naona tumtaje mtu anayedumaza vita ya Covid-19, na tuwe wazi bila woga kusema fulani unatupotosha hovyo unasababisha vifo, maneno ya kuzungusha zungusha, watu kushangilia uongo vita hii itatushinda, wenye nafasi kama viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa tunasubiri tamko lenu, ila tabia yenu ya kujifanya hamuoni sasa ona mnavyoangamia!
Haya; anza wewe nasi tutamalizia.
 
Back
Top Bottom