TCU kwa hili mmetukwaza watanzania

Njowepo

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
9,710
2,226
Kuna mwanafunzi jina kapuni alichaguliwa kwenda Zanzibar university na TCU baadae jamaa wa zenji wakasema wanafunzi wamekuwa wengi so waca cancel majina kibao na kuwaludishia TCU.
TCU wakafanya 2nd selection si ndo wakampanga jamaa chuo kingine kwa fani tofauti na ELIMU na ambayo hata hakuichagua.
Kwa juhudi zake binafsi akaenda TCU na form za moja ya vyuo vinavyotoa BA in Ed akawapelekea TCU ili wampe baraua ya utambulisho kwenye icho chuo bse 2nd selection wamempanga siko.
To my surprise TCU wakagoma na kumwambia akasome kwa iyo ya 2nd selection ambayo si ridhaa yake.
Nilipofuatilia kumbe si yeye mwenye ilo tatizo kulikuwa na vijana kama 20 ivi with similar case.
Maswali
1.Ivi TCU hawajui vyuo vya Tanzania kuwa wanaitaji wanafunzi wangapi katika fani Fulani mpaka wanapeleka wanafunzi kupita idadi?
2,Kama uzembe ni wao na mtu at last minutes anawapelekea option nao wanakataa ivi hawa TCU wana watoto wanawasomesha kweli ie ni wazazi?Bse huyu mwanafunzi inabidi asisome mwaka huu mpaka mwakani bse wamemwambia iyo 2nd selection haina mkopo ni kujilipia nae ni motto wa mkulima
3.Kwa nini wanatoa majibu mda mfupi kabla ya vyuo kufunguliwa labda watajitetea uchaguzi,je nao walikuwa bize na kazi ya uwakala?
4,Kwa nini wanamchagulia mtu option ambayo haipo kwenye selection zake na wala hakuisomea?

OMBI
TCU need to be more than serious sio kila mzazi ana uwezo wa kumlipia mwanae ada ya chuo hasa kwa majibu mnayoyatoa vijana wakija apo kwa ajili ya kufanya mabadiliko ambayo yanatokana na makosa yenu.

Kuweni wazalendo na mtambue si kila mtanzania anaweza jilipia ada ya chuo
 
When academic matters are being politisized!

Tanzani tuna safari ndefu!:redfaces:
 
Kuna mzungu aliwai nambia kuwa Tz you are not serious in everything sikutaka ata kupokea mifano toka kwake bse najua ni kweli
 
Siasa sasa imeshaingia kwenye elimu ya juu, na hayo ndo matunda yake
 
When academic matters are being politisized!

Tanzani tuna safari ndefu!:redfaces:

Baba Enock hapo kwenye red, mimi natofautiana nawe sana. tatizo ni irresponsibility. kuna baadhi ya watu hawataki kuwajibika katika makosa waliyofanya wao. Kosa hilo kimsingi sio hao madogo waliofanya. They are innocent.
Lijitu linalofahamu taratibu baada ya kuvurunda na linaonyeshwa kosa lake, halitaki kurekebisha na liko radhi hao madogo waadhibiwe kwa kukosa shule just kwa lenyewe kutokuwajibika ipasavyo hata baada ya kujulishwa kosa.

Na si ajabu hela hizo ikawa ndiyo yamegeuza kula yao kwa mwaka huu if linked with HELB.
 
Back
Top Bottom