Uchaguzi 2020 TCAA yawajibu CHADEMA! Yasema CHADEMA waliomba kibali cha kuruka kwenda Dar leo saa tatu asubuhi

Leak

JF-Expert Member
Feb 22, 2012
52,206
42,067
Wasalaam wana jamvi!

Baada ya mgombea wa CHADEMA kuwatuhumu mamlaka ya anga kumchelewesha kwenda Dar kwa kutumia helkopta ...leo mamlaka ya anga wamemjibu na kushangazwa na upotoshaji wao!

Mamalaka ya anga wameweka wazi kuwa helkopta ya Lissu haikuwa na Ratiba ya kwenda dar ikitokea Kilimanjaro bali ilikuwa na Ratiba ya kutoka Killimanjaro kurudi Nairobi

Mamlaka wanasema State Aviation walipeleka maombi ya mabadiliko ya ratiba hiyo saa tatu asubuhi wakisema watakwenda Dar -Tanganyika Packers.

Mamlaka ya anga wanasema hata hivyo maombi ya kibali hicho yalikuwa na mapungufu kwani kwamujibu wa sheria za anga unapoomba kibali unatakiwa kuonesha unakwenda wapi na baada ya hapo utakwenda wapi..hivyo wamiliki wa helkopta waliambiwa wakaeekebishe maombi na kuondoa mapungufu ili wapewe kibali!

Hata hivyo chadema na wamiliki walirekebisha maombi yao na kupewa ruhusa ya kwenda Dar Tanganyika Packers!

Hivyo si kweli walinyimwa kibali bali walijichelewesha wenyewe wakati wanaujua utaratibu!​

IMG_0813.jpg
 
Wambieni hao TCAA ni wapuuzi tu kama walivyo Lumumba walojaza matope ,ujinga, upumbavu ..

T.Lissu na team yake sio wajinga, eti kurekebisha Kibali iwachukue masaa manne .

Ukweli ni kuwa Mwamba Tundu Antipas Lissu aliamua mwenyewe kwa makusudi kabisa, kumuamuru Rubani wa Chopa yake kuondoa mzigo kama ambavyo aliamua kutumia Mtumbwi kuvuka ziwa.

HUYO NDIO LISSU.
 
ASANTE SANA KWA HILI, NILIKUWA NAAMINI KIBALI ANACHO ILA ALITAKA KUTENGENEZA CHUKI TUU. SIO RAHISI AU HAIWEZEKANI KURUSHA NDEGE BILA APPROVAL YA FLIGHT PLAN, NA NILIUZA MASWALI MENGI SANA .

Na hata nikamalizia kuwa baada ya helicopter kufika Kawe bila ruhusa hio ndege ataenda kuipaki nyumbani kwake? Watu wa Insurance watamwacha? na ataendeshaji bila kuwa na contact na control tower ya karibu na anako kwenda?

Na mwenye ndege anaruhusu kwani amepandwa na ujinga gani au aliokota pesa ya kununua hiyo helicopter? Na kuna uwezekano jeshi letu la anga likaichukulia ni ndege ya adui kwa kuwa haina utambulisho angani wa mamlaka husika.
 
Hakuna Rubani yeyote mwenye leseni na mwenye akili timamu atakayekubali kuruka bila idhini ya Mamlaka ya Anga! Kufanya hivyo maana yake ameamua kuondoka kwenye huduma ya kurusha ndege Kitaifa na Kimataifa!!
Kwani yule rubani Mtanzania aliyeiba ndege ya Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977 Jumuiya ilipovunjika aliirusha ndege kwa ruhusa ipi?
 
ASANTE SANA KWA HILI, NILIKUWA NAAMINI KIBALI ANACHO ILA ALITAKA KUTENGENEZA CHUKI TUU. SIO RAHISI AU HAIWEZEKANI KURUSHA NDEGE BILA APPROVAL YA FLIGHT PLAN, NA NILIUZA MASWALI MENGI SANA .

Na hata nikamalizia kuwa baada ya helicopter kufika Kawe bila ruhusa hio ndege ataenda kuipaki nyumbani kwake? Watu wa Insurance watamwacha? na ataendeshaji bila kuwa na contact na control tower ya karibu na anako kwenda?Na mwenye ndege anaruhusu kwani amepandwa na ujinga gani au aliokota pesa ya kununua hiyo helicopter? Na kuna uwezekano jeshi letu la anga likaichukulia ni ndege ya adui kwa kuwa haina utambulisho angani wa mamlaka husika.

Lissu asingewavimbia TCAA wangetoa kibali cha kuruka keshokutwa.
 
Back
Top Bottom