Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,941
- 9,947
Jana saa mbili usiku nilikuwa nikiangalia taarifa ya habari ya TBC1 na habari kuu jana ilikuwa ni kutua kwa mahelkopita huko Igunga kwa ajili ya kutumika katika mikutano ya kampeni. TBC1 walionyesha helkopita ya CCM ikitua na Makamba akapokelewa na Mwigulu na watu wengine. Kisha ikaonyeshwa kwa UFUPI SANA Mwigulu akihutubia na kisha makamba akasikika akisema maneno mawili matatu tu basi. Pia TBC1 haikuonyesha UMATI wa watu ambao hao viongozi wa CCM walikuwa wakihutubia!! Kwa kifupi coverage kwa CCM ilikuwa kidogo sana.
Kisha nikashuhudia coverage ya CHADEMA. Walianza kuonyesha helkopita ikiwa angani na maneno CHADEMA yakionekana, kisha wakaionyesha helkopita ikiwa eneo fulani ambalo naamini ni kituo cha mafuta ikiwa inakunywa mafuta. Baada ya hapo helkopita ya CHADEMA ikaonyeshwa ikitua huko Nkinga na Mwenyekiti wao akashuka na kuhutubia. Kinyume na walivyo cover hotuba ya CCM, hapa Mbowe alipewa muda mreeefu akihutubia kuhusu mambo ya siasa na dini na wakati huohuo TBC1 ikionyesha umati wa watu ambao Mbowe alikuwa akihutubia. Baada ya hotuba TBC1 walionyesha helkpita ya CHADEMA ikituka kuondoka eneo la mkutano.
Kwangu mimi naona TBC1 hawakuitendea haki CCM kwa kuipa coverage kidogo sana hasa juu ya helkopita ambayo imegeuka kuwa ni kete ya kisiasa huko Igunga. Pia TBC1 hawakumuonyesha mpambanaji Magufuli wakati akiunguruma huko Igunga.
Kisha nikashuhudia coverage ya CHADEMA. Walianza kuonyesha helkopita ikiwa angani na maneno CHADEMA yakionekana, kisha wakaionyesha helkopita ikiwa eneo fulani ambalo naamini ni kituo cha mafuta ikiwa inakunywa mafuta. Baada ya hapo helkopita ya CHADEMA ikaonyeshwa ikitua huko Nkinga na Mwenyekiti wao akashuka na kuhutubia. Kinyume na walivyo cover hotuba ya CCM, hapa Mbowe alipewa muda mreeefu akihutubia kuhusu mambo ya siasa na dini na wakati huohuo TBC1 ikionyesha umati wa watu ambao Mbowe alikuwa akihutubia. Baada ya hotuba TBC1 walionyesha helkpita ya CHADEMA ikituka kuondoka eneo la mkutano.
Kwangu mimi naona TBC1 hawakuitendea haki CCM kwa kuipa coverage kidogo sana hasa juu ya helkopita ambayo imegeuka kuwa ni kete ya kisiasa huko Igunga. Pia TBC1 hawakumuonyesha mpambanaji Magufuli wakati akiunguruma huko Igunga.