mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 802
- 725
Serikali ya Tanzania imependekeza marekebisho ya sheria ya viwango sura 130 ili kuhamisha majukumu ya kusimamia masuala ya chakula na vipodozi kwa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ambayo inasimamia majukumu hayo kwa sasa.
Kutokana na kubadilishwa kwa majukumu hayo, imependekezwa kuwa badala ya kuitwa TFDA, iitwe Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).
Kufuatia pendekezo hili, TBS itachukua jukumu la kuunganisha utaratibu wa usajili wa majengo, bidhaa, udhibiti wa bidhaa na udhibiti wa bidhaa kutoka nje.
Hayo yameelezwa leo Jumatano Juni 26, 2019 na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji wakati akiwasilisha bungeni muswada wa sheria ya fedha mwaka 2019.
“Inapendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura ya 219 ili kuiondolea TFDA jukumu la kusimamia chakula na vipodozi.”
Kutokana na kubadilishwa kwa majukumu hayo, imependekezwa kuwa badala ya kuitwa TFDA, iitwe Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA).
Kufuatia pendekezo hili, TBS itachukua jukumu la kuunganisha utaratibu wa usajili wa majengo, bidhaa, udhibiti wa bidhaa na udhibiti wa bidhaa kutoka nje.
Hayo yameelezwa leo Jumatano Juni 26, 2019 na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Ashatu Kijaji wakati akiwasilisha bungeni muswada wa sheria ya fedha mwaka 2019.
“Inapendekeza kufanya marekebisho ya Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi sura ya 219 ili kuiondolea TFDA jukumu la kusimamia chakula na vipodozi.”