Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,488
- 13,608
Mleta mada ni wale wale wanaopufushwa na mahaba kwa mtu badala ya kuangalia substance. Kilichofanyika Dodoma kama kikifanyika ndani ya CDM maana yake kitakuwa ni chama mbadala wa kweli wa CCM. Lakini hakiwezi kufanyika, sana sana gia zitabadilikia angani.waliounga mkono membe, migiro, january, na wengineo isipokuwa lowasa, baada ya kupitishwa magufuli walikubali wakamuunga mkono na kuendelea na mwenendo mwema katika chama.
waliomuunga mkono lowasa hawakukubali kumuunga mkono magufuli, walibaki ccm kimkakati huku wakimuunga mkono lowasa na kuiba siri za chama ili kufanikisha ushindi wa lowasa huko alikokuwa chadema! hapo ndo dhana ya usaliti inapokuja! na msaliti unajua adhab yake, kama ingekuwa jeshini anauawa kabisa, ila kwenye chama anafukuzwa tu.
hata hivo sio wote waliomuunga mkono lowasa akiwa ccm wamefukuzwa! umeona kimbisa amebaki, inchimbi onyo kali, bashe bado yupo, msukuma yupo, na wengine wengi sana! walioendelea na usaliti ndo wametimuliwa.
sasa mleta mada acha kutumia hisia na kutafta huruma ya wasaliti! hii adhabu hata huko kwenu chadema ndo mlimpa zitto..