TCU yafuta baadhi ya Vyuo, yaruhusu vingine kufanya udahili na vingine vyasitishiwa udahili

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,445
3,403
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesitisha udahili na kufuta baadhi ya Vyuo vilivyofungiwa mwaka 2017 na kutakiwa kufanya maboresho mbalimbali lakini hawakufanikiwa kurekebisha dosari hizo

Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa kimeendelea kuziwa kufanya udahili kutokana na kutokidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa

Vyuo vilivyoruhusiwa kufanya udahili kwa baadhi ya masomo ni Chuo cha Umoja wa Waafrika Tanzania, Teofilo Kisanji (Mbeya), Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Mihayo na Chuo Kikuu cha Kampala-Tanzania

Vingine ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian, Chuo Kikuu Kishiriki cha Uhandisi na Teknolojia cha Mt. Joseph, Chuo Kikuu Kishiriki cha Kikristo cha Tiba Kilimanjaro (KCMUCo) na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stefano Moshi (SMMUCo)

Vyuo vilivyofutwa ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Jacob, Chuo Kikuu Kishiriki cha Kadinali Rugambwa (KARUMUKO), Chuo Kikuu cha Teofile Kisanji (Dar), Chuo Kikuu cha Mt. Yohana Kituo cha Mt. Marko na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Arusha

Vingine ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah Kibira (JOKUCo), Chuo Kikuu cha Mlima Meru (MMU), Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU) na Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB)

Aidha, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amesema Chuo Kikuu Kishiriki na Sayansi Shiriki cha Mt. Francis cha Ifakara (SFUCHAS) kimeruhusiwa kufanya udahili kuanzia mwaka 2020/21
 
Kuongoza kwa vyuo Kikristo kufungiwa ni dalili ya ubabaishaji na upigaji mwingi uliojaa kwenye Taasisi za kidini. Jina la Mungu linadhalilisha kupitia biashara. Wanaacha kuokoa roho wanakimbilia kufanya biashara kwa mgongo wa dini. Hii ni dhambi mbaya sn

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kama shule za kiislamu zinavowaibiwa watu pesa zao huku zikishika mkia kila mwaka matokeo ya kidato cha nne na form six yaani wanazalisha mazuzu tuu na kuyapandikiza majini na mapepo.
 
Kuongoza kwa vyuo Kikristo kufungiwa ni dalili ya ubabaishaji na upigaji mwingi uliojaa kwenye Taasisi za kidini.

Jina la Mungu linadhalilisha kupitia biashara. Wanaacha kuokoa roho wanakimbilia kufanya biashara kwa mgongo wa dini. Hii ni dhambi mbaya sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi waislam wana vyuo vikuu vingapi hapa Tz?

dodge
 
Hoja ya Kitaaluma imegeuzwa kidini, tusifike huko tafadhali, chuo kibovu ni janga kwa Taifa zima na waathiriwa sio dini Fulani tu.
 
Kuongoza kwa vyuo Kikristo kufungiwa ni dalili ya ubabaishaji na upigaji mwingi uliojaa kwenye Taasisi za kidini.

Jina la Mungu linadhalilisha kupitia biashara. Wanaacha kuokoa roho wanakimbilia kufanya biashara kwa mgongo wa dini. Hii ni dhambi mbaya sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani kama ni upigaji

Ninachowaza kwa upande wangu labda hawakuwa na mitaji ya kutosha ili kukidhi hivo vigezo hasa miundo mbinu ya kutosha, Wahadhiri wenye sifa stahiki na mengine kama hayo
 
Wewe mtu wewe,huwezi tafsiri jina!Kama wao wanajiita st John university wewe huwezi tuambia mt. Yohana.Haipendezi.
Ni sawa na kutafsiri majina kv mh.Pombe wewe useme hon.Alcohol au hon.Beer!
Au bwana Masamaki use Mr The fishes!
Au hon.Godbless useme mh.Mungubariki!

Hii ni kujaribu kupotosha
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), imesitisha udahili na kufuta baadhi ya Vyuo vilivyofungiwa mwaka 2017 na kutakiwa kufanya maboresho mbalimbali lakini hawakufanikiwa kurekebisha dosari hizo

Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastian Kolowa kimeendelea kuziwa kufanya udahili kutokana na kutokidhi viwango vya Kitaifa na Kimataifa

Vyuo vilivyoruhusiwa kufanya udahili kwa baadhi ya masomo ni Chuo cha Umoja wa Waafrika Tanzania, Teofilo Kisanji (Mbeya), Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Mihayo na Chuo Kikuu cha Kampala-Tanzania

Vingine ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian, Chuo Kikuu Kishiriki cha Uhandisi na Teknolojia cha Mt. Joseph, Chuo Kikuu Kishiriki cha Kikristo cha Tiba Kilimanjaro (KCMUCo) na Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Stefano Moshi (SMMUCo)

Vyuo vilivyofutwa ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Askofu Mkuu Jacob, Chuo Kikuu Kishiriki cha Kadinali Rugambwa (KARUMUKO), Chuo Kikuu cha Teofile Kisanji (Dar), Chuo Kikuu cha Mt. Yohana Kituo cha Mt. Marko na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Arusha

Vingine ni Chuo Kikuu Kishiriki cha Josiah Kibira (JOKUCo), Chuo Kikuu cha Mlima Meru (MMU), Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU) na Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UoB)

Aidha, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amesema Chuo Kikuu Kishiriki na Sayansi Shiriki cha Mt. Francis cha Ifakara (SFUCHAS) kimeruhusiwa kufanya udahili kuanzia mwaka 2020/21

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hatuwasikii wakifuta shule za msingi na za sekondari ambapo wanafunzi wanakaa chini bila madawati?

Ndalichako fungia na shule za msingi maana huko ndipo kwenye dimbwi la kusomea ujinga!

Kwa kuthibitisha hili, matunda ya shule za kata tumeyaona kwenye Kiingereza cha Waziri wa elimu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huko ifakara hao sijui ni masista au mapadri wanashusha majengo na vitega uchumi balaa. Na sasa wanaongeza chuo. Na sasa wamejenga hospitali ya kansa huko ifakara. Hao sio watu wa mchezo.
Sijui pesa wanatoa wapi.
 
Ingependeza kama ingefafanuliwa kuwa hivyo vyuo vikuu vishiriki vilivyotajwa ni campus ipi na ipi maana kuna main campus na matawi yake. Mfano Chuo Kikuu cha Marian kuna main campus kule Bagamoyo na tawi lake lipo Dar.
 
Back
Top Bottom