Team Visasi: Waliomunga Mkono Lowassa Niwasaliti Je Waliomunga Mkono Migiro, Membe na January

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Sijaelewa hoja ya hao wanaoitwa "wasaliti" ndani ya CCM. Hivi kumuunga mkono mtu kwenye kura za maoni ni usaliti? Unapotangaza nia ya kugombea definatelly kuna watu watakuunga mkono na kukupigania. Baada ya kura za maoni kama jina lako halitapitishwa mtamuunga mkono aliyepitishwa. Sasa hapo usaliti unakujaje?

Mimi nilipotangaza nia ya ubunge Moshi (V) kuna watu waliniunga mkono, lakini baada ya mchakato wote kukamilika akapitishwa Mhe.Komu, na tukamuunga mkono. Nilifunga safari kutoka Songea kwenda Moshi kumuombea kura. Na waliokua wakiniunga mkono wakamssuport Komu. Sasa je Komu angewaita wasaliti kwa sababu hawakumuunga mkono kwenye kura za maoni?

Ninachokifahamu ni kwamba hao waliofukuzwa CCM walimuunga mkono Lowassa akiwa CCM wakati wa kura za maoni. Walipigana kuhakikisha jina la Lowassa linapitishwa kama jina la mgombea Urais kupitia CCM. Lakini baada ya Magufuli kupitishwa walimuunga mkono. Mfano mzuri ni Msukuma. Huyu alifunga safari kwa Helcopter hadi Arusha kumuunga mkono Lowassa wakati wa kutangaza nia. Lakini alipopitishwa JPM, akahamia upande wa JPM na kumnadi. Sasa mtu kama huyu anaitwaje msaliti?

Neno usaliti maana yake ni nini? Kwahiyo ndani ya CCM ni dhambi kuwaunga mkono wagombea wengine wakati wa kura za maoni? Yani unataka kwenye kura za maoni watu wote wamuunge mkono mtu mmoja tu. Hapo ndo itaonekana hamna usaliti?

Sasa naanza kuelewa kwanini 2020 wanataka apitishwe peke yake. Wakiriluhusu wagombea wengine, wafuasi wao wataitwa wasaliti tena.

Anyway, waliomuunga mkono Lowassa wameitwa wasaliti na kufukuzwa, vipi waliomuunga mkono Membe, Migiro, January etc. Hawa usaliti wao utajadiliwa lini na watafukuzwa lini? [HASHTAG]#TeamVisasi[/HASHTAG]
 
Tatizo linakuja pale ambapo mtu unayemuunga mkono anashindwa na kuhama chama wewe ndo unakuwa unamuibia siri za chama pamoja na kukihujumu chama.Pia kwa hoja yako hiyo na wao walikuwa wanatakiwa wakubali kushindwa maana siyo kila unayemuunga mkono lazima ashinde...
hawakurupuki tu kufukuza mtu.
 
Sijui kama hiyo ni sababu ya hitimisho, walikuwa wengi sana waliomuunga mkono Lowasa akiwa kwenye harakati zake ila baada ya kumpata Mgombea wao walinyamaza na kumuunga mkono mgombea wa chama na sio makundi tena, Nchimbi, Kimbisa na wakereketwa wengine wa Lowasa walijirudi na kumpigia kampeni Magufuli.
Taarifa za kufukuzwa kwao ni kitendo cha kuendelea kumkumbatia Mh. Lowasa akiwa Chadema wao wakiwa CCM. Zipo taarifa zilikuwa zikitoka kuwa kuna watu wameachwa ccm makusudi ili kukamilisha kazi, basi jua ni kina Sofia, Madabida na wengineo.
Kama issue ilikuwa ni kuwatimua waliomuunga mkono Mh. Lowasa akiwa CCM basi kina Bashe nao wangepigwa chini kitambo.
Wapo CCM walioamua kusepa bila kuwa wanafiki kwa mapenzi yao kwa Lowasa, Mgeja, Mahanga, Masha.....wengine walibaki kumakizia kazi ila kabla ya kumakiza wakamalizwa wao.
 
Sijaelewa hoja ya hao wanaoitwa "wasaliti" ndani ya CCM. Hivi kumuunga mkono mtu kwenye kura za maoni ni usaliti? Unapotangaza nia ya kugombea definatelly kuna watu watakuunga mkono na kukupigania. Baada ya kura za maoni kama jina lako halitapitishwa mtamuunga mkono aliyepitishwa. Sasa hapo usaliti unakujaje?

Mimi nilipotangaza nia ya ubunge Moshi (V) kuna watu waliniunga mkono, lakini baada ya mchakato wote kukamilika akapitishwa Mhe.Komu, na tukamuunga mkono. Nilifunga safari kutoka Songea kwenda Moshi kumuombea kura. Na waliokua wakiniunga mkono wakamssuport Komu. Sasa je Komu angewaita wasaliti kwa sababu hawakumuunga mkono kwenye kura za maoni?

Ninachokifahamu ni kwamba hao waliofukuzwa CCM walimuunga mkono Lowassa akiwa CCM wakati wa kura za maoni. Walipigana kuhakikisha jina la Lowassa linapitishwa kama jina la mgombea Urais kupitia CCM. Lakini baada ya Magufuli kupitishwa walimuunga mkono. Mfano mzuri ni Msukuma. Huyu alifunga safari kwa Helcopter hadi Arusha kumuunga mkono Lowassa wakati wa kutangaza nia. Lakini alipopitishwa JPM, akahamia upande wa JPM na kumnadi. Sasa mtu kama huyu anaitwaje msaliti?

Neno usaliti maana yake ni nini? Kwahiyo ndani ya CCM ni dhambi kuwaunga mkono wagombea wengine wakati wa kura za maoni? Yani unataka kwenye kura za maoni watu wote wamuunge mkono mtu mmoja tu. Hapo ndo itaonekana hamna usaliti?

Sasa naanza kuelewa kwanini 2020 wanataka apitishwe peke yake. Wakiriluhusu wagombea wengine, wafuasi wao wataitwa wasaliti tena.

Anyway, waliomuunga mkono Lowassa wameitwa wasaliti na kufukuzwa, vipi waliomuunga mkono Membe, Migiro, January etc. Hawa usaliti wao utajadiliwa lini na watafukuzwa lini? [HASHTAG]#TeamVisasi[/HASHTAG]

waliounga mkono membe, migiro, january, na wengineo isipokuwa lowasa, baada ya kupitishwa magufuli walikubali wakamuunga mkono na kuendelea na mwenendo mwema katika chama.

waliomuunga mkono lowasa hawakukubali kumuunga mkono magufuli, walibaki ccm kimkakati huku wakimuunga mkono lowasa na kuiba siri za chama ili kufanikisha ushindi wa lowasa huko alikokuwa chadema! hapo ndo dhana ya usaliti inapokuja! na msaliti unajua adhab yake, kama ingekuwa jeshini anauawa kabisa, ila kwenye chama anafukuzwa tu.

hata hivo sio wote waliomuunga mkono lowasa akiwa ccm wamefukuzwa! umeona kimbisa amebaki, inchimbi onyo kali, bashe bado yupo, msukuma yupo, na wengine wengi sana! walioendelea na usaliti ndo wametimuliwa.

sasa mleta mada acha kutumia hisia na kutafta huruma ya wasaliti! hii adhabu hata huko kwenu chadema ndo mlimpa zitto..
 
Tatizo linakuja pale ambapo mtu unayemuunga mkono anashindwa na kuhama chama wewe ndo unakuwa unamuibia siri za chama pamoja na kukihujumu chama.
hawakurupuki tu kufukuza mtu.

Siri zipi hizo? Wakati Chama kinalindwa na nguvu kubwa ya Dola?
 
Sijui kama hiyo ni sababu ya hitimisho, walikuwa wengi sana waliomuunga mkono Lowasa akiwa kwenye harakati zake ila baada ya kumpata Mgombea wao walinyamaza na kumuunga mkono mgombea wa chama na sio makundi tena, Nchimbi, Kimbisa na wakereketwa wengine wa Lowasa walijirudi na kumpigia kampeni Magufuli.
Taarifa za kufukuzwa kwao ni kitendo cha kuendelea kumkumbatia Mh. Lowasa akiwa Chadema wao wakiwa CCM. Zipo taarifa zilikuwa zikitoka kuwa kuna watu wameachwa ccm makusudi ili kukamilisha kazi, basi jua ni kina Sofia, Madabida na wengineo.
Kama issue ilikuwa ni kuwatimua waliomuunga mkono Mh. Lowasa akiwa CCM basi kina Bashe nao wangepigwa chini kitambo.
Wapo CCM walioamua kusepa bila kuwa wanafiki kwa mapenzi yao kwa Lowasa, Mgeja, Mahanga, Masha.....wengine walibaki kumakizia kazi ila kabla ya kumakiza wakamalizwa wao.
Je wameisha wote? Kuna alama gani mtu anayo kuwa siyo mtiifu kwa Lowasa kwa mfano!
 
Je wameisha wote? Kuna alama gani mtu anayo kuwa siyo mtiifu kwa Lowasa kwa mfano!
Unafikiri wameamka tu asubuhi wakasema fukuza huyu bila ushahidi, kuisha sio hoja yao ila yoyote atakayejaribu kwa vitendo ndio atawajibika.
Hawa wote wameshiriki kwa vitendo, kama nafsi yako inapenda nani wa kuja kuifungua ili aone? Unafikiri kila aliyekuwa ccm anaipenda ccm au chadema anaipenda chadema kwa dhati? Onyesha mapenzi yako kwa vitendo kama utapona.
 
Sijaelewa hoja ya hao wanaoitwa "wasaliti" ndani ya CCM. Hivi kumuunga mkono mtu kwenye kura za maoni ni usaliti? Unapotangaza nia ya kugombea definatelly kuna watu watakuunga mkono na kukupigania. Baada ya kura za maoni kama jina lako halitapitishwa mtamuunga mkono aliyepitishwa. Sasa hapo usaliti unakujaje?

Mimi nilipotangaza nia ya ubunge Moshi (V) kuna watu waliniunga mkono, lakini baada ya mchakato wote kukamilika akapitishwa Mhe.Komu, na tukamuunga mkono. Nilifunga safari kutoka Songea kwenda Moshi kumuombea kura. Na waliokua wakiniunga mkono wakamssuport Komu. Sasa je Komu angewaita wasaliti kwa sababu hawakumuunga mkono kwenye kura za maoni?

Ninachokifahamu ni kwamba hao waliofukuzwa CCM walimuunga mkono Lowassa akiwa CCM wakati wa kura za maoni. Walipigana kuhakikisha jina la Lowassa linapitishwa kama jina la mgombea Urais kupitia CCM. Lakini baada ya Magufuli kupitishwa walimuunga mkono. Mfano mzuri ni Msukuma. Huyu alifunga safari kwa Helcopter hadi Arusha kumuunga mkono Lowassa wakati wa kutangaza nia. Lakini alipopitishwa JPM, akahamia upande wa JPM na kumnadi. Sasa mtu kama huyu anaitwaje msaliti?

Neno usaliti maana yake ni nini? Kwahiyo ndani ya CCM ni dhambi kuwaunga mkono wagombea wengine wakati wa kura za maoni? Yani unataka kwenye kura za maoni watu wote wamuunge mkono mtu mmoja tu. Hapo ndo itaonekana hamna usaliti?

Sasa naanza kuelewa kwanini 2020 wanataka apitishwe peke yake. Wakiriluhusu wagombea wengine, wafuasi wao wataitwa wasaliti tena.

Anyway, waliomuunga mkono Lowassa wameitwa wasaliti na kufukuzwa, vipi waliomuunga mkono Membe, Migiro, January etc. Hawa usaliti wao utajadiliwa lini na watafukuzwa lini? [HASHTAG]#TeamVisasi[/HASHTAG]

Bosi achaga usaniii. Hivi uliwezaje kufika kugombea ubunge kwa such kind of reasoning and deduction. Where is your major which justifies your sylogism and conclusion. Du yani unafumbwa hivi na majibu yako afu unayatungia mada. Hivi hujajiuliza kwanini mambo mengi ya siri yanatoka. Mbona mna dharau sana vyeo hivi na uwezo wa kujua wabaya. Unasema kisasi du. Kweli asiyejua mpe bundle. Let me put it for you like this:Your agenda is to attack either mkuu au chama. So what you do is to search anything to fit the heading and the mada mliyo nayo. Ndo mana hutaona sifa hata moja why ? Mtu makini uliyetaka kugombea ubunge ingekuwa unachambua. Unaangalia nyuma tulipotoka. Tulipo na nini tunahitaji kama watanzania sio wamarekani au wacuba. We are we as Tanzanians. Tatizo letu la kwanza pamoja na mambo mengine wavivu sana. Wapiga domo sana. Sekta binafsi ndo wanabanana. Mitandao imeturoga. Hakuna hoja ila matusi. Unaona kabisa watu wanaanzisha hoja kwa moto. Akija kuishikia mtu bango. Mnaangalia nani. Mbaya wenu mnageuka. Hantaki kuona zaidi ya pua zenu. Its too sad.
 
Back
Top Bottom