Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,395
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA(TCRA) YATOA ONYO KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUAJIRI WATANGAZAJI WASIO NA TAALUMA.
Mamlaka ya Mawasiliano nchini imetoa onyo kwa vyombo vya habari hususani redio na televisheni kwa kile inachodai kuwa vyombo hivyo vimekua na tabia ya kuajiri watangazaji wasio na taaluma hiyo.
Katika tarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo Septemba 14 imewataka wamiliki wa vyombo hivyo kuzingatia matakwa ya sheria na masharti ya leseni ya utangazaji kwa kuhakikisha kuwa wanaotangaza katika vyombo vyao wana vigezo vya kitaaluma kama waandishi wa habari.
Mamlaka hiyo imefafanua kuwa kwa mujibu wa sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kifungu cha 19(1) kinaeleza kuwa kufanya kazi kama mwandishi wa habari pasipo kuthibitishwa kwa mujibu wa sheria ni kuvunja sheria na kwa mujibu wa kanuni ya 17(2) ya vyombo vya habari ya mwaka 2017 ili mtu athibitishwe kuwa mwandishi pamoja na mambo mengine anatakiwa kuwa na shahada au stashahada ya uandishi wa habari au inayohusiana na masuala ya vyombo vya habari kutoka chuo kinachotambulika kinachotoa elimu ya masuala hayo au shahada au stashahada ya masuala ya Vyombo vya Habari.
Kuwa na watangazaji wasio na elimu juu ya masuala ya habari na utangazaji kunapelekea kutendeka kwa makosa mengi ya kutozingatia miiko ya uandishi na utangazaji wa habari, hivyo kuwa kinyume na matakwa ya kifungu cha 7(2)(a)(iii) cha sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kinachotaka vyombo vya habari kuzingatia misingi na miiko ya uandishi wa vyombo vya habari.
Aidha, Mamlaka imevikumbusha na kuvionya vyombo vya habari kuwa hatua zaidi zitachukuliwa, ikiwa ni pamoja na kutoza faini, au kufuta leseni ya chombo chochote kitakachokiuka masharti ya leseni, kanuni na Sheria.
Ikumbukwe kuwa mamlaka hiyo ilitoa taarifa kuwa mpaka kufikia mwaka 2021 Vyombo vyote vya Habari vinatakiwa kuwa na waandishi na watangazaji waliokidhi vigezo vya kitaaluma.
Mamlaka ya Mawasiliano nchini imetoa onyo kwa vyombo vya habari hususani redio na televisheni kwa kile inachodai kuwa vyombo hivyo vimekua na tabia ya kuajiri watangazaji wasio na taaluma hiyo.
Katika tarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo Septemba 14 imewataka wamiliki wa vyombo hivyo kuzingatia matakwa ya sheria na masharti ya leseni ya utangazaji kwa kuhakikisha kuwa wanaotangaza katika vyombo vyao wana vigezo vya kitaaluma kama waandishi wa habari.
Mamlaka hiyo imefafanua kuwa kwa mujibu wa sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kifungu cha 19(1) kinaeleza kuwa kufanya kazi kama mwandishi wa habari pasipo kuthibitishwa kwa mujibu wa sheria ni kuvunja sheria na kwa mujibu wa kanuni ya 17(2) ya vyombo vya habari ya mwaka 2017 ili mtu athibitishwe kuwa mwandishi pamoja na mambo mengine anatakiwa kuwa na shahada au stashahada ya uandishi wa habari au inayohusiana na masuala ya vyombo vya habari kutoka chuo kinachotambulika kinachotoa elimu ya masuala hayo au shahada au stashahada ya masuala ya Vyombo vya Habari.
Kuwa na watangazaji wasio na elimu juu ya masuala ya habari na utangazaji kunapelekea kutendeka kwa makosa mengi ya kutozingatia miiko ya uandishi na utangazaji wa habari, hivyo kuwa kinyume na matakwa ya kifungu cha 7(2)(a)(iii) cha sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kinachotaka vyombo vya habari kuzingatia misingi na miiko ya uandishi wa vyombo vya habari.
Aidha, Mamlaka imevikumbusha na kuvionya vyombo vya habari kuwa hatua zaidi zitachukuliwa, ikiwa ni pamoja na kutoza faini, au kufuta leseni ya chombo chochote kitakachokiuka masharti ya leseni, kanuni na Sheria.
Ikumbukwe kuwa mamlaka hiyo ilitoa taarifa kuwa mpaka kufikia mwaka 2021 Vyombo vyote vya Habari vinatakiwa kuwa na waandishi na watangazaji waliokidhi vigezo vya kitaaluma.