TCU rudisheni mfumo wa kudahili wanafunzi vyuoni kwa njia ya mtandao (CAS)

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,301
12,600
TCU ni taasisi inayodhibiti ubora wa elimu ya juu. Inakagua, inashauri, inaruhusu Na kusimamisha au kufuta vyuo visivyokidhi vigezo vya ubora. Hivyo, vyuo vyote ambavyo vinatoa mafunzo vimefikia vigezo (minimum) vya ubora wa kumudu kutoa mafuzo yaliyokusudiwa. Ingawa ni kweli vyuo vinatofautiana kwa ubora.

TCU ndiyo yenye takwimu za vyuo vikuu vyote kuhusu kozi, ubora na idadi ya wanafunzi wanaoweza kudahiriwa kwenye kila chuo pamoja na ada inayotozwa kwa kila chuo.

Kabla ya kufutwa na Rais JPM wanafuzi walikuwa wanatuma maombi ya kujiunga vyuo vikuu kwa kutumia CAS kuchagua kozi na vyuo na mfumo huo wa udahiri ulikuwa na uwezo wa kumpangia mwanafuzi kozi aliyoomba kwenye chuo alichoomba kulingana na ufaulu wake na idadi ya walioomba kozi hiyo kwenye chuo hicho. Na kama nafasi kwenye chuo hicho imejaa mfumo ulikuwa ukimpeleka kwenye chuo kingine chenye nafasi bila usumbufu na gharama ya ziada kwa mwanafunzi.

Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki.

Kufanya hivi kuna hasara zifuatazo:
1. Mwanafunzi anatumia hela nyingi kwenye maombi ya nafasi vyuoni.
2. Wanafuzi wanarundikana kwenye chuo kimoja wakati kuna nafasi kwenye vyuo vingine.
3. Unatoa nafasi ya wazazi kutoa rushwa kubwa vyuoni ili watoto wao wachaguliwe kozi fulani kwenye chuo fulani.
4. Baadhi ya vyuo vimepata nafasi ya kuwabagua wanafunzi wanaotoka kaya maskini wenye hela za kudunduliza kulipia karo kubwa za vyuo vyao.
5. Utaratibu unatoa mwanya kwa watendaji wa vyuo kuchagua ndugu zao, kabila na rafiki zao kupata nafasi ya kusoma chuoni kwao na kuwaacha watoto wengine wenye ufaulu mkubwa kuliko walioingizwa chuoni.
6. Mfumo unatoa mwanya wa UDINI kwenye selection. Anaechagua nani achaguliwe anaweza kusukumwa na vionjo vya udini na dhehebu lake kupatia nafasi kwanza watoto wa dini na dhehebu lake hata kama walioachwa wana ufaulu mkubwa kuliko waliopendelewa.

7. Vyuo vinadahiri kupita uwezo wao waliokadiriwa.

Faida zilizokusudiwa za utaratibu huu wa sasa ni moja tu, kuwa mwanafunzi atachagua chuo anachokitaka yeye. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa hata kwenye utaratibu huu sio kweli kuwa wanafunzi wote wanachaguliwa kwenye vyuo walivyovitaka, bado wanaendelea kudahiriwa kwenye vyuo vyenye nafasi kama zamani baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo wanavyovipenda.

Wanafunzi na wazazi wanadanganywa na majina ya vyuo kumbe elimu ni ileile hata kwa vyuo vingine.

Kudhibitisha ukweli huu TCU ipitie ufaulu wa wanafunzi wote walioomba kwenye vyuo ilinganishe na ufaulu wa wanafunzi wote waliodahiriwa kwenye vyuo wataogundua dhambi hii ya ubaguzi.
 
Bado nadhani jiwe alizingua kwa kustopisha hii CAS..ilikuwa ni system moja nzuri sana.

Halafu hii ya kusema mwanafunzi anachagua kozi na chuo anachokitaka ni upumbavu mtupu..hata CAS ilikuwa inakupa nafasi tano ya kuchagua vyuo na kozi na unazipanga kwa priority...na inapunguza kujuana sana na kupendeleana..Hii system mpya hata kama TCU ina oversee lakini bado nadhani ina mianya mingi ya rushwa.

Kibongobongo bado CAS ilikuwa nzuri,jiwe alikurupuka kama kawaida yake ya kutaka cheap popularity.
 
Bado nadhani jiwe alizingua kwa kustopisha hii CAS..ilikuwa ni system moja nzuri sana.

Halafu hii ya kusema mwanafunzi anachagua kozi na chuo anachokitaka ni upumbavu mtupu..hata CAS ilikuwa inakupa nafasi tano ya kuchagua vyuo na kozi na unazipanga kwa priority...na inapunguza kujuana sana na kupendeleana..Hii system mpya hata kama TCU ina oversee lakini bado nadhani ina mianya mingi ya rushwa.

Kibongobongo bado CAS ilikuwa nzuri,jiwe alikurupuka kama kawaida yake ya kutaka cheap popularity.
Alilishwa matangopori Mzee wa watu, walimtumia bila yeye kufahamu.
 
Alilishwa matangopori Mzee wa watu, walimtumia bila yeye kufahamu.
CAS ilikuwa inajenga taifa lisilokuwa na ubaguzi wa dini, kabila, kanda wala kujuana kwenye elimu. Ufaulu ndio uliokuwa unawaunganisha watoto. Hatukatai kuwa hata kwenye CAS kulikuwa na wakora waliokuwa wanamanipulate mfumo, lakini ni rahisi kudili na mkora mmoja kuliko kudili na nyoyo za kibaguzi za vyuoni na taasisi.
 
TCU ni taasisi inayodhibiti ubora wa elimu ya juu. Inakagua, inashauri, inaruhusu Na kusimamisha au kufuta vyuo visivyokidhi vigezo vya ubora. Hivyo, vyuo vyote ambavyo vinatoa mafunzo vimefikia vigezo (minimum) vya ubora wa kumudu kutoa mafuzo yaliyokusudiwa. Ingawa ni kweli vyuo vinatofautiana kwa ubora.

TCU ndiyo yenye takwimu za vyuo vikuu vyote kuhusu kozi, ubora na idadi ya wanafunzi wanaoweza kudahiriwa kwenye kila chuo pamoja na ada inayotozwa kwa kila chuo.

Kabla ya kufutwa na Rais JPM wanafuzi walikuwa wanatuma maombi ya kujiunga vyuo vikuu kwa kutumia CAS kuchagua kozi na vyuo na mfumo huo wa udahiri ulikuwa na uwezo wa kumpangia mwanafuzi kozi aliyoomba kwenye chuo alichoomba kulingana na ufaulu wake na idadi ya walioomba kozi hiyo kwenye chuo hicho. Na kama nafasi kwenye chuo hicho imejaa mfumo ulikuwa ukimpeleka kwenye chuo kingine chenye nafasi bila usumbufu na gharama ya ziada kwa mwanafunzi.

Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki.

Kufanya hivi kuna hasara zifuatazo:
1. Mwanafunzi anatumia hela nyingi kwenye maombi ya nafasi vyuoni.
2. Wanafuzi wanarundikana kwenye chuo kimoja wakati kuna nafasi kwenye vyuo vingine.
3. Unatoa nafasi ya wazazi kutoa rushwa kubwa vyuoni ili watoto wao wachaguliwe kozi fulani kwenye chuo fulani.
4. Baadhi ya vyuo vimepata nafasi ya kuwabagua wanafunzi wanaotoka kaya maskini wenye hela za kudunduliza kulipia karo kubwa za vyuo vyao.
5. Utaratibu unatoa mwanya kwa watendaji wa vyuo kuchagua ndugu zao, kabila na rafiki zao kupata nafasi ya kusoma chuoni kwao na kuwaacha watoto wengine wenye ufaulu mkubwa kuliko walioingizwa chuoni.
6. Mfumo unatoa mwanya wa UDINI kwenye selection. Anaechagua nani achaguliwe anaweza kusukumwa na vionjo vya udini na dhehebu lake kupatia nafasi kwanza watoto wa dini na dhehebu lake hata kama walioachwa wana ufaulu mkubwa kuliko waliopendelewa.

7. Vyuo vinadahiri kupita uwezo wao waliokadiriwa.

Faida zilizokusudiwa za utaratibu huu wa sasa ni moja tu, kuwa mwanafunzi atachagua chuo anachokitaka yeye. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa hata kwenye utaratibu huu sio kweli kuwa wanafunzi wote wanachaguliwa kwenye vyuo walivyovitaka, bado wanaendelea kudahiriwa kwenye vyuo vyenye nafasi kama zamani baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo wanavyovipenda.

Wanafunzi na wazazi wanadanganywa na majina ya vyuo kumbe elimu ni ileile hata kwa vyuo vingine.

Kudhibitisha ukweli huu TCU ipitie ufaulu wa wanafunzi wote walioomba kwenye vyuo ilinganishe na ufaulu wa wanafunzi wote waliodahiriwa kwenye vyuo wataogundua dhambi hii ya ubaguzi.
Kweli kabisa mkuu
TCU hapa inabidi waliangalie upya ili swala kwa mapana yake
 
"Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki."

Tusidanganyane, mwanafunzi aombe chuo anachotaka na akasome huko huko.

Suala la kusema eti elimu za vyuo vikuu vinafanana huo ni uongo mkubwa! Elimu zinatofautiana kabisaa.

Je, kuna mzazi yoyote aliyelalamikia gharama kubwa za kuomba vyuo vingi?

Kila mhitimu ana vigezo vyake vya kuomba chuo, mwingine anataka aishi mkoa fulani kutokana na sababu zake, sasa akipangiwa mkoa mwingine na CAS si ni shida!

Ipo wazi, baada ya kufuta mfumo wa CAS, vyuo fulani vya ujanja ujanja vilianza kukosa wanafunzi, kw sababu wanafunzi walikuwa hawavitaki.

Baadhi ya vyuo vilitumia hila kupata idadi kubwa ya wanafunzi, na kuzima ndoto za wahitimu. CAS inampeleka kwenye kozi na chuo ambavyo hana interest nazo!

Toa elimu bora, matangazo kwa sana, utapata tu wanafunzi, usitegemee CAS ikubebe baada ya kuhonga TCU!
 
Wale wa zamani watakuwa wanakumbuka, yaani unaomba chuo zaidi ya kimoja, na majibu yanakuja "Multiple Selection", una confirm chuo kimoja maisha yanaendelea, na HESLB wanakufuata huko huko ulipo-confirm.

Kule kwenye chuo kingine, nafasi inajazwa kwa second selection.

Tuache ujanja ujanja wa kutaka kuwahonga TCU ili chuo kipate wanafunzi wengi.

Napinga kwa nguvu zote mwanafunzi kupangiwa chuo na TCU.

Pamoja na mapungufu ya jiwe, ila kwenye hili ntaendelea kumuunga mkono.
 
Huo mfumo ulifeli kwa kuwachagulia wanafunzi fani wasizozitaka.
Na vyuo wasivyovitaka.

Yaan mtu anaenda kusoma chuo kikuu fani asiyoitaka wala kuiomba, Na hajui inahusiana na nini.

Ulikua ni upuuz wa kiwango cha Lami.
 
Mfumo wa kuomba direct ni mzuri saana kwa 7bu
1... gharama ni uniform (10000) tu na kwingine free kabisa.
2... fursa ya kuomba course nyingi zaidi kuanziw 3 hadi 15 (udsm).
3... uhuru wa kuombaa vyuo upendavyoo.
4... kuondoa nentality ya chuo fulani ndio bora zaidi angali vyote viko under TCU guidelines, requlations
 
"Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki."

Tusidanganyane, mwanafunzi aombe chuo anachotaka na akasome huko huko.

Suala la kusema eti elimu za vyuo vikuu vinafanana huo ni uongo mkubwa! Elimu zinatofautiana kabisaa.

Je, kuna mzazi yoyote aliyelalamikia gharama kubwa za kuomba vyuo vingi?

Kila mhitimu ana vigezo vyake vya kuomba chuo, mwingine anataka aishi mkoa fulani kutokana na sababu zake, sasa akipangiwa mkoa mwingine na CAS si ni shida!

Ipo wazi, baada ya kufuta mfumo wa CAS, vyuo fulani vya ujanja ujanja vilianza kukosa wanafunzi, kw sababu wanafunzi walikuwa hawavitaki.

Baadhi ya vyuo vilitumia hila kupata idadi kubwa ya wanafunzi, na kuzima ndoto za wahitimu. CAS inampeleka kwenye kozi na chuo ambavyo hana interest nazo!

Toa elimu bora, matangazo kwa sana, utapata tu wanafunzi, usitegemee CAS ikubebe baada ya kuhonga TCU!
Unaposema kuna vyuo vya ujanjaujanja haitofautiani na kuitukana TCU na serikali nzima. TCU huwa inafungia vyuo vyote vya ujanjaujanja na orodha ya vyuo vilivyositishiwa udahiri ama kufutwa ipo wazi hata kwenye website za TCU. Hivyo kusema kuna vyuo vya ujanjaujanja ni sawa na kusema TCU is bogus.

Sio kweli kuwa wanafunzi wanachaguliwa kwenye vyuo wanavyovipenda (first choice). Mwanafunzi anaechaguliwa kwenye chuo anachokipenda ni yule tu mwenye ufaulu mkubwa kuliko waombaji wengine alioomba nao kwenye kozi husika. Vinginevyo chuo kitalazimika kiwaache waombaji wengine wenye sifa kuliko zake kwa kutumia kujuana, undugu, rushwa, udini, ukanda, uwezo wa kulipa na sababu nyingene nje ya academic qualifications. Wanafunzi walioachwa kwa sababu hizi hawana choice wataenda chuo chochote halali wakasome kuepuka kubakia nyumbani mwaka mzima wasubiri kuomba kwenye chuo wanachokipenda.

Hivyo kwa ufupi unapotosha umma. Mfumo wa CAS ulikuwa unampeleka mwanafunzi kwenye first choice yake kama ufaulu wake unawazidi waombaji wengine. Taifa letu bado changa bado tunaendelea kujenga utaifa na uzalendo. Hakika JPM alidanganywa kuhusu CAS na wasiokuwa na nia njema kwa taifa.

CAS iliwaleta pamoja watoto wa taifa hili bila kujali matabaka. Sasa hivi chuo na taasisi inachagua nani asome kwake na nani asisome bila kujali sana sifa za kitaaluma za mwanafunzi. Chuo cha kiislam kingependa kuona majina mengi ya akina Abdallah, Omari, Zaina, Samia kuliko Rose, Antony, George, Glory nk. Hapa tunarudi nyuma kama taifa. Kuna vyuo havitaki kuona wanafunzi waliosoma shule za Kata kwa kisingizio kuwa hawataweza kulipa ada yao, huu ni msiba mkubwa kwa taifa kama upuuzi huu utaruhusiwa kusonga mbele.
 
"Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki."

Tusidanganyane, mwanafunzi aombe chuo anachotaka na akasome huko huko.

Suala la kusema eti elimu za vyuo vikuu vinafanana huo ni uongo mkubwa! Elimu zinatofautiana kabisaa.

Je, kuna mzazi yoyote aliyelalamikia gharama kubwa za kuomba vyuo vingi?

Kila mhitimu ana vigezo vyake vya kuomba chuo, mwingine anataka aishi mkoa fulani kutokana na sababu zake, sasa akipangiwa mkoa mwingine na CAS si ni shida!

Ipo wazi, baada ya kufuta mfumo wa CAS, vyuo fulani vya ujanja ujanja vilianza kukosa wanafunzi, kw sababu wanafunzi walikuwa hawavitaki.

Baadhi ya vyuo vilitumia hila kupata idadi kubwa ya wanafunzi, na kuzima ndoto za wahitimu. CAS inampeleka kwenye kozi na chuo ambavyo hana interest nazo!

Toa elimu bora, matangazo kwa sana, utapata tu wanafunzi, usitegemee CAS ikubebe baada ya kuhonga TCU!
Hila gani? Unamaanisha TCU haijui majukumu yake? Una maanisha TCU hawana integrity, unamaanisha TCU ni wala rushwa? You have to qualify your statement. Huo ndio ujinga aliolishwa Rais hadi akaiponda CAS. Kama kuna mtumishi wa TCU alifanya ujinga kwanini asisiginwe yeye?
 
Wewe una maslahi na vyuo binafsi, au umetumwa na hivyo vyuo! Kwanini umchagulie mtu kusoma chuo fulani?

Fuatilia mambo yalikuwaje huko nyuma. Unaomba chuo unachotaka hata vinne, na vyote ukichaguliwa una-confirm kimoja, zile nafasi tatu katika vyuo vingine vinajazwa kwa second selection
 
Unaposema kuna vyuo vya ujanjaujanja haitofautiani na kuitukana TCU na serikali nzima. TCU huwa inafungia vyuo vyote vya ujanjaujanja na orodha ya vyuo vilivyositishiwa udahiri ama kufutwa ipo wazi hata kwenye website za TCU. Hivyo kusema kuna vyuo vya ujanjaujanja ni sawa na kusema TCU is bogus.

Sio kweli kuwa wanafunzi wanachaguliwa kwenye vyuo wanavyovipenda (first choice). Mwanafunzi anaechaguliwa kwenye chuo anachokipenda ni yule tu mwenye ufaulu mkubwa kuliko waombaji wengine alioomba nao kwenye kozi husika. Vinginevyo chuo kitalazimika kiwaache waombaji wengine wenye sifa kuliko zake kwa kutumia kujuana, undugu, rushwa, udini, ukanda, uwezo wa kulipa na sababu nyingene nje ya academic qualifications. Wanafunzi walioachwa kwa sababu hizi hawana choice wataenda chuo chochote halali wakasome kuepuka kubakia nyumbani mwaka mzima wasubiri kuomba kwenye chuo wanachokipenda.

Hivyo kwa ufupi unapotosha umma. Mfumo wa CAS ulikuwa unampeleka mwanafunzi kwenye first choice yake kama ufaulu wake unawazidi waombaji wengine. Taifa letu bado changa bado tunaendelea kujenga utaifa na uzalendo. Hakika JPM alidanganywa kuhusu CAS na wasiokuwa na nia njema kwa taifa.

CAS iliwaleta pamoja watoto wa taifa hili bila kujali matabaka. Sasa hivi chuo na taasisi inachagua nani asome kwake na nani asisome bila kujali sana sifa za kitaaluma za mwanafunzi. Chuo cha kiislam kingependa kuona majina mengi ya akina Abdallah, Omari, Zaina, Samia kuliko Rose, Antony, George, Glory nk. Hapa tunarudi nyuma kama taifa. Kuna vyuo havitaki kuona wanafunzi waliosoma shule za Kata kwa kisingizio kuwa hawataweza kulipa ada yao, huu ni msiba mkubwa kwa taifa kama upuuzi huu utaruhusiwa kusonga mbele.
"Sasa hivi chuo na taasisi inachagua nani asome kwake na nani asisome bila kujali sana sifa za kitaaluma za mwanafunzi."

Acha kupotosha umma. Huwezi kuchaguliwa chuo fulani kama hauna sifa za kuingia katika hiyo kozi. Ukiona mtu amejiunga kozi fulani, ujue ana vigezo vya kujiunga.
 
TCU ni taasisi inayodhibiti ubora wa elimu ya juu. Inakagua, inashauri, inaruhusu Na kusimamisha au kufuta vyuo visivyokidhi vigezo vya ubora. Hivyo, vyuo vyote ambavyo vinatoa mafunzo vimefikia vigezo (minimum) vya ubora wa kumudu kutoa mafuzo yaliyokusudiwa. Ingawa ni kweli vyuo vinatofautiana kwa ubora.

TCU ndiyo yenye takwimu za vyuo vikuu vyote kuhusu kozi, ubora na idadi ya wanafunzi wanaoweza kudahiriwa kwenye kila chuo pamoja na ada inayotozwa kwa kila chuo.

Kabla ya kufutwa na Rais JPM wanafuzi walikuwa wanatuma maombi ya kujiunga vyuo vikuu kwa kutumia CAS kuchagua kozi na vyuo na mfumo huo wa udahiri ulikuwa na uwezo wa kumpangia mwanafuzi kozi aliyoomba kwenye chuo alichoomba kulingana na ufaulu wake na idadi ya walioomba kozi hiyo kwenye chuo hicho. Na kama nafasi kwenye chuo hicho imejaa mfumo ulikuwa ukimpeleka kwenye chuo kingine chenye nafasi bila usumbufu na gharama ya ziada kwa mwanafunzi.

Sasa hivi wanafunzi lazima waombe wenyewe kwenye vyuo husika kwa gharama zao, hivyo mwanafuzi atalazimika kuomba vyuo zaidi ya kimoja kwa gharama za uombaji za kila chuo na chuo ndicho kinanachochagua wanafunzi wa kusoma kwenye chuo chao na kutuma majina TCU kwa uhakiki.

Kufanya hivi kuna hasara zifuatazo:
1. Mwanafunzi anatumia hela nyingi kwenye maombi ya nafasi vyuoni.
2. Wanafuzi wanarundikana kwenye chuo kimoja wakati kuna nafasi kwenye vyuo vingine.
3. Unatoa nafasi ya wazazi kutoa rushwa kubwa vyuoni ili watoto wao wachaguliwe kozi fulani kwenye chuo fulani.
4. Baadhi ya vyuo vimepata nafasi ya kuwabagua wanafunzi wanaotoka kaya maskini wenye hela za kudunduliza kulipia karo kubwa za vyuo vyao.
5. Utaratibu unatoa mwanya kwa watendaji wa vyuo kuchagua ndugu zao, kabila na rafiki zao kupata nafasi ya kusoma chuoni kwao na kuwaacha watoto wengine wenye ufaulu mkubwa kuliko walioingizwa chuoni.
6. Mfumo unatoa mwanya wa UDINI kwenye selection. Anaechagua nani achaguliwe anaweza kusukumwa na vionjo vya udini na dhehebu lake kupatia nafasi kwanza watoto wa dini na dhehebu lake hata kama walioachwa wana ufaulu mkubwa kuliko waliopendelewa.

7. Vyuo vinadahiri kupita uwezo wao waliokadiriwa.

Faida zilizokusudiwa za utaratibu huu wa sasa ni moja tu, kuwa mwanafunzi atachagua chuo anachokitaka yeye. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa hata kwenye utaratibu huu sio kweli kuwa wanafunzi wote wanachaguliwa kwenye vyuo walivyovitaka, bado wanaendelea kudahiriwa kwenye vyuo vyenye nafasi kama zamani baada ya kukosa nafasi kwenye vyuo wanavyovipenda.

Wanafunzi na wazazi wanadanganywa na majina ya vyuo kumbe elimu ni ileile hata kwa vyuo vingine.

Kudhibitisha ukweli huu TCU ipitie ufaulu wa wanafunzi wote walioomba kwenye vyuo ilinganishe na ufaulu wa wanafunzi wote waliodahiriwa kwenye vyuo wataogundua dhambi hii ya ubaguzi.
Mtoa mada unauumiza moyo wangu katika jambo alilolifanya mwendazake la maaana ni pamoja.na hili mimi huo mfumo ulinipeleka IFM na niliweka last option na nichuo ambacho nilikua sikipendi imesababisha mpaka nisimalize degree yangu yan huu mfumo mpya mzuri sanaaa najutaaa yan bora huu mfumo mpya ningeenda kusoma chuo cha ndoto yangu UDSM
 
"CAS iliwaleta pamoja watoto wa taifa hili bila kujali matabaka"

Yaani matabaka unayaona kuanzia chuo kikuu au unapaswa uyakemee kuanzia shule za msingi?! Huko chuo kikuu ni kumalizia tu elimu. Acha wahitimu wawe huru kusoma vyuo wanavyovitaka.

Ipo hivi, vyuo bora lazima vitagombaniwa na wahitimu. Hivyo, mwenye ufaulu wa juu ndiyo atapata nafasi.

Huwezi kusema eti vyuo vikuu vinafanana kwa kila kitu. Sema vyuo vikuu vya hapa bongo vilivyo hai vinakidhi vigezo vya TCU ndo mana havijafutwa, ila tofauti zipo katika vitu vya ziada, mfano usimamizi wa tafiti, muda wa kufanya tafiti, vifaa, kujituma kwa walimu nk.

Matabaka yapingwe huku chini ambapo kuna gap kubwa kati ya shule za serikali na binafsi, vijijini na mijini.
 
Wewe una maslahi na vyuo binafsi, au umetumwa na hivyo vyuo! Kwanini umchagulie mtu kusoma chuo fulani?

Fuatilia mambo yalikuwaje huko nyuma. Unaomba chuo unachotaka hata vinne, na vyote ukichaguliwa una-confirm kimoja, zile nafasi tatu katika vyuo vingine vinajazwa kwa second selection
Hata sasa watoto hawasomi vyuo wanavyovitaka (wish) wao. Wengi wanachangua vyuo vya serikali sio kwasababu wanavipenda au ni bora kuliko vingine bali uwezo wa wazazi kumudu kulipa ada. Vyuo vya serikali vinaendeshwa kwa Kodi za wananchi hivyo ada yake ni ndogo sana, hii inasababisha watoto wengi wasipate nafasi kwenye vyuo hivyo na kuishia kwenda vyuo vingine bila kupenda.

Hivyo usiudanganye umma kuwa Siku hizi watoto wanasoma kwenye vyuo wanavyovipenda. Ili uweze kusoma kwenye chuo unachokipenda lazima ama ufaulu wako uwe mkubwa sana au atumie rushwa, kujuana, umaarufu, ukabila, udini, au mtoto wa mkubwa/kigogo.
 
"Sasa hivi chuo na taasisi inachagua nani asome kwake na nani asisome bila kujali sana sifa za kitaaluma za mwanafunzi."

Acha kupotosha umma. Huwezi kuchaguliwa chuo fulani kama hauna sifa za kuingia katika hiyo kozi. Ukiona mtu amejiunga kozi fulani, ujue ana vigezo vya kujiunga.
Inaonekana wewe hujui sana mambo haya. TCU huwa inatoa minimum qualifications (entry qualifications) yaani kiwango cha chini cha mwanafunzi kujiunga na kozi fulani. Mfano inaweza kusema kiwango cha kusoma udakatari lazima upate angalau alama D kwenye masomo ya Physics, chemistry na biology. Sasa ufisadi unaofanyika kwa mfumo wa sasa wa udahiri ni kwamba kwa sababu anazozifahamu yeye chuo kina mamlaka ya kumchagua mwanafunzi mwenye DDD na kumuacha yule mwenye ufaulu wa CCC au BBB au DCD au CCB, etc. Yaani kama mwanafunzi ana ufaulu wa DDD na ana hela za kulipa ada atachaguliwa na kumuacha yule mwenye ufaulu wa CCB lakini ana hela za kudunduliza. Hivyo hivyo MTU anaweza kuwachangua wenye ufaulu mdogo kwa rushwa, udini, ukabila na kuwaacha wanafunzi wenye sifa kubwa za kuchaguliwa. Kumbuka kuwa kila chuo kimepewa idadi ya wanafunzi kinachoweza kuwadahiri kwa mwaka kwa kila kozi.
 
Hakika, irudishwe...
Nakwambia kwa utaratibu wa sasa wa sasa wanafunzi wenye ufaulu wa point 10, 9, Na 8 wameachwa Na kudahiriwa watoto wenye ufaulu wa points 6 Na 7 vyuoni kwa sababu za rushwa, kujuana, mtoto wa kigogo, ndugu, ukabila, umaskini wa wazazi, udhehebu, nk.

Je, kwa mwendo huu tutafika?
 
Kwanza unawatengenezea hao watoto tatizo ambalo hawana na hawajaliona kama ni kero kwao.
Alafu unaishia kusema kuna Udini, ukabila na Rushwa bila kusema wazi ni wapi hapo kwenye hayo mambo.
 
Back
Top Bottom