Kuna mnada umeanzishwa na Vodacom Tanzania kwa wateja wake ambapo ili kushiriki inabidi utoe kiasi cha Tshs. 500 kama kiingilio.
Kisha wanaweka dau la kupata rice cooker kwa kima cha chini lakini ukijumlisha hizo 500/- wanazotoa ni hela nyingi sana . Hii ni kama bahati nasibu lakini voda wanachorudisha kwa wananchi ni kidogo sana. Hii ni utapeli halafu TCRA mmekaa kimya.
Haiwezekani mtu akusanye Tshs. 500 kwa wateja wachache kabisa tuseme 200,000. Jumla wanapata zaidi ya Tshs. 100,000,000/ halafu wao wanampa mshindi kitu cha thamani ya kisichozidi 500,000/.
Sio sawa kabisa. Kinachochukuliwa kwa wananchi ni kingi sana. Hii inamaanisha hawa watu wanaondoa mzunguko wa hela kwenye jamii kwa kiasi cha Tshs. 100,000,000/ kila siku . Wao wanarudisha kiasi kisichozidi Tshs. 500,000/ kwenye jamii.
Please TCRA, TRA be serious about this. Nchi haiwezi kuachiwa kampuni kubwa zifanye chochote wanachotaka. Serikali mnabidi mlinde wananchi wenu dhidi ya mabepari kama hawa maana hiyo ndio hasa kazi yenu.
Kisha wanaweka dau la kupata rice cooker kwa kima cha chini lakini ukijumlisha hizo 500/- wanazotoa ni hela nyingi sana . Hii ni kama bahati nasibu lakini voda wanachorudisha kwa wananchi ni kidogo sana. Hii ni utapeli halafu TCRA mmekaa kimya.
Haiwezekani mtu akusanye Tshs. 500 kwa wateja wachache kabisa tuseme 200,000. Jumla wanapata zaidi ya Tshs. 100,000,000/ halafu wao wanampa mshindi kitu cha thamani ya kisichozidi 500,000/.
Sio sawa kabisa. Kinachochukuliwa kwa wananchi ni kingi sana. Hii inamaanisha hawa watu wanaondoa mzunguko wa hela kwenye jamii kwa kiasi cha Tshs. 100,000,000/ kila siku . Wao wanarudisha kiasi kisichozidi Tshs. 500,000/ kwenye jamii.
Please TCRA, TRA be serious about this. Nchi haiwezi kuachiwa kampuni kubwa zifanye chochote wanachotaka. Serikali mnabidi mlinde wananchi wenu dhidi ya mabepari kama hawa maana hiyo ndio hasa kazi yenu.