TBC - Ushauri wa bure

Mlima meru

Senior Member
Dec 30, 2012
114
20
Mimi nimekuwa nikifuatilia vipindi mbalimbali vya kuelimisha pamoja na vile vinavyo ruhusu watazamaji kuchangia kwa kuoiga simu
Kero yangu ni kuwa;
kUtumia simu moja kupokea wakati una watazamaji zaidi ya laki mbili nahisi sio sawa kwani hata ukiweka namba kumi as long as zinapokelewa na simu moja ambayo haina hata uwezo wa kuhold simu tatu kwa pamoja nahisi ni kubaki nyuma ki technologia.
Ushauri
1. Kwa technologia ya sasa, ingetangiwa pamoja na simu..muwe na namna nyingine ya kupokea maoni mfano kwa mtandao eg. face book, twiter au hata whatuspp na hata kwa message kwenye simu.
Mbona naona habari za biashara na uchumi mnatumia Ipad, ambayo mnayo tayari; kwa nini msiitumie kwa kazi zaidi ya hizo??
2. Kwa nini msiwe na utaratibu wa katangaza kuwa kipindi kijacho au kipindi cha siku flani tutakuwa na watu wa TRA hivyo tunaomba mtutumie maswali ambayo mngependa kufaham kwa? namba ya message na hata email.


Faida zake:
watu wa pembezoni ambao technologia ya mtandao haijafika wangekuwa wakipata simu kwa urahisi kwa kuwa watu wa mijini wangetumia zaidi hizo njia mbadala.
mngeweza kupata mawazo mengi mazuri ya kuwauliza mlio waalika kwenye jopo.

Nawakilisha
 
Back
Top Bottom