TBS na Wafanyabiashara Hawawatendei Haki Watanzania

Sioni mantiki ya malalamiko ya waswahili kwa sababu sisi Tunapenda bidhaa za bei rahisi pengine ni kulingana na uwezo wetu.
Nchi ambayo bado mitumba hata ya taulo, vyupi nk ni dili ni nchi masikini na yenye Watu wasiojitambua. Kuwauzia bidhaa feki haiepukiki
Ni lini ulinunua tishet 60000?au kadet 75000?bidhaa original zipo ila hatuzimudu bei na mfanyibiashara anaangalia walaji wanataka nini kulingana na uwezo wao.
Siyo kweli.

Leo hii ukitaka vifaa vya umeme vya kutoka Japan, UK, Germany, Brazil, US, siyo rahisi kuvipata. Zimejaa takataka za China.

Kwangu mimi na wengi wenye kujitambua, ni aheri ninunue kitu kwa laki 2 kinachodumu miaka mitano kuliko ununue kitu toka China kwa sh laki 1, halafu kikadumu miezi 6.

Bidhaa za China, katika uhalisia ni aghali sana. Maana unaweza kununua kiatu sh 90,000 ukavaa miezi miwili tu, kimeachia sole, wakati Italy original 200,000 unakaa nacho miaka 6. Ioi ni aghali katika viatu hivyo viwili?
 
Kwenye vipodozi ndio kabisa. Madukani vipo vipodozi feki na hatarishi kabisa kwa afya ya binadamu.
Hakuna kilicho bora cha mchina. Kuna rafiki yangu alinunua malorry 3 aina ya FAW, yote mapya, yote yaliletwa siku moja. Wiki ya kwanza, moja likaleta tatizo. Walifungua, kuangalia, ikaonekana part moja ilitengenezwa vibaya, wakaamua kubadilisha hiyo part. Rafiki yangu akawaambia mafundi kuwa wafungue yale mawili yaliyobakia. Walichoshudia hawakuamini. Gari aina moja, model moja, kuna part nyingine, lorry moja lilikuwa na baadhi ya parts tofauti kabisa na yale mawili.

Wanaonunua magari ya China, wanakuambia kuwa average life span ya magari ya mchina, practically ni miaka 3. Baada ya hapo, kila siku ni matengenezo. Ya mjapan ni miaka 10.
 
China kila bidhaa zipo.nzuri na mbaya ni wewe tu chaguo lako.
tbs wakikaza wafanyabiashara wengi watalia
Ili kuwalinda walaji, lazima TBS isimamie viwango. Kuruhusu mtu anunue takataka, akijua amenunua bidhaa iliyo bora, ni kumwumiza mlaji.
 
Upande wa nguo ndio shida

Nguo unanunua leo ukifua TU tayari ishafubaa wale wazee wa kadeti nadhan tunaelewana hapa

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Nimejikuta nawaza tu. Kwa nini Tanzania kwa shehena ya pamba inayovunwa tusiwe na viwanda vya kadet, tishet, blauzi, mashati, chupi, suti, mashuka, jezi, pedi, pamba za hospitali, makanzu, vest, vitambaa. Tuuze nguo soko la ndani na afrika mashariki na kati na afrika nzima.

Hata kwenye viatu ni hivyohivyo

Tunakwama wapi, je gharama ni kiasi gani?
 
Nimejikuta nawaza tu. Kwa nini Tanzania kwa shehena ya pamba inayovunwa tusiwe na viwanda vya kadet, tishet, blauzi, mashati, chupi, suti, mashuka, jezi, pedi, pamba za hospitali, makanzu, vest, vitambaa. Tuuze nguo soko la ndani na afrika mashariki na kati na afrika nzima.

Hata kwenye viatu ni hivyohivyo

Tunakwama wapi, je gharama ni kiasi gani?
Wanao agiza vitu toka nje wanajua
 
Hakuna kilicho bora cha mchina. Kuna rafiki yangu alinunua malorry 3 aina ya FAW, yote mapya, yote yaliletwa siku moja. Wiki ya kwanza, moja likaleta tatizo. Walifungua, kuangalia, ikaonekana part moja ilitengenezwa vibaya, wakaamua kubadilisha hiyo part. Rafiki yangu akawaambia mafundi kuwa wafungue yale mawili yaliyobakia. Walichoshudia hawakuamini. Gari aina moja, model moja, kuna part nyingine, lorry moja lilikuwa na baadhi ya parts tofauti kabisa na yale mawili.

Wanaonunua magari ya China, wanakuambia kuwa average life span ya magari ya mchina, practically ni miaka 3. Baada ya hapo, kila siku ni matengenezo. Ya mjapan ni miaka 10.
Gari lolote la mchina matumizi yake ni miezi 18 tu kwa kuwa kwa kipindi hicho gari huwa na muonekano wa kuvutia na linatumia mafuta kidogo mno. Ila Muda ukifika au kukaribia inabidi uuze fastafasta. Ndio maana wanaonunua mabasi/malori ya mchina huwa wanayauza fastafasta kisha wananunua mengine fastafasta.
 
Mara kadhaa, watu mbalimbali wamekuwa wakihoji uwezo wa TBS katika kuhakikisha ubora wa viwango vya bidhaa wanazopewa Watanzania.

Kuhusu TBS, mara kadhaa, tumeuliza:

1) Je, haina utalaam?
2) Haina maadili?
3) Au haina vifaa?

Leo, kila mahali, zimezagaa bidhaa duni kabisa kutoka China. Bidhaa za China zisizo na ubora, ni balaa kubwa kwa uchumi wa Afrika.

Kwa upande mwingine, wanaouhujumu uchumi wa Tanzania, na Afrika kwa ujumla ni wafanyabiashara. China, bidhaa zenye ubora ni zile zinazotengenezwa na makampuni ya Ulaya na America, yaliyowekeza nchini China, ambazo soko lake kubwa huwa ni huko huko Ulaya na America. Makampuni mengi ya China, yanayomilikiwa na Wachina, ndiyo yanayotengeneza bidaa duni za kuiga, ambazo soko lake ni Afrika. Bidhaa hizi ni janga kwa uchumi na ustawi wa Afrika, ni bidhaa zinazoua uchumi wa Afrika.

Wafanyabiashara wa Tanzania, ndio wanaoenda kununua bidhaa kwenye makampuni hayo ya wachina yanayotengeneza bidhaa duni, na kuzileta Tanzania. Bidhaa hizi ni za viwango duni sana, na zinaua uchumi wa Tanzania na Afrika, huku zikiitajirisha China. Huu ni wizi wa wazi unaofanywa na Serikali ya China kwa Waafrika. Huu ni wizi wa kidola. Kwa nini nchi ya China iruhusu makampuni yanayotengeneza bidhaa fake? Kwa nini iruhusu bidhaa hizi duni kusafirisgwa kuja Afrika? Ina maana Serikali ya China imeruhusu uharamia huu dhidi ya Afrika?

Jambo la kusikitisha, siku hizi, karibia maduka yote yamejaa hizi bidhaa duni toka China. Kwenye baadhi ya miji, unazunguka maduka yote, hakuna duka hata moja ambalo lina bidhaa kutoka mataifa mengine.

Ushauri kwa wafanyabiashara, baadhi yenu agizeni bidhaa toka mataifa kama Japan, Singapore, Hong Kong, Malaysia, UK, Germany, US, au bidhaa zilizotengenezwa nchini China kwenye makampuni ya kutoka Ulaya na America, hakika mtapata wateja wengi, waliochoshwa na hizi bidhaa duni za makampuni ya Kichina.

Serikali iamke, idhibiti ubora wa bidhaa toka China. Serikali iangalie uwezo wa TBS kiutaalam na kiutendaji. Kwa utendaji wake wa sasa taasisi hii ya TBS haina maana yoyote kwa Watanzania.
Hata Marekani yenyewe imejaa bidhaa za China, sasa sijajua hasira zako zinatokea wapi
 
Tatizo sio wafanyabiashara au TBS

Tatizo lililopo Ni purchasing power ndogo ya watanzania na waafrika Wana vipato vidogo ndio maana soko la bidhaa zinazolishwa Ulaya na Marekani haziuziki soko Kama Tanzania zitakudodea dukani

Bila interference ya mchina watanzania wengi wangetembea uchi peku peku bila viatu na wangepikia vyungu

Mchina kahakikisha kila mtanzanzia anatembea kapendeza .Ukiwa na shilingi elfu 20 tu waweza pata nguo Hadi viatu vya kutokea vipya vya kichina

Suala vinadumu muda gani Hilo swala lingine. kiatu umenunua kwa shilingi elfu Saba unataka kidumu muda gani kiatu Cha Bei hiyo?

Sawa kiatu kitakatika nk lakini solution ipo Kuna mafundi viatu wa kushona kibao kwa shilingi Mia tano tu anakishona unaendelea nacho

Wazungu na wamarekani Kama soko wangeona lipo wangeshatua zamani nchini na maduka ya vitu vyao

Tanzania na Africa kwa uwezo tulionao twaweza mudu kununua tu bidhaa za China na mitumba kuanzia magari Hadi nguo ndio maana wauza magari mitumba Ni wengi sio wa magari mapya ukileta magari mapya yatakudodea dukani
 
Tatizo sio wafanyabiashara au TBS

Tatizo lililopo Ni purchasing power ndogo ya watanzania na waafrika Wana vipato vidogo ndio maana soko la bidhaa zinazolishwa Ulaya na Marekani haziuziki soko Kama Tanzania zitakudodea dukani

Bila interference ya mchina watanzania wengi wangetembea uchi peku peku bila viatu na wangepikia vyungu

Mchina kahakikisha kila mtanzanzia anatembea kapendeza .Ukiwa na shilingi elfu 20 tu waweza pata nguo Hadi viatu vya kutokea vipya vya kichina

Suala vinadumu muda gani Hilo swala lingine. kiatu umenunua kwa shilingi elfu Saba unataka kidumu muda gani kiatu Cha Bei hiyo?

Sawa kiatu kitakatika nk lakini solution ipo Kuna mafundi viatu wa kushona kibao kwa shilingi Mia tano tu anakishona unaendelea nacho

Wazungu na wamarekani Kama soko wangeona lipo wangeshatua zamani nchini na maduka ya vitu vyao

Tanzania na Africa kwa uwezo tulionao twaweza mudu kununua tu bidhaa za China na mitumba kuanzia magari Hadi nguo ndio maana wauza magari mitumba Ni wengi sio wa magari mapya ukileta magari mapya yatakudodea dukani
Upo sahihi kabisa. Mfano halisi ni kuhusu jezi za mpira. Sisi tunanunua kwa 20000-30000 Material ni lowgrade sythetic polyester. Ila jezi quality kabisa bei ni kuanzia laki Mbili mpaka laki sita bei ya UK.

Sasa bongo nani atanunua jezi ya laki mbili au laki sita?😂
 
Kwa ufahamu wangu, hizi bidhaa ambazo ni duni kutoka China ni maalumu kwa watu wa kipato cha chini ambao hawataweza kumudu bei ghali za bidhaa ambazo ni bora.

China kwenye maduka ya rejareja hawakufichi kuhusu ubora wa bidhaa ambazo wanauza.

Mchina anakupangia bidhaa mbili zinafanana na anakwambia ubora wake na bei zake.

Wafanya biashara wetu wanaenda kunua hizi bidhaa lakini bado wanakuja kutuuzia kwa bei ya juu tofauti na ubora wake.- nadhani hapa ndipo penye kosa lenyewe.

Ki msingi mimi bado sijaona ubaya wa mchina kwani yeye anafanya biashara, na anataka afanye biashara na watu wa madaraja yote.

Malaka zetu ndizo zenye tatizo katika kudhibiti haya yote.
 
Tatizo sio wafanyabiashara au TBS

Tatizo lililopo Ni purchasing power ndogo ya watanzania na waafrika Wana vipato vidogo ndio maana soko la bidhaa zinazolishwa Ulaya na Marekani haziuziki soko Kama Tanzania zitakudodea dukani

Bila interference ya mchina watanzania wengi wangetembea uchi peku peku bila viatu na wangepikia vyungu

Mchina kahakikisha kila mtanzanzia anatembea kapendeza .Ukiwa na shilingi elfu 20 tu waweza pata nguo Hadi viatu vya kutokea vipya vya kichina

Suala vinadumu muda gani Hilo swala lingine. kiatu umenunua kwa shilingi elfu Saba unataka kidumu muda gani kiatu Cha Bei hiyo?

Sawa kiatu kitakatika nk lakini solution ipo Kuna mafundi viatu wa kushona kibao kwa shilingi Mia tano tu anakishona unaendelea nacho

Wazungu na wamarekani Kama soko wangeona lipo wangeshatua zamani nchini na maduka ya vitu vyao

Tanzania na Africa kwa uwezo tulionao twaweza mudu kununua tu bidhaa za China na mitumba kuanzia magari Hadi nguo ndio maana wauza magari mitumba Ni wengi sio wa magari mapya ukileta magari mapya yatakudodea dukani
waTZ wanaoenda kuigiza sana,hivi mtu mshahara wa laki5-million,unaweza kumudu kununua suruali ya 70000 na BADO vitu vingine na familia kiujumla,Sisi tukubali mchina anatuweka na sisi ktk ulimwengu wa kisiasa tu Japo ni low quality,Hivi kama si Tecno,Itel na simu nyingi za kichina mpaka leo tungeendelea kwenda internet cafe kulipa jero jero,na Hata TV tungezisikia kwenye bomba huku tukiendelea kujipachinga mitumba mwili mzima tena ile sagurasagura.


Cha muhimu tu tukuzeni viwanda vidogovidogo vya ndani na kuwaezesha Zaid Sido,ikiwezekana tuamishe technology ya china na viwanda VYAO kufanyia shughuli zao hapahapa.

Pia kodi za serikali na soko la uhakika liwepo nchini,hopefully tutapunguza maronya walau kudumu hata 3years tu
 
Mlimani maduka ya nguo za quality kama Gsm watu wanakimbia wanaenda kkoo ,Sasa utegemee mwenye Duka aendelee kia mzembe,Hata azam naye na visimbuzi kageukia china
 
Back
Top Bottom