Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 18,590
- 22,200
TCRA mlituingiza kwenye mfumo wa alama za vidole kwenye laini za simu tukidhani mmeamua kutulinda dhidi ya wahalifu wanaotumia laini za simu holela, kumbe sivyo kwani bado wapo!
TCRA wamiliki wa ving'amuzi hupandisha bei za vifurushi huku picha ni za zamani na marudiomarudio miaka nenda miaka rudi!
Wamiliki wanatuuzia vifurushi ndani ya mifuko myeusi ya plastiki! Yaani hatupewi vipeperushi vya nini kilichomo ndani ya vifurushi! Nyie hamjali mnajionea sawa, hebu pitieni vifurushi vipya vya Azam muone tunavyopigwa, kwa kifupi wamepandisha bei.
TCRA wamiliki wa ving'amuzi hupandisha bei za vifurushi huku picha ni za zamani na marudiomarudio miaka nenda miaka rudi!
Wamiliki wanatuuzia vifurushi ndani ya mifuko myeusi ya plastiki! Yaani hatupewi vipeperushi vya nini kilichomo ndani ya vifurushi! Nyie hamjali mnajionea sawa, hebu pitieni vifurushi vipya vya Azam muone tunavyopigwa, kwa kifupi wamepandisha bei.