TCRA yavipiga faini Vituo vya runinga ya Tsh. Mil 60 kwa kukiuka maadili ya uandishi na kutangaza habari za kichochezi

Kama Vipi media waache kutangaza habari za kisiasa na kuelimisha.

Yaani, program zoa zote wapige viburudisho mwanzo hadi mwisho kama soccer, muziki and the likes kwa muda wa mwezi mmoja tuone matokeo yake.

Any way, I am dreaming so don't take that piece of advice as a serious issue.

Hapana mimi naonelea vionyeshe CCM kwa kwenda mbele,kila kitu kuanzia Mwenyekiti anapoingia ofisini mpaka anapotoka hii ni pamoja na Latibu wa CCM na Msemaji Mkuu wa CCM,hii naona itapendeza sana itasaidia vituo hivi visipgwe fine kila wakati.

Hawa Tume ya Haki za Binaadamu watumie Citizen TV -Kenya,BBC,na Aljazira tutazitafuta tu hizi za nyumbani waziachie Lumumba
 
Bila mchuzi kumwagika tutakua mafala sana
tukisema ..wanasema tumeichoka Amani ..
kama katiba mpya haitopatikana bhasi tukubali kuendelea kuyaona haya mazingaombwe ...labda itokee chama tawala kibadilike kiutendaji ..yaaani waamua kuwa shetani mwenye mtazmo wakubadilika nakuwa malaika...jambo ambalo sioni kama linawezekana labda litawezekana katk zile simulizi za abunuasi tu...

kama mambo yataendelea kuwa hivi ..basi soon tutaskia kuna watu wameingia Amazon

[HASHTAG]#Atubu[/HASHTAG]
 
Dah ni hatari sana, pesa ngumu wengine sidhani kama Kodi wamemaliza kulipa wanashushiwa fine nyingi.
 
Dada wa marekani faini yake sh ngap mbona sijaona ufafanuzi wake maana napo kuna uchochezi kule...hivo vifungieni tu maana mnataka kusifiwa tu
 
Star tv NA azam 2 KWA KUWA WAMEKUBALI NA KUFYATA MKIA WAMETOZWA FAINI NDOGO

Ch. 10, ITV na EATV KWA KUWA WAMESMAMIA UKWELI KUWA WALIKUWA SAHIH WAMEPGWA FAINI NDEFU, HUU NI UONEVU UNAOPASWA KUPINGWA HADI NA SHETANI

TBC1 INATANGAZA UONGO KILA UCHAO LAKN HAWACHUKULIWI HATUA.

KIONGOZI DHAIFU HUOGOPA MEDIA
 
Naipongeza sana serkali kwa hatua hii...

Kila MTU ajitathimini kile anachosambaza
 
TCRA wakitolea uamuzi juu ya vituo vya habari vilivyo kiuka kanuni za utangazaji ambavyo ni ITV, CHANNEL TEN, EAST AFRICA TV, na AZAM 2 Tv.

Vituo hivi virusha maoni ya kituo cha sheria na haki za binadamu juu ya kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi wa marudio ya madiwani kuwa uligubikwa na vurugu na ni hatari kwa mwelekeo wa taifa kwa schaguzi zijazo.

vilitoa katika taarifa ya habari


Wanaohusika wenyewe ni watu ambao hata TV hawaangalii na kama wanaangalia sidhani kama wanakumbuka walichokiona. Dementia people. Stupid and retarded in their mind by kulazimishwa kufanya wasichokiamini.
 


Uamuzi kuhusu shauri namba 4 la mwaka 2017/18 dhidi ya Star Television.

Kupitia kipindi chake cha taarifa ya habari kilichorushwa kati ya saa mbili usiku kikisema kuwa uchaguzi ulikuwa na uvunjifu wa haki za binadamu juu ya vyombo vya dola

Kwa kurusha taarifa hiyo kituo cha Star Television kinatuhumiwa kukiuka sheria zifuatazo;
  • Kutangaza habari za uchochezi zinazoweza kuhatarisha amani ya nchi na taifa kinyume na kanuni za utangazaji za mwaka 2015
  • Kukiuka maadili ya uandishi kwa kutangaza habari zisizokuwa na mizania na kinyume ya kanuni ya utangazaji
Sehemu ya habari hiyo ya StarTv ni hii hapa kwa nukuu "Mwenyekiti wa chama Chadema tawi la Dar es Salaam, ndugu Dikson ambaye alijeruhiwa vibaya sana na kuonekana kuwa amelazwa katika wodi kwa sababu ya uchaguzi, Picha ya chini tunaona mawakala wa chadema wa Arumeru ambao alishambuliwa na mapanga wakiwa wanatimiza wajibu wao"

"Ukiukwaji huo wa haki za binadamu umehusihwa kupigwa kwa binadamu na kukamatwa kwa baadhi ya viongozi wa kisiasa pamoja na kubuguziwa kwa mawakala mbalimbali. Kumekuwa na vitendo vya matumizi mabaya ya nguvu na vyombo vya dola, matukio ya watu kutwekwa na watu wasijulikana, watu kupigwa na vitendo hivi vimeripotiwa kufanywa na vyombo vya dola na watu wasiojulikana wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa vyama vya siasa"

Wito wa kufika kwenye kamati ya maudhui
Tarehe 5/12/2017 uongozi wa Star Tv uliitwa kutoa utetezi kwanini wasichukuliwe hatua kwa kukiuka kanuni za utangazaji;

Baada ya kuwaita, kamati na hao viongozi ilipata nafasi ya kutazama kipindi ili kujua kama ilikiuka kanuni za utangazaji.

Uongozi wa Star Tv ulitoa utetezi kama ifuatavyo:
1.Vyombo vya habari vya habari vilikaribishwa kwenye mkutano wa kituo cha sheria na haki za binadamu kwa lengo la kuzungumzia tathmini ya uchaguzi mdogo.

2.Walisikitishwa na taarifa iliyotolewa na taasisi ya kituo cha sheria na haki za binadamu, taarifa hiyo ilikuwa na makosa lakini mhariri wa zamu hakuyaona na kwamba hakupaswa kutangazwa bila kuifanyia marekebisho.

3.Star Tv walishachukua hatua za ndani kwa mhariri ili kuhakikisha suala hilo halijirudii.

4.Star Tv walieleza kuwa si tu kuwa taarifa hiyo ilikiuka kanuni za utangazaji bali ilikiuka sera ya kituo chao.

Star Tv waliomba radhi kwa taarifa isiyozingatia kanuni za utangazaji

Star Tv wamekiuka kanuni namba sita ya kanuni ya utangazaji;
Pamoja na kwamba taarifa hiyo ilikuwa inaihusu tume ya uchaguzi hawakuwasiliana na tume ya uchaguzi kupata undani wa taarifa hiyo. Pia hawakuwasiliana na jeshi la polisi ili kupata mizania ya habari hiyo.

Kamati imeitazama taarifa hiyo na utetezi wa Star Tv

Pamoja na kukiri kutenda kosa, kamati imejiridhisha kuwa imekiuka kanuni za utangazaji za mwaka 2015.

Baada ya kubaini makosa hayo, kamati ya maudhui inaamua yafuatayo

1.Star Tv inatozwa faini ya shilingi milioni 2 na nusu kwa kosa la kutangaza habari za uchochezi.
2.Star Tv inatozwa faini ya shilingi milioni 2 na laki tano kwa kutangaza kanuni za utangazaji.
3.Kwa kutozingatia mizania ya habari Star Tv inatozwa shilingi milioni 2 na laki 5

Kwa makosa yote Star Tv inatozwa shilingi za kitanzania milioni 7 na laki 5
Faini hiyo inatakiwa kulipwa ndani ya siku 30. Pia Star Tv inawekwa chini ya uangalizi maalum wa TCRA.
Uamuzi huu umetolewa leo tarehe 2/01/2017

Sasa tunasoma uamuzi unaohusu shauri namba sita mwaka 2017/18 unaohusu azamu two.

Kituo cha azam two, kinatuhumiwa kukiuka kanuni za utangazaji katika kipindi cha tarehe 30/11/2017.
=>Kilitangaza tathmini ya kituo cha sheria za haki za binadamu. Kwa kurusha taarifa hiyo, kutuo cha azam two kilikiuka kanuni zifuatazo;

Wito wa kufika mbele ya kamati ya maudhui

Azam two waliitwa mbele ya kamati ya maudhui ili wajitetee kwanini wasichukuliwe hatua

Malelezo ya azam

=>Walikiri na kukubali kutangaza habari hiyo
=>Kwa ujumla waandishi walijitahidi kwa uwezo wao kupata maelezo ya ziada kutoka tume ya uchaguzi lakini hawakufanikiwa. Kutokana na hili ndipo walipofanya uamuzi ambao haukuwa wa busara.

=>Ilikuwa imeandaliwa mkurugenzi atoe ufafanuzi lakini hakuwa tayari maana alikuwa kwenye mkutano.

=>Azam two waliahidi kuhakikisha waandishi wao wanazingatia weledi kwa kuweka uzalendo mbele.

Azam two;

Nimalizie kwa kukuomba radhi wewe na kamati yako

Kwa kuzingatia azam two wametenda makosa, kamati imeamua yafuatayo;

1.Azam inatozwa milioni 2 na laki 5 kwa kutangaza habari za uchochezi
2.Azam two inatozwa milioni 2 na laki 5 kwa kutangaza habari zisizozingatia maadili
3.Kwa kutozingatia mizania azam two inatozwa milioni 2 na laki 5.

Jumla azam two inatozwa jumla ya shilingi milioni 7 na laki 5

Pia azam two inawekwa chini ya uangalizi maalum wa TCRA kwa miezi 6


Uamuzi huu umetolewa na kusomwa leo tar 02/01/2018

Shauri kuhusu kituo cha East Africa Television

Kamati imeangalia maelezo ya East Africa Televisheni
Pamoja na kutokiri kutenda kosa, kamati imejiridhisha, kituo cha East Africa Television kimekiuka kanuni za huduma za utangazaji.

Uamuzi wa kamati
Kamati ya maudhui imejiridhisha kipindi cha Hotmix kimekiuka kanuni za utangazaji na imeamua yafuatayo;

1.EATV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa kutangaza habari za uchochezi
2.EATV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa kutangaza habari zisizozingatia maadili
3.EATV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa kutozingatia mizania ya utangazaji.

Jumla EATV inatozwa faini ya milioni 15, faini inapswa kulipwa ndani ya siku 30

Pia EATV inawekwa chini ya uangalizi wa TCRA kwa miezi 6

Shauri namba tano mwaka 2017/18 kuhusu kituo utangazaji wa channel ten

Kituo cha utangazaji cha channel ten kinatuhumiwa kurusha taarifa inayokiuka kanuni za utangazaji.

Kituo cha channel ten kilirusha habari ya kituo cha haki za binadamu tathmini ya kituo cha sheria na haki za binadamu.

Utetezi wa channel ten ni kwamba ilitolewa na taasisi iliyosajiliwa.Pili tathmini ya kituo cha sheria na haki za binadamu ililenga kuutahadharisha umma. Channel ten wanasema taarifa hiyo ilikuwa na ushahidi wa picha. Nne kituo cha sheria na haki za binadamu ni chombo kilichosajiliwa kisheria nchini.

Katika kutoa majumuisho yao channel ten walisema kamati ipokee utetezi wao na kusitisha kusudio la kuichukulia hatua.

Kutokana na tathmini na baada ya kusikiliza uetetezi, kamati ya maudhui imejiridhisha chanel ten imekiuka kanuni za utangazaji;

Kamati imetoa uamuzi ufuatao;

1. Channel ten inatozwa sh milioni 5 kwa kosa la uchochezi
2.Channel ten inatozwa faini ya milioni 5 nyingine kwa kuzingatia kanuni za uandishi
3. Kwa kosa la kutozingatia mizania channel ten inatozwa sh milioni 5 pia.

Faini inatakiwa kulipwa ndani ya siku 30, pia channel ten inawekwa chini ya uangalizi kwa miezi 6.

Uamuzi kuhusu shauri namba tatu la mwaka 2017/18 la kituo cha utangazaji cha ITV;

Kituo cha ITV kinatuhumiwa kurusha habari za uchochezi kilichorushwa tarehe 30 Nov 2017. Kilirusha habari za kituo cha sheria na haki za binadamu kuhusu tathmini ya uchaguzi mdogo.

Utetezi wa ITV;
1.ITV walithibisha kutangaza habari hiyo tarehe 30 Nov 2017, walisema ililenga kuthibiti uwezekano wa kutokea vurugu.

2. Madhui hayakuwa ya uchochezi na Habari hiyo haikulenga kutokea vurugu.

3.Maadili ya uandishi yalizingatiwa na hakukuwa na taarifa ya Jeshi la polisi au tume ya uchaguzi kukanusha.

4.Taarifa ililenga kuishauri serikali

5.Walijiridhisha kuwa lengo kuu la tamko na kauli zilizotolewa hazikuwa za uchochezi

6. Walihakiki na kujiridhisha kuwa taasisi hii imesajiliwa kisheria.

Katika kujumuisha utetezi wao ITV walisema;
Taarifa ililenga kuishauri serikali, ilizingatia mizania na kwamba kituo chao hakikukiuka kanuni za utangazaji.

Kamati ya maudhui inaamua yafuatayo.

1.ITV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa kutangaza habari za uchochezi
2.ITV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa kutangaza habari ambazo hazikuzingatia maadili ya uandishi
3.Kwa kutozingatia mizania ITV inatozwa faini ya shilingi milioni 5

Kwa makosa yote ITV inatozwa faini ya sh milioni 5 kwa makosa yote matatu.
Faini hiyo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30.

Haki ya kukata rufaa kwenye baraza la kibiashara uko wazi.

Kwa vile haya masuala ni ya kisheria haturuhusu maswali, ndiyo maana hapa tumeweka kipengele kwamba watu wana haki ya kukata rufaa, tukianza kuuliza maswali tutaingilia mkondo wa kisheria.

Udikteta ndani ya kazi. Tunarudi enzi za Mkoloni na mahakama yake
 
Labda nikusaidie kueleza nilivyomuelewa.
Vituo tajwa hapo juu vimetozwa faini kwa kosa la kutangaza taarifa inayoelezwa na tcra kua na maudhui ya kichochezi. Habari hii chanzo chake ni tathmini iliyofanywa na kituo cha haki za binadamu (hiyo ripoti|tathmini ndiyo ilitangazwa na vituo hivyo vya habari) hivyo basi, kama taarifa hiyo ilikua na uchochezi basi hata kituo cha haki za binadu wanapaswa kuwajibishwa kwa kutoa taarifa ya kichochezi. Kwamaana nao washughulikiwe kama wachochezi wengine kwa sheria kufuata mkondo wake. Nadhani nimeweza kukusaidia pale ambapo hukuelewa alipoeleza mkuu hapo.
Na haswa wao ndo wangekamatwa kwa kuleta habari za uchochezi, mbna hawakuchukuliwa hatua yyte ile wao?
 
Kwa mara ya kwanza Tanzania ndio naliona hilo. Ni kanuni tu? Au kuna jambo lingine?
 
Back
Top Bottom