Nimeshawishika kuandika mada hii baada ya kuona rais Samia kalizungumzia suala la umuhimu wa TEHAMA, alipofanya mahojiano na gazeti la mwanachi la March 17, 2022.
Wadau wa Blog tuliathiriwa pakubwa sana na sheria ya kusajili blogu kwa kulipia. Wengine tulilazimika kuzifunga blogu zetu kwa sababu tulikuwa hatupati faida ya fedha, zaidi ya kutoa elimu kwa jamii. Tukaona, isiwe kesi, ngoja tufunge hizo blogu mana serikali inaona tunafaidi sana.
Sheria ile bado inafanya kazi mpaka sasa, ijapokuwa TCRA walipunguza viwango vya bei, lakini hata viwango vilivyopo ni gharama kubwa kwa vijana.
Kiukweli sheria ile haifai hata kidogo kwa nchi inayoendelea kama Tanzania, kwani inarudisha nyuma maendeleo ya TEHAMA na ubunifu kwa vijana.
Naomba nieleweke, sipingi udhibiti wa hizi blogu, bali naunga mkono kuweka sheria mbalimbali ila napinga kwa nguvu zote TCRA kutoza gharama za usajili wa blogu. Kwani kuna ubaya gani TCRA wakazisajili bure na kuendelea kuzisimamia?
Yaani TCRA wanafanya blogu chanzo cha mapato, wakati blogu nyingi ni za vijana wahitimu wa chuo ambao hawana mitaji. Ni aibu!. Badala TCRA iwape mitaji wabunifu wa TEHAMA, yenyewe ndio inataka ipewe hela. Du!
Namnukuu rais Samia alipofanya mahojiano na Gazeti la Mwananchi tarehe 17-03-2022. Maelezo ya mh rais yemenipa nguvu ya kuiomba TCRA waondoe tozo kwa blogu, na Paypal iruhusiwe nchini ili vijana wajiajiri kupitia hii mitandao;
Mh rais Samia: "Lakini jingine ni kwamba sasa hivi ulimwengu unakwenda na mitandao, kwa hiyo tuna matarajio ya kuweka chuo kikubwa cha shughuli za mitandao, kufundisha vijana wetu ili wasiachwe na ulimwengu."
Mh rais Samia: "Waende na ulimwengu pamoja na ujuzi mbalimbali watakaokuwa nao, lakini kwenye kazi zao hizohizo kwa kiasi kikubwa watatumia mitandao, kutafuta utaalamu zaidi ni mitandao, kutafuta soko zaidi ni mitandao, kujua mtaji uko wapi ni mitandao, kila kitu ni mitandao, kwa hiyo tunakwenda kuweka mkazo kwenye hilo pia."
Maoni yangu; Ukisoma nukuu ya rais utagundua, rais anajuwa umuhimu wa mitandao katika ulimwengu wa sasa. Kupitia mitandao, watu wanaweza kutengeneza faida mfano kufanya biashara za mtandaoni.
Hicho cbuo kikubwa cha TEHAMA hakitakuwa na maana, kama kina TCRA wataendelea kuwatoza wahitimu gharama za kusajili blogu.
Pia, raisi anatakiwa afahamu, ni lazima njia za malipo lazima zirahisishwe, mfano Paypal iruhusiwe nchini. Hii itawasaidia vijana wapambanaji wa mitandao kupata fedha.
Tunatakiwa tufahamu kuwa, utandawazi una faida na hasara ila faida ni nyingi sana kuliko hasara.
Tatizo Watanzania huwa tunahisi hii nchi ni mbinguni, eti hatutaki tupate negatives za utandawazi hata kidogo. Utawasikia watu wakisema, ukiruhusu Paypal, basi tutaingiza pesa za kufadhili ugaidi au kutakatisha fedha.
Kwani kuna ugumu gani wa kufanya utafiti kwa nchi za Kiafrika kama yetu ili kubaini faida na hasara za Paypal na mitandao kwa ujumla?
Viongozi wa serikali fanyeni study tour kwa sababu inaonekana rais ana exposure kubwa kuliko mawaziri wake!
Soma mwenyewe mahojiano kati ya rais Samia na gazeti la Mwananchi (17-03-2022):
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Wadau wa Blog tuliathiriwa pakubwa sana na sheria ya kusajili blogu kwa kulipia. Wengine tulilazimika kuzifunga blogu zetu kwa sababu tulikuwa hatupati faida ya fedha, zaidi ya kutoa elimu kwa jamii. Tukaona, isiwe kesi, ngoja tufunge hizo blogu mana serikali inaona tunafaidi sana.
Sheria ile bado inafanya kazi mpaka sasa, ijapokuwa TCRA walipunguza viwango vya bei, lakini hata viwango vilivyopo ni gharama kubwa kwa vijana.
Kiukweli sheria ile haifai hata kidogo kwa nchi inayoendelea kama Tanzania, kwani inarudisha nyuma maendeleo ya TEHAMA na ubunifu kwa vijana.
Naomba nieleweke, sipingi udhibiti wa hizi blogu, bali naunga mkono kuweka sheria mbalimbali ila napinga kwa nguvu zote TCRA kutoza gharama za usajili wa blogu. Kwani kuna ubaya gani TCRA wakazisajili bure na kuendelea kuzisimamia?
Yaani TCRA wanafanya blogu chanzo cha mapato, wakati blogu nyingi ni za vijana wahitimu wa chuo ambao hawana mitaji. Ni aibu!. Badala TCRA iwape mitaji wabunifu wa TEHAMA, yenyewe ndio inataka ipewe hela. Du!
Namnukuu rais Samia alipofanya mahojiano na Gazeti la Mwananchi tarehe 17-03-2022. Maelezo ya mh rais yemenipa nguvu ya kuiomba TCRA waondoe tozo kwa blogu, na Paypal iruhusiwe nchini ili vijana wajiajiri kupitia hii mitandao;
Mh rais Samia: "Lakini jingine ni kwamba sasa hivi ulimwengu unakwenda na mitandao, kwa hiyo tuna matarajio ya kuweka chuo kikubwa cha shughuli za mitandao, kufundisha vijana wetu ili wasiachwe na ulimwengu."
Mh rais Samia: "Waende na ulimwengu pamoja na ujuzi mbalimbali watakaokuwa nao, lakini kwenye kazi zao hizohizo kwa kiasi kikubwa watatumia mitandao, kutafuta utaalamu zaidi ni mitandao, kutafuta soko zaidi ni mitandao, kujua mtaji uko wapi ni mitandao, kila kitu ni mitandao, kwa hiyo tunakwenda kuweka mkazo kwenye hilo pia."
Maoni yangu; Ukisoma nukuu ya rais utagundua, rais anajuwa umuhimu wa mitandao katika ulimwengu wa sasa. Kupitia mitandao, watu wanaweza kutengeneza faida mfano kufanya biashara za mtandaoni.
Hicho cbuo kikubwa cha TEHAMA hakitakuwa na maana, kama kina TCRA wataendelea kuwatoza wahitimu gharama za kusajili blogu.
Pia, raisi anatakiwa afahamu, ni lazima njia za malipo lazima zirahisishwe, mfano Paypal iruhusiwe nchini. Hii itawasaidia vijana wapambanaji wa mitandao kupata fedha.
Tunatakiwa tufahamu kuwa, utandawazi una faida na hasara ila faida ni nyingi sana kuliko hasara.
Tatizo Watanzania huwa tunahisi hii nchi ni mbinguni, eti hatutaki tupate negatives za utandawazi hata kidogo. Utawasikia watu wakisema, ukiruhusu Paypal, basi tutaingiza pesa za kufadhili ugaidi au kutakatisha fedha.
Kwani kuna ugumu gani wa kufanya utafiti kwa nchi za Kiafrika kama yetu ili kubaini faida na hasara za Paypal na mitandao kwa ujumla?
Viongozi wa serikali fanyeni study tour kwa sababu inaonekana rais ana exposure kubwa kuliko mawaziri wake!
Soma mwenyewe mahojiano kati ya rais Samia na gazeti la Mwananchi (17-03-2022):
Rais Samia: Tutafanya mabadiliko kwenye elimu, polisi
Rais Samia Suluhu Hassan amesema mapendekezo yaliyotolewa na tume zilizoundwa kuchunguza matukio yaliyofanywa na baadhi ya askari polisi baada ya malalamiko ya wananchi yataleta “mabadiliko...
www.mwananchi.co.tz
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app