Mimi ni mteja wa Vodacom nikiwa na line yao na pia line yao ya internet. Nimekuwa nikinunua kifurushi chao kila mwezi kwa gharama ya Tshs. 35,000 na kifurushi hiki kwa siku za nyuma nilikuwa ninakitumia kwa mwezi mzima.
Nimeendelea kununua kifurushi cha GB10 kwa Tshs. 35,000 ili nikitumie kwa mwezi mzima lakini kwa siku za karibuni tarehe 27.11.2019 nilinunua kifurushi tena cha GB10 kwa Tshs. 35,000 ili nikitumie kwa mwezi mzima lakini cha ajabu tarehe 30.11.2019 nilipata taarifa kupitia simu yangu kuwa sina salio kwenye kifurushi changu yaani baada ya siku tatu sina salio?.
Serikali imewekwa na wananchi pale penye matatizo ni budi serikali isaidie wananchi wake. Kitendo kama hiki kinatakiwa kifuatiliwe na huu ni wizi wa mchana. Ninaiomba TCRA iingilie kati suala hili.
Nimeendelea kununua kifurushi cha GB10 kwa Tshs. 35,000 ili nikitumie kwa mwezi mzima lakini kwa siku za karibuni tarehe 27.11.2019 nilinunua kifurushi tena cha GB10 kwa Tshs. 35,000 ili nikitumie kwa mwezi mzima lakini cha ajabu tarehe 30.11.2019 nilipata taarifa kupitia simu yangu kuwa sina salio kwenye kifurushi changu yaani baada ya siku tatu sina salio?.
Serikali imewekwa na wananchi pale penye matatizo ni budi serikali isaidie wananchi wake. Kitendo kama hiki kinatakiwa kifuatiliwe na huu ni wizi wa mchana. Ninaiomba TCRA iingilie kati suala hili.