TCU mnajua kuna wafanyakazi wamesitishiwa mshahara kwa ajili yenu?

mirindimo

JF-Expert Member
Nov 2, 2009
821
1,338
Hizi taasisi za serikali kuna haja ya kuzifumua na kuzijenga upya kwa kuweka watu ambao ni waadilifu na watakua tayari kuwatumikia watanzania. Tukianzia na TCU, hawa jamaa bado wana system ya business as usual yaani kama huna mtu unamfahamu hapa utasugua gaga mpaka utie akili.

Kuna mashirika watumishi wake wamesitishiwa mishahara yao kwa sababu hawajahakiki vyeti lakini ukiuliza watumishi hao wanakwambia wameshatuma vyeti vyao na taarifa zao kwenye mtandao wa TCU zaidi ya mwezi na jamaa wamekaa kimya hakuna anaehangaika kuhakiki. Hivi mnajua mnao watesa ni watanzania wenzenu, dada zenu kaka zenu mama zenu wadogo zenu. Kwani mna matatizo gani hapo ofisini?

Na ukifika pale utakuta wanacheza karata na game zingine kwenye kompyuta au simu zao. Wengine wamefungua site za udaku au wako snapchat au facebook.

Nafikiri kuna haja ya rais kuchapa viboko na kufukuza kazi siku moja watumishi wa aina hii.
 
Hata nyie mna matatizo mlishindwa nini kuhakiki vyeti kabla mkiisha kurupushwa ndio mnaenda kukurupusha wenzenu.
 
Hata nyie mna matatizo mlishindwa nini kuhakiki vyeti kabla mkiisha kurupushwa ndio mnaenda kukurupusha wenzenu.
Nahisi na wewe ni mcheza game ofisini pia,subirini kiama chenu kinakuja.Hata nilete bado dakika 2 huo ni wajibu wako
 
Mlipataje kazi bila vyeti kuhakikiwa?
We ni wale wale pia , kwanza elewa kazi inapatikana kuanzia na vyeti vya Diploma,Degree ukija Masters wengi wamesoma nje najaribu kukuelewesha yaelekea we umesoma Tz tu,sasa ukimaliza masomo yako nje ya nchi lazima jamaa wahakiki,hapo ndio shida inapoanzia hata ukipelemapema vipi kama pale ndani huna mtu wa kua ana push kidogo kila siku jamaa wakifika ofisini ni kuangalia leo Wema kapost nini.....we endelea kusubiri uhakiki.Sasa tamko linapokuja kutoka unakuta na wewe ulisha submit vyeti vyako lakini jamaa hawajatoa review zao !!
 
Moja ya vitu ambavyo havisumbui nchi hii ni kuhakiki cheti pale TCU.

Unapojaza fomu na ikikamilika....baada ya siku moja au mbili wewe mwenyewe ukiangalia mtandaoni utakuta wamekuandikia status na uende ukachukue lini. Hawanaga longolongo kabisa. Ndani ya siku saba unapata cheti chako.

Sema ninachokiona kwasasa (baada ya kukurupushwa huko makazini) pengine wamepokea maombi mengi hivyo kuchukua muda kuhakiki.

Angalizo;

Mwombaji awe anaangalia status yake kwasababu kama kuna kitu kimepungua huwa hawakupigii simu bali wanaandika status "kitu fulani kinatakiwa". Usipoangalia...utakua umekaa tu unasubiri cheti!
Ni kweli pengine wakati wanaanza hii kazi ya kuhakiki walikua committed na baada ya kuona wanaweza igeuza fursa wamebadilika,unachosema ni kweli na kila mda wanacheki status lakini ni zaidi ya mwezi sasa tangu kurekebisha walipotolea marekebisho status iko vile vile haijaguswa na mimi pia nilioneshwa nikashuhudia hilo nikasema ntalileta jamvini kulijadili na pengine wahusika wakiliona wanaweza litolea ufafanuzi.Kwa sababu tunaamini teknolojia hizi ni kwa ajili ya kurahisisha maisha na utendaji wa kazi zetu lakini wakati mwingine inapogeuka kua mwiba kwa watumiaji inakera kidogo
 
We ni wale wale pia , kwanza elewa kazi inapatikana kuanzia na vyeti vya Diploma,Degree ukija Masters wengi wamesoma nje najaribu kukuelewesha yaelekea we umesoma Tz tu,sasa ukimaliza masomo yako nje ya nchi lazima jamaa wahakiki,hapo ndio shida inapoanzia hata ukipelemapema vipi kama pale ndani huna mtu wa kua ana push kidogo kila siku jamaa wakifika ofisini ni kuangalia leo Wema kapost nini.....we endelea kusubiri uhakiki.Sasa tamko linapokuja kutoka unakuta na wewe ulisha submit vyeti vyako lakini jamaa hawajatoa review zao !!
Mimi nimesoma nje na cha kwangu walikihakiki ndani ya wiki mbili. Kulikoni ?
 
Back
Top Bottom