chuma cha mjerumani
JF-Expert Member
- Dec 4, 2013
- 11,118
- 22,504
Jielimishe.
TCRA haisimamii Magazeti wala Majarida. Magazeti na Majarida yanasimamiwa na Idara ya Habari Maelezo ambayo ipo chini ya Wizara ya Habari. Idara hii ndiko hayo magazeti yanapata usajili na kusimamiwa. Hata wewe kama unahitaji kuanzisha gazeti utaenda huko.
TCRA inasimamia vyombo vya Utangazaji, Simu,Posta,na Mawasiliano yote ya Kielektroniki zikiwemo redio call,mawasiliano ya ndege, kuthibitisha vyombo vipya vya mawasiliano, mambo ya vipeto kv DHL, mambo ya mkongo nk nk wakiwemo online media, coded number kv *150*01# nk nk...
Kwa hiyo malalamiko yako haya yawasilishe Idara ya Habari Maelezo.
Ni muhimu tujenge utamaduni wa kujifunza juu ya vitu vyetu ndugu watanzania ili tuelewe mifumo yetu kiukamilifu.
Wasalaam!.
N'yadikwa
Technology imebadilika hiki sio kipindi Cha nyerere. Vyombo vyote vya habari vipo online/pia Facebook/Twitter/Instagram
Unavyosema havipo chini ya tcra unanishangaza. Na habari zao huwa wanazitoa online vile vile.
Ukiona vichwa vya habari vinatrend mitandaoni jua ni wao wanavitoa.
KUBALI TUU KUNA DOUBLE STANDARD.