May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,162
- 8,820
Kama ilivyo kawaida yangu leo nilikuwa nafuatilia moja ya vipindi ninavyopenda kusikiliza kupitia Redio Free Africa...Kipindi kinaitwa "sintosahau".
Si mara ya kwanza nimeona kuna mapungufu mahali na sijui kama Mamlaka huwa zinafuatilia, au labda kwao sio tatizo...mara kadhaa nimeshasikia Msimuliaji akiachwa tu kuzihusisha Taasisi za Nchi au hata kutaja Majina ya watu wenye Mamlaka au waliowahi kuwa kwenye Mamlaka, sidhani kama hii ni sawa.
Nilishasikia Msimuliaji hapo hapo Free Africa wakati mmoja akimtaja kwa jina aliyekuwa Kamanda au Mkuu wa kituo wa sehemu wakati anaelezea mkasa wake.
Leo walikuwa wanamuhoji Jambazi Mstaafu, Bw Edgar Charles, let's hope kwamba hilo sio jina lake halisi, na kama ni halisi sioni kama imekaa sawa hii hata kwa usalama wake Msimuliaji...nadhani inaweza kuwa sio shida kama Muhusika sasa ni Mtu mzima na ni Kiongozi wa kiimani aliyeamua kwa utashi wake kwamba sasa hana cha kuficha wala kuogopa kwani anaongozwa na imani yake.
Huyu bw amehusisha Jeshi (JESHI) alipoongelea namna walivyokuwa wanapata silaha, mimi si Mtaalamu lakini siamini kama hii ni sawa...ni sawa kama angewapa taarifa wahusika lakini sio hadharani maana hakuna wa kuthibitisha au kukanusha.
Huwa nafuatilia kipindi cha Dokta Isack, kila nikisikiliza naweza kugundua kabisa kwamba kunakuwa na umakini sana Msimuliaji asitoke kwenye mstari, Dokta atamtahadharisha Msimuliaji kabla hajajibu swali, au kumkatisha maelezo akigundua anakoelekea siko.
Mimi si Mwanahabari lakini nadhani kuna mambo ningetanguliza tu 'common sense' nje ya taaluma.
Vipi usalama wa Msimuliaji mwenyewe iwapo waliokuwa 'wamemuajiri' watasikiliza na kuona kama huyu Jamaa atatuharibia jina?...Vipi waliopo kazini nao (haswa wa upande wa usalama) wakihisi siri zao zinatolewa na Mtu waziwazi na wanamjua?.
"Wanasemaga tulikuwa tunarushiana risasi na Majambazi tukafanikiwa kuwazidi nguvu" hii si ni siri ya Geshi jameni?.
Si mara ya kwanza nimeona kuna mapungufu mahali na sijui kama Mamlaka huwa zinafuatilia, au labda kwao sio tatizo...mara kadhaa nimeshasikia Msimuliaji akiachwa tu kuzihusisha Taasisi za Nchi au hata kutaja Majina ya watu wenye Mamlaka au waliowahi kuwa kwenye Mamlaka, sidhani kama hii ni sawa.
Nilishasikia Msimuliaji hapo hapo Free Africa wakati mmoja akimtaja kwa jina aliyekuwa Kamanda au Mkuu wa kituo wa sehemu wakati anaelezea mkasa wake.
Leo walikuwa wanamuhoji Jambazi Mstaafu, Bw Edgar Charles, let's hope kwamba hilo sio jina lake halisi, na kama ni halisi sioni kama imekaa sawa hii hata kwa usalama wake Msimuliaji...nadhani inaweza kuwa sio shida kama Muhusika sasa ni Mtu mzima na ni Kiongozi wa kiimani aliyeamua kwa utashi wake kwamba sasa hana cha kuficha wala kuogopa kwani anaongozwa na imani yake.
Huyu bw amehusisha Jeshi (JESHI) alipoongelea namna walivyokuwa wanapata silaha, mimi si Mtaalamu lakini siamini kama hii ni sawa...ni sawa kama angewapa taarifa wahusika lakini sio hadharani maana hakuna wa kuthibitisha au kukanusha.
Huwa nafuatilia kipindi cha Dokta Isack, kila nikisikiliza naweza kugundua kabisa kwamba kunakuwa na umakini sana Msimuliaji asitoke kwenye mstari, Dokta atamtahadharisha Msimuliaji kabla hajajibu swali, au kumkatisha maelezo akigundua anakoelekea siko.
Mimi si Mwanahabari lakini nadhani kuna mambo ningetanguliza tu 'common sense' nje ya taaluma.
Vipi usalama wa Msimuliaji mwenyewe iwapo waliokuwa 'wamemuajiri' watasikiliza na kuona kama huyu Jamaa atatuharibia jina?...Vipi waliopo kazini nao (haswa wa upande wa usalama) wakihisi siri zao zinatolewa na Mtu waziwazi na wanamjua?.
"Wanasemaga tulikuwa tunarushiana risasi na Majambazi tukafanikiwa kuwazidi nguvu" hii si ni siri ya Geshi jameni?.