TCRA naombeni majibu haya kabla ya kuhitaji alama za vidole za kila mmiliki line, je technology ya kisasa imewashinda?

Fingerprint bado ni valid mkuu. Security wise hizo mbinu zote ulizotaja mtu akiwa makini anaweza asijulikane akifanya uhalifu, ila fingerprint hata kama hatujamkamata lkn tutajua kuwa huyu ni fulani. Hili zoezi limefanyiwa careful scrutinization na wataalam wa teknohama, cybersecurity, security na forensic investigation experts, usidhani ww unajua kuliko wenzako mkuu.

Changamoto ulizotaja ni ndogo sana, zinatatulika kirahisi tu. Watz huwa hawaoni umuhimu wa vitambulisho hadi pale itokee kinahitajika ndio wanaanza kuhangaika, watavipata tu tena kwa wakati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Halafu bado wanataka tuamini kua wanao uwezo.shida ni nini kwamba kama ku link tuuu na database ya nida hawawezi sasa nini wataweza. ?


Ndio maana hata ukipoteza/ibiwa simu uki report kwao hawawezi kuku saidia hadi uwe na imei number.
Cha ajabu kwenye requirement za ID wanataka tutumie national ID ambako tayari kuna fingerprints zetu. Why wasifanye integration ya hizo systems mbili. Why kuwe na duplicate fingerprints TCRA na NIDA?

Sent using Jamii Forums mobile app

USOGA WI KUA KATI MWINA NSONGOO
 
Nimeenda kusajiri line wakachukua saini yangu, wakapiga picha yangu passport size, copies za IDs zangu

Alafu naona sms kuwa niende tena kusajiri upya
Kiukweli SITAENDA wacha wafunge tu line

NIDA walichukua alama za vidole
NEC walichukua alama za vidole
bado TCRA nao tena?

Kwani alama za vidole huwa zina tabia ya kubadilika baada ya muda?

Hawawezi kuchua kutoka kwa wenzao NEC, NIDA?

Alama za vidole ni unique
kila mtu na zake dunia nzima!

sasa zimewachanganya?
Hapa kwa kweli kila mtu ana mwisho wa uvumilivu wake


Sent from my iPhone using JamiiForums
Watu wanaweza tumia kitambulisho chako cha NIDA kusajili line na hiyo laini akatumia mtu ambaye sio wewe. Sasa endapo wakitumia fingerprint za NIDA bila kukuchukua alama za vidole upya kama unavoshauri huoni kuwa utakuwa linked kwenye tukio la uhalifu ingawa wewe mwenyewe si muhusika bali kimetumika kitambulisho chako tu kusajilia laini ambayo imehusishwa na uhalifu?

Fingerprint lazima zichukuliwe ili kuhakikisha kuwa fingerprint zako zinakuwa linked directly na simkadi yako na picha yako bila ya shaka yoyote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoa mada una hoja nzuri sana ..... INTEGRATION ya hizi system automatically ingefaa zaidi kuliko sisi wananchi kupoteza muda mwingi kwenye foleni

Yaani kwa kuwa ID ya NIDA ina fingerprint zetu na zimehifadhiwa kwenye kanzidata(database) basi ni rahisi kuzihamishia kwenye mfumo wao hao TCRA... yaani akiingiza namba yangu ya kitambulisho mfano 19900101-5897569-123456 inaleta details zote na hizo alama za vidole, kwa hiyo ni kitendo cha kuzihamishia hizo taarifa kwenye profile mpya ya TCRA as SIMPLE as that..


SEMA SASA SIJUI WATANZANIA TUNAKWAMA WAPI?
Uchambuzi dhaifu mkuu. Kwa muktadha wa usalama, suala uliloeleza ni hatari sana, watu watabambikiziwa sana kesi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 1073902




Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema lengo la mfumo mpya wa usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole linatokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya wananchi waliosajili laini kwa kutumia vitambulisho feki.



Kuanzia Mei Mosi mwaka huu, wananchi wote wanatakiwa kusajili laini zao kwa mfumo huo, na laini ambazo hazitasajiliwa zitafungiwa pindi tutakapotangaza muda wa ukomo.



“Tunatambua kwa kutumia mfumo huu, itaondoa udanganyifu mkubwa unaosababisha kuwepo kwa ugumu wa TCRA katika kudhibiti vitendo vya uhalifu kwa kutumia mitandao,” amesema Mhandisi Mihayo.



Aidha Mihayo amesema katika mfumo huo wananchi watatakiwa kwenda na kitambulisho cha uraia au namba ya kitambulisho kwa ajili ya kusajili laini zao.



Hayo yamelezwa leo na Meneja wa Mamlaka hiyo Kanda ya Ziwa, Francis Mihayo, wakati wa kuzindua kampeni ya kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa mfumo huo mkoani wa Simiyu.
Naunga mkono hoja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm Kama n finger print walichukua kwa kutumia smartsimu zao,na laini inasema usajili umekamilika, wanataka finger print za nn Tena, au wanahakiki idadi ya vitambulisho?? Yaan kuangalia kuwa walivyotengeza na vilivyobaki n sahihi???
 
Mkuu hutaki kutambuliwa? Fingerprints ni kwa ajili ya kukutambua in relation to that Simcard. Bado fingerprints zinatumika nchini mwetu kumtambua mtu hata huko ulaya bado wanawatambua raia wao kwa njia ya fingerprints na DNA. Acha waanze kwanza kututambua kwa fingerprints. We need to start from somewhere mkuu!
Nyie ndio majitu mnaopata ZERO kwenye NECTA!! Maelezo yanasema vile, wewe unabwabwaja upupu! Umeambiwa fingerprints are nothing kwenye security, zaidi sana patatokea hasara ya mapato maana sio kila mtu atamudu hizo procedures!

Mungu okoa huyu ZEZETA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hutaki kutambuliwa? Fingerprints ni kwa ajili ya kukutambua in relation to that Simcard. Bado fingerprints zinatumika nchini mwetu kumtambua mtu hata huko ulaya bado wanawatambua raia wao kwa njia ya fingerprints na DNA. Acha waanze kwanza kututambua kwa fingerprints. We need to start from somewhere mkuu!

Wana namba za simu NIDA ambako wana picha mpaka finger print zako, wanajua wazazi wako shule ulizosoma na utambulisho wako wote, na walijitanabahi kuwa hivi vitambulisho vya NIDA ni digital haswa, sasa nini kinawashinda kulink hizo database mbili? ikiwa NIDA wanazo?
 
Under 18 yrs wote hakuna kumiliki sim card. Hili ni katazo lisilo rasmi toka TCRA.
Mobile services providers oyee!!!
Nahisi hili katazo linakinzana na Katiba - kuminya uhuru wa mawasiliano.
Lawyers mpo?
 
Wana namba za simu NIDA ambako wana picha mpaka finger print zako, wanajua wazazi wako shule ulizosoma na utambulisho wako wote, na walijitanabahi kuwa hivi vitambulisho vya NIDA ni digital haswa, sasa nini kinawashinda kulink hizo database mbili? ikiwa NIDA wanazo?
Kumbuka Kampuni za Simu ni private sector na NIDA ni Gov. Hivyo huwezi kuzilink system zao mkuu kuogopa usalama wa data.
 
Kumbuka Kampuni za Simu ni private sector na NIDA ni Gov. Hivyo huwezi kuzilink system zao mkuu kuogopa usalama wa data.

Serikali inauwezo wa kuomba data base hizo kisheria kabisa na ikapata. Wanafanya biashara Tanzania wameafiki kufuata sheria za Tanzania, ni uzembe tu.
 
Serikali inauwezo wa kuomba data base hizo kisheria kabisa na ikapata. Wanafanya biashara Tanzania wameafiki kufuata sheria za Tanzania, ni uzembe tu.
Mkuu hapo anayetaka data ni Kampuni za Simu kutoka NIDA ili aweze kulink na Database zao wala si NIDA
 
Kupata no ya kitambulisho toka NIDA garama ni 100tsh. Wakati kitambulisho unalipia sijajua kama kila mtu ana uwezo wa kulipia iyo 100
 
Cha ajabu kwenye requirement za ID wanataka tutumie national ID ambako tayari kuna fingerprints zetu. Why wasifanye integration ya hizo systems mbili. Why kuwe na duplicate fingerprints TCRA na NIDA?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona TRA kwenye leseni za kuendesha vyombo vya moto wanachukua finger print?
 
Mkuu hapo anayetaka data ni Kampuni za Simu kutoka NIDA ili aweze kulink na Database zao wala si NIDA

TCRA ndio wametangaza ambao ndio serikali na ndio NIDA au unaonaje wewe? au TCRA hawawezi kuomba database NIDA, taasisi mbili za serikali moja?
 
46 Reactions
Reply
Back
Top Bottom