comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 8,222
- 5,946
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezipiga faini ya Sh38.1 bilioni kampuni sita za simu kwa kosa la kutofikia viwango vya ubora wa huduma kama ilivyoanishwa na kanuni za ubora wa huduma za mwaka 2018.
Hata hivyo, mamlaka hiyo imezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie kuwekeza kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.
===
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezipiga faini ya Sh38.1 bilioni kampuni sita za simu kwa kosa la kutofikia viwango vya ubora wa huduma kama ilivyoanishwa na kanuni za ubora wa huduma za mwaka 2018.
Hata hivyo, mamlaka hiyo imezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie katika kuwekeza kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.
Kampuni hizo na faini zilizotozwa kwenye mabano ni ni Airtel (Sh11.5 bilioni), Tigo (Sh13 bilioni), Halotel (Sh3.4 bilioni), Vodacom (Sh7.8 bilioni), Zantel (Sh1 bilioni) na TTCL Sh1.3 bilioni.
Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba amesema mamlaka hiyo ilipima ubora wa huduma za mawasiliano katika robo ya mwisho ya mwaka 2020 na kubaini watoa huduma hao hawakufikia baadhi ya vigezo vya viwango vya ubora.
Amesema kwa mujibu wa kanuni ya 20 ya kanuni za ubora wa huduma za mawasiliano, mtoa huduma anayeshindwa kufikia vigezo anatakiwa kulipa faini.
“TCRA imeazimia kwamba badala ya kulipwa fedha hizo, tuzielekeze kwa watoa huduma. Kila mtoa huduma atumie kiasi chake alichotakiwa kulipa, akiwekeze katika kuboresha huduma.”
“Tunatoa siku tisini na tumekubaliana kwa kusaini hati ya makubaliano maalum, mtoa huduma atakayefanya kinyume TCRA itachukua hatua zaidi za kiudhibiti na kisheria pasipo kutoa taarifa,” amesema Kilaba.
Chanzo: Mwananchi
Hata hivyo, mamlaka hiyo imezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie kuwekeza kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezipiga faini ya Sh38.1 bilioni kampuni sita za simu kwa kosa la kutofikia viwango vya ubora wa huduma kama ilivyoanishwa na kanuni za ubora wa huduma za mwaka 2018.
Hata hivyo, mamlaka hiyo imezielekeza kampuni hizo kutozipeleka fedha hizo TCRA badala yake wazitumie katika kuwekeza kuboresha ubora wa huduma ndani ya siku 90.
Kampuni hizo na faini zilizotozwa kwenye mabano ni ni Airtel (Sh11.5 bilioni), Tigo (Sh13 bilioni), Halotel (Sh3.4 bilioni), Vodacom (Sh7.8 bilioni), Zantel (Sh1 bilioni) na TTCL Sh1.3 bilioni.
Mkurugenzi wa TCRA, James Kilaba amesema mamlaka hiyo ilipima ubora wa huduma za mawasiliano katika robo ya mwisho ya mwaka 2020 na kubaini watoa huduma hao hawakufikia baadhi ya vigezo vya viwango vya ubora.
Amesema kwa mujibu wa kanuni ya 20 ya kanuni za ubora wa huduma za mawasiliano, mtoa huduma anayeshindwa kufikia vigezo anatakiwa kulipa faini.
“TCRA imeazimia kwamba badala ya kulipwa fedha hizo, tuzielekeze kwa watoa huduma. Kila mtoa huduma atumie kiasi chake alichotakiwa kulipa, akiwekeze katika kuboresha huduma.”
“Tunatoa siku tisini na tumekubaliana kwa kusaini hati ya makubaliano maalum, mtoa huduma atakayefanya kinyume TCRA itachukua hatua zaidi za kiudhibiti na kisheria pasipo kutoa taarifa,” amesema Kilaba.
Chanzo: Mwananchi