TCU yawanyanyasa wananchi mkoa wa Kagera.......mkoa mzima NBC bank iko moja tu

JamiiForums

Official JF Response
Nov 9, 2006
6,200
4,984
Posted by Ta Muganyizi | May 14, 2012

Katika hali inayochanganya TCU walitoa tangazo kuwa kwa wale wahitimu wanaotaka kujiunga na vyo vikuu lazima wanunue vocha kwenye Benki ya NBC watu walinunua kadi hizo wakarudi makwao ili wakwangue waombe nafasi vyuoni. Cha ajabu vocha zote ukizikwangua na kuzitumia unaambiwa vocha number does'nt exist!!! imebidi watoke wilayani kwao kurudi Bukoba mjini..........maaana katika mkoa wa Kagera benki ya NBC iko Bukoba mjini tu, kwingineko benki hiyo haipo. TCU hawajatoa walau tangazo kwa nini vocha hizo hazifanyi kazi na tatizo ni nini!!!!!

Hii imesumbua sana wananchi mwenye maelezo ya kutosha anaweza fafanua hapa inakuwaje. Baadhi wameanza kuhisi kuwa kuna business ya watu wa TCU na NBC maana ni kwa nini isiwe NMB ambayo iko karibia kila wilaya?
 
Last edited by a moderator:
Jana usiku Prof wa tcu na team yake walikuwa itv lakini sikusikia wanalitolea ufafanuzi suala hilo la kuhama CRDB na kwenda NBC na sio NMB ambayo imezagaa nchi nzima - pengine pale hapakuwa mahala pake - wachangiaji walichanganya mambo na kukazania suala la mikopo badala ya kuzamia katika ufanisi wa TCU katika zoezi hili tokea waanze takriban miaka 2 iliyopita. voUcher sasa zina kubalika tokea jana au juzi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom