TCRA Mtandao wa Vodacom unamawasiliano mabovu, tunaomba muingilie kati.

analysti

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
729
612
Nimekuwa ni mteja na mtumiaji wa mtandao wa Vodacom (Data na Simu) kwa miaka mingi sasa.
Kwa kipindi cha kuanzia mwishoni mwa mwaka jana mpaka hivi sasa mawasiliano kupitia mtandao wa vodacom limekuwa ni suala la kubahatisha. Ni jambo la kawaida ukampigia mtu ukaambiwa hapatikani ilhali yupo hewani, unaweza ukawa unaongea na mtu ghafla unaanza kutomsikia au yeye kutokukusikia, mara sauti inakatika na kurudi. Ukija upande wa Data ndo kabisaa, nimeshindwa kutumia Data kupitia line ya vodacom ni zaidi ya miezi Mitano sasa, hakuna network kabisa.
Tunaomba mamlaka inayosimamia utoaji wa huduma za mawasiliano iangalie namna gani inaweza kuingilia kati na kuhakikisha huduma zinazotolewa zinakidhi matakwa ya mteja angalau kwa kiwango cha chini kabisa (Minimum standard).
 
Mitandao yote ni mibovu kupita kiasi

Yawezekana ni kweli, lakini kwa kipindi cha hivi karibuni Vodacom wamezidi. Nimeshindwa kuelewa ni kwamba wameelemewa na wateja au ni kitugani hakiendi vizuri. Maana imekuwa ni too much. Nimefanya utafiti kidogo, na nimegundua tatizo ni kubwa mnoo. Nina hakika wao wenyewe wanataarifa na wanapuuzia kwa sababu wanazozijua wao ilhali sisi watumiaji tunaumia.
 
Yawezekana ni kweli, lakini kwa kipindi cha hivi karibuni Vodacom wamezidi. Nimeshindwa kuelewa ni kwamba wameelemewa na wateja au ni kitugani hakiendi vizuri. Maana imekuwa ni too much. Nimefanya utafiti kidogo, na nimegundua tatizo ni kubwa mnoo. Nina hakika wao wenyewe wanataarifa na wanapuuzia kwa sababu wanazozijua wao ilhali sisi watumiaji tunaumia.
Mitambo mibovu mkuu
 
Nina line 3 za halotel zote za chuo(simu, modem na router) upo hapo? wote ni majanga.

kitu ambacho nimegundua ni aina ya matumiz ya bundle na aina ya cm anayotumia mtu fulan vnaeza vikafanya mwengine aseme mtandao fulan ni mbovu...ss apo kat yenu either yy matumiz yke ya net ni ya kusurf tu ndmn anaona net iko sawa au ww simu yako ndo kisababish cha kufanya uone network haiko sawa
 
kitu ambacho nimegundua ni aina ya matumiz ya bundle na aina ya cm anayotumia mtu fulan vnaeza vikafanya mwengine aseme mtandao fulan ni mbovu...ss apo kat yenu either yy matumiz yke ya net ni ya kusurf tu ndmn anaona net iko sawa au ww simu yako ndo kisababish cha kufanya uone network haiko sawa
Mimi mwenyewe nimeamua kuacha kutumia laini ya vodacom kwenye matumizi mengine isipokuwa mpesa tu.

Tatizo lilianza nikitumiwa sms baadhi hazifiki nikaenda voda shop wakaniambia nibadirishe simu nikafanya hivyo. Ikafuata kwenye kupigiwa, unaweza ukapigiwa akaambiwa anayekupigia haupatikani lakini kwangu sms inaingia kwamba nilitafutwa. Upande wa data mchana siwezi kutumia, usiku ni afadhali lakini siyo siku zote. Kwa sasa nimehamia kwingine kwa upande wa data na calls tu.
 
kitu ambacho nimegundua ni aina ya matumiz ya bundle na aina ya cm anayotumia mtu fulan vnaeza vikafanya mwengine aseme mtandao fulan ni mbovu...ss apo kat yenu either yy matumiz yke ya net ni ya kusurf tu ndmn anaona net iko sawa au ww simu yako ndo kisababish cha kufanya uone network haiko sawa
Sijakuelewa
 
Sometimes Ni Location Ambayo Upo Kama Upo Ushirombo Vijijini Usitegemee Access yako ya Internet itafanana na Mtu Aliyekuwepo Dar

Pia Aina ya Simu Unayotumia inaweza Ikawa Source Nayo I Think Unatumia TECNO WHEREVER
 
Du msema kweli mpenzi Wa mungu, Mimi nipo dar japo sio katikat ya mji lakn internate ya Voda ni tatizo kwa siku za karibun, nanunua bando hadi linaexpire simalizi, kwa data Voda wanatatizo kubwa sana
 
Sometimes Ni Location Ambayo Upo Kama Upo Ushirombo Vijijini Usitegemee Access yako ya Internet itafanana na Mtu Aliyekuwepo Dar

Pia Aina ya Simu Unayotumia inaweza Ikawa Source Nayo I Think Unatumia TECNO WHEREVER
Kama unategemea sana laini ya voda utajua mleta mada anachokizungumzia. Lakini kama una laini za mitandao mingine huwezi kuelewa. Kuna muda unaweza ukapigiwa simu msielewane mazungumzo hadi ukate upige upya.
 
kitu ambacho nimegundua ni aina ya matumiz ya bundle na aina ya cm anayotumia mtu fulan vnaeza vikafanya mwengine aseme mtandao fulan ni mbovu...ss apo kat yenu either yy matumiz yke ya net ni ya kusurf tu ndmn anaona net iko sawa au ww simu yako ndo kisababish cha kufanya uone network haiko sawa

Kimsingi tunacholalamikia mabadiliko ya ubora wa huduma. Binafsi nimekuwa nikitumia device hiyo hiyo na bundle hiyo hiyo ktk location hiyo hiyo. Kipindi cha nyuma internet ilikuwa ni nzuri na hakukuwa na shida ya mawasiliano kwa simu. Kwa kutumia device hiyo hiyo na kifurushi hicho hicho na eneo hilo hilo, hivi sasa hakuna kinachofanyika kabisa nikitumia vodacom. Hakuna mawasiliano ya simu hakuna data, hali ni mbaya mnooo. And it is very frustrating......
 
Kimsingi tunacholalamikia mabadiliko ya ubora wa huduma. Binafsi nimekuwa nikitumia device hiyo hiyo na bundle hiyo hiyo ktk location hiyo hiyo. Kipindi cha nyuma internet ilikuwa ni nzuri na hakukuwa na shida ya mawasiliano kwa simu. Kwa kutumia device hiyo hiyo na kifurushi hicho hicho na eneo hilo hilo, hivi sasa hakuna kinachofanyika kabisa nikitumia vodacom. Hakuna mawasiliano ya simu hakuna data, hali ni mbaya mnooo. And it is very frustrating......
Sasa si wanalazimika kulipa kodi
Kitendo ambacho zamani walikuwa wanalipa kiduchu na miprofit kibao
 
Back
Top Bottom