TCRA kudhibiti utoaji huduma za vifurushi kwa kampuni za simu

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Katika kukabiliana na malalamiko juu ya huduma ya vifurushi zinazotolewa na kampuni mbalimbali za simu nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetengeneza kanuni ndogo zitakazoratibu utoaji wa huduma hizo.

Kuandaliwa kwa kanuni hizo kumekuja kufuatia maoni 3278 yaliyotolewa na wananchi kuhusu vifurushi hivyo.

Akizungumza leo Jumanne Machi 2, 2021 mkurugenzi mkuu wa TCRA, James Kilaba amesema utekelezaji wa kanuni hizo utaanza Aprili 2, 2021.

Miongoni mwa yaliyoelekezwa kwenye kanuni hizo ni huduma zote za vifurushi lazima zipate vibali vya TCRA huku mamlaka hiyo pia ikitoa mwongozo wa bei zilizowekwa na mamlaka hiyo.

Nyingine ni vifurushi vyote havitaondolewa au kurekebishwa ndani ya miezi mitatu baada ya kuidhinishwa.

Pia, mtoa huduma atatakiwa kutoa taarifa kila wakati matumizi ya kifurushi yatakapofikia asilimia 75 kabla ya kuisha na kitakapomalizika kabisa kwa asilimia 100.

1.jpg
2.jpg
3.jpg
4.jpg
5.jpg
 
Waache unafki inamaana wao hawaoni rises of price ya mabando mpaka wasubirie malalamiko kutoka kwa wananchi?

Kazi ya TCRA ni nini sasa kama wanashindwa kukagua mienendo ya kampuni ambazo ziko chini yake?

Kwa maana hiyo walalamikaji wangekausha TCRA isingeweza kusanuka mchezo mchafu unaofanywa na hizi kampuni za mawasiliano?

Pili hii habari sioni kama itakuwa na msaada wowote, kama waziri wa mawasiliano alitoa ilani na kuzikemea hizo kampuni baada ya malalamiko kutoka kwa wananchi na bado hakuna hatua yeyote iliyochukuliwa kutokomeza huo unyonyaji. Nini kinachofanya tuamini tamko hili la TCRA litazaa matunda?
 
Nilicho kuja kugundua ni kwamba hii mitandao ina milikiwa na vigogo wa serikalini ambao wameficha identity zao wasijulikane na wananchi ila viongozi wakubwa kwenye system wanajua mchezo wote

Na ndio maana inakua ni ngumu kuwa dhibiti kwasababu ya kulindana, leo ukimuaribia mwenzako kesho utakuja utawala ambao ambao ni partnership na uliyemuaribia hivyo kupitia madaraka anaweza kukuharibia na wewe kama kisasi

Sasa ili wao waepuka hayo ilibidi mwananchi aumie, na tunaumia kweli imagine dangote alipokuwa analeta cement yake aliweka bei mfuko mmoja uuzwe 7000 lakini kwakua kuna vigogo wana biashara kama hiyo na wao bei zao ni 15,000/= ilibidi serikali imlazimishe auze bei ambayo inafanana na makampuni ya ndani
 
Hivi hawa jamaa wanakusanya Kodi kiasi gani kwenye hivyo vifurushi ? Huenda they are part of the problem...
 
Back
Top Bottom