Johnny Sins
JF-Expert Member
- Nov 4, 2019
- 2,538
- 3,826
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa kushirikiana na watoa huduma, imetangaza kufanya uhakiki wa laini zote za simu zilizosajiliwa ili kuondoa wale waliosajili kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine.
Pia uhakiki huo utawahusu wale waliosajili laini zao kwa kutumia kitambulisho tofauti ambao wote watachukuliwa hatua za kisheria.
Kwa mujibu wa tangazo la mamlaka hiyo lililochapishwa na gazeti hili juzi, TCRA imeamua kufikia uamuzi huo ili kujiridhisha waliosajili laini zao za simu kwa kutumia kitambulisho sahihi.
Ofisa mwandamizi wa TCRA, alipoulizwa kuhusu lini uhakiki huo utaanza, alisema hawajasema wataanza lini, huku akiendelea kusisitiza uzimaji wa laini ambazo hazijasajiliwa linaendelea.
Katika tangazo hilo, TCRA ilisema kuwa kwa kushirikiana na watoa huduma itafanya uhakiki huo.
"Kusajili laini ya simu kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine ni kosa sanjari na kupewa laini iliyojasiliwa na mtu mwingine.”
Tangazo hilo limesema kuwa onyo na tahadhari zitaendelea kutolewa kwa makundi yote yanayohusika na usajili wa laini hizo.
“Kwa waliositishiwa huduma za laini zao za simu kuanzia Januari 20, wanaweza kuendelea na utaratibu wa usajili kwa lengo la ama kurudisha laini hizo zilizofungwa kama zitakuwa bado zipo au kupata mpya, mchakato huu ni endelevu,” sehemu ya tangazo hilo ilisema.
Pia tangazo hilo linasema watumiaji au waombaji wapya wa laini za simu wataendelea kusajiliwa muda wowote kwa kutumia kitambulisho cha Taifa na kuhakikiwa kwa alama za vidole.
Uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa ulikuwa ufanyike Desemba 31, mwaka jana, lakini Rais John Magufuli aliongeza siku 20 na mchakato huo ulikamilika Januari 20, mwaka huu.
Akitoa taarifa za uzimaji laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, alisema linafanyika kwa awamu ili kuondoa usumbufu na kwamba walikuwa wamezima laini 975,041.
Alisema kundi la kwanza waliozimiwa laini zao ni watu 656,091 ambao wana vitambulisho vya Taifa au Namba lakini hawajasajili laini zao.
Alisema kundi la pili la watu 318,950 waliosajili laini zao kwa kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa alama za vidole.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pia uhakiki huo utawahusu wale waliosajili laini zao kwa kutumia kitambulisho tofauti ambao wote watachukuliwa hatua za kisheria.
Kwa mujibu wa tangazo la mamlaka hiyo lililochapishwa na gazeti hili juzi, TCRA imeamua kufikia uamuzi huo ili kujiridhisha waliosajili laini zao za simu kwa kutumia kitambulisho sahihi.
Ofisa mwandamizi wa TCRA, alipoulizwa kuhusu lini uhakiki huo utaanza, alisema hawajasema wataanza lini, huku akiendelea kusisitiza uzimaji wa laini ambazo hazijasajiliwa linaendelea.
Katika tangazo hilo, TCRA ilisema kuwa kwa kushirikiana na watoa huduma itafanya uhakiki huo.
"Kusajili laini ya simu kwa kutumia kitambulisho cha mtu mwingine ni kosa sanjari na kupewa laini iliyojasiliwa na mtu mwingine.”
Tangazo hilo limesema kuwa onyo na tahadhari zitaendelea kutolewa kwa makundi yote yanayohusika na usajili wa laini hizo.
“Kwa waliositishiwa huduma za laini zao za simu kuanzia Januari 20, wanaweza kuendelea na utaratibu wa usajili kwa lengo la ama kurudisha laini hizo zilizofungwa kama zitakuwa bado zipo au kupata mpya, mchakato huu ni endelevu,” sehemu ya tangazo hilo ilisema.
Pia tangazo hilo linasema watumiaji au waombaji wapya wa laini za simu wataendelea kusajiliwa muda wowote kwa kutumia kitambulisho cha Taifa na kuhakikiwa kwa alama za vidole.
Uzimaji wa laini za simu ambazo hazijasajiliwa ulikuwa ufanyike Desemba 31, mwaka jana, lakini Rais John Magufuli aliongeza siku 20 na mchakato huo ulikamilika Januari 20, mwaka huu.
Akitoa taarifa za uzimaji laini za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, alisema linafanyika kwa awamu ili kuondoa usumbufu na kwamba walikuwa wamezima laini 975,041.
Alisema kundi la kwanza waliozimiwa laini zao ni watu 656,091 ambao wana vitambulisho vya Taifa au Namba lakini hawajasajili laini zao.
Alisema kundi la pili la watu 318,950 waliosajili laini zao kwa kitambulisho cha Taifa kabla ya kuanza mfumo wa kusajili kwa alama za vidole.
Sent using Jamii Forums mobile app