TCRA na TRA, mchezo wa Vodacom mnada poa si sahihi kwa uchumi wa nchi

ruukada

Member
Feb 24, 2014
66
112
Kuna mnada umeanzishwa na Vodacom Tanzania kwa wateja wake ambapo ili kushiriki inabidi utoe kiasi cha Tshs. 500 kama kiingilio.

Kisha wanaweka dau la kupata rice cooker kwa kima cha chini lakini ukijumlisha hizo 500/- wanazotoa ni hela nyingi sana . Hii ni kama bahati nasibu lakini voda wanachorudisha kwa wananchi ni kidogo sana. Hii ni utapeli halafu TCRA mmekaa kimya.

Haiwezekani mtu akusanye Tshs. 500 kwa wateja wachache kabisa tuseme 200,000. Jumla wanapata zaidi ya Tshs. 100,000,000/ halafu wao wanampa mshindi kitu cha thamani ya kisichozidi 500,000/.

Sio sawa kabisa. Kinachochukuliwa kwa wananchi ni kingi sana. Hii inamaanisha hawa watu wanaondoa mzunguko wa hela kwenye jamii kwa kiasi cha Tshs. 100,000,000/ kila siku . Wao wanarudisha kiasi kisichozidi Tshs. 500,000/ kwenye jamii.

Please TCRA, TRA be serious about this. Nchi haiwezi kuachiwa kampuni kubwa zifanye chochote wanachotaka. Serikali mnabidi mlinde wananchi wenu dhidi ya mabepari kama hawa maana hiyo ndio hasa kazi yenu.
 
1. Wajinga ndio waliwao .....
2. Isije kuwa wanatekeleza maelekezo toka juu ili wachangie kununua PPE's.
 
Kuna mnada umeanzishwa na Vodacom Tanzania kwa wateja wake ambapo ili kushiriki inabidi utoe kiasi cha Tshs. 500 kama kiingilio.

Kisha wanaweka dau la kupata rice cooker kwa kima cha chini lakini ukijumlisha hizo 500/- wanazotoa ni hela nyingi sana . Hii ni kama bahati nasibu lakini voda wanachorudisha kwa wananchi ni kidogo sana. Hii ni utapeli halafu TCRA mmekaa kimya.

Haiwezekani mtu akusanye Tshs. 500 kwa wateja wachache kabisa tuseme 200,000. Jumla wanapata zaidi ya Tshs. 100,000,000/ halafu wao wanampa mshindi kitu cha thamani ya kisichozidi 500,000/.

Sio sawa kabisa. Kinachochukuliwa kwa wananchi ni kingi sana. Hii inamaanisha hawa watu wanaondoa mzunguko wa hela kwenye jamii kwa kiasi cha Tshs. 100,000,000/ kila siku . Wao wanarudisha kiasi kisichozidi Tshs. 500,000/ kwenye jamii.

Please TCRA, TRA be serious about this. Nchi haiwezi kuwachiwa kampuni kubwa zifanye chochote wanachotaka. Serikali mnabidi mlinde wananchi wenu dhidi ya mabepari kama hawa maana hiyo ndio hasa kazi yenu.
Sio lazima kila kinachokuja lazima ukipokee!
 
Inawezekana hata msindi asipatikane ,kwa mfano.
Washiriki watu wako na dau la pekee Yani hayafanani na dau la mtu yoyote.
A-505
B-707
C-901
Mshindianatakiwa 1 .hapokitu inarudi stoo

Kuwa makini piga kazi tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwenye namba ya NIDA anisaidie namba yake nisajili line ya Voda nilifukuzie hili rice cooker.
 
Mitandao ya simu kwa kushirikiana Tcra wanawaibia Sana wateja... Kwenye salio na hizo huduma za kitapeli...
 
Inawezekana hata msindi asipatikane ,kwa mfano.
Washiriki watu wako na dau la pekee Yani hayafanani na dau la mtu yoyote.
A-505
B-707
C-901
Mshindianatakiwa 1 .hapokitu inarudi stoo

Kuwabmakini piga kazi tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mshindi ni mwenye dau la chini kabisa 505. (As per the rules)

Ila huu mchezo voda wanapiga hela mno.
Wanainvest rice cooker wanaingiza mamilioni

I'll be back
 
Hivi wanapata kibali cha shirika la bahati nasibu au wanachonga dili tu na watu wa TCRA ili wapige pesa ya bwerere, maana rice cooker kwa shilingi milioni 100 siyo mchezo.
 
Ukiwauliza vigezo na masharti hawakupi vyote

Halafu mnada kama mnada, dau langu kama halijakidhi viwango inabidi nirudishiwe, lakini wao wanalichukua, wanapiga hela sana
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom