Tchc card hazitusaidii chochote na hatupati huduma

Jethro

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
2,219
370
Wana JF,

Nimekuja kugundua kuwa sie watanzania twajaribu kwenda na wakati lakini matokeo yake hukwamia njiani na huo ustaarabu unatushinda kabisa kwani kuna mahali kuna kundi la watu wajanja wanafanya biashara zao kwa kupitia migongo ya watu kwanini nasema hivyo,

Tunapo kwenda tibiwa kwenye hizi hospitali zetu wengine hutumia NSSF CARD,TCHC CARD, na zinginezo ila TCHC CARD kwakweli hazitusaiidii kabisa, Majuzi dada yangu alikwenda tibiwa na yeye ni mja mzito na huwa wanavipimo vingi sasa katika kupimwa akaambiwa wanataka kujua kipimo cha Hormones na kian cost 50,000/=Tshs lakini wahudu wa ile Hospital waka ikataaa ile card na wakasema TCHC ni wasumbufu sana ikabidi alipe Cash na ukiwatafuta hawa TCHC wana namba lukuki kwa kifupi kupatikana kwao ni kwa nadra namba zote zilizopo kwa Card TCHC ukipiga duuu utasubili sana,

Na cha ajabu kingine hizi card ati huwa zina mashariti kiwango fulani cha pesa ndio hizo hospitali hukubali na kikizidi hutibiwi basi wawe wazi watuambia mwisho ni kiasi gani kama ni laki 1,2,3,4,5 tujuae maana huko kwa hospital huwa twakimbizana na ma accountants.

Je wenzangu wana JF hamjawahi kukutana na haya mambo toeni nanyi maoni yenu karibuni.
 
Back
Top Bottom