TBC n ITV hawana tofauti....!!!???

Dr. Chapa Kiuno

JF-Expert Member
Sep 11, 2009
443
18
Wadau, hivyi kweli mnaielewa TBC esp ratiba zao za kuonesha mechi kila jumamosi? Maana kila inapofikia mechi ya Man U basi siku hiyo hawataonesha LIKE WISE kwa wenzao ITV n Radio 1 wamegoma kabisa kuonesha mechi za Simba au hata kutoa habari zozote za Simba... Hii ni sahihi kweli?


Maoni jamani n wala tusijenge chuki.
 
Hawa ITV wana matatizo sana, wakikorofishana kidogo tu na viongozi wa timu basi wanasusa kutangaza habari za timu husika. hii si mara ya kwanza kwa ITV/Radio One kususa habari za simba.
 
kwa tbc hawa hawana ratiba na hawajali mda.hata taarifa ya habari inaanza saa mbili na dk 5.
imekuwa ya kibiashara zaid. kwenye mpira hawana ratiba,

kwa itv hawa ndoi maboga kweli, hata habari zao za michezo huwa za makombe ya kuku. ni bora kipengere cha michezo wangefuta kabisa
 
kwa tbc hawa hawana ratiba na hawajali mda.hata taarifa ya habari inaanza saa mbili na dk 5.
imekuwa ya kibiashara zaid. kwenye mpira hawana ratiba,

kwa itv hawa ndoi maboga kweli, hata habari zao za michezo huwa za makombe ya kuku. ni bora kipengere cha michezo wangefuta kabisa
Mkuu, uko sahihi kabisa... TBC wako kibiashara n ITV wako after BOSI anataka nini... Ndy maana huwa anaweza akaongea hata dk 10 ndani ya habari bila kukatishwa... C wakubali tu Simba anatisha season hii?
 
kwa tbc hawa hawana ratiba na hawajali mda.hata taarifa ya habari inaanza saa mbili na dk 5.
imekuwa ya kibiashara zaid. kwenye mpira hawana ratiba,

kwa itv hawa ndoi maboga kweli, hata habari zao za michezo huwa za makombe ya kuku. ni bora kipengere cha michezo wangefuta kabisa

Ukitaka kupata uhondo wa habari za michezo cheki Star tv. jamaa wako juu sana.
 
Ukitaka kupata uhondo wa habari za michezo cheki Star tv. jamaa wako juu sana.

Mlachake nimekugongea thanx mimi nadhani STAR TV wapo juu zaidi ya hawa wawili. Yaani kwenye michezo wapo juu sana utaona habari zao ni za kina na kwa undani zaidi ya ITV. ITV bana wakionesha chandimu cha Bongo kwenye habari yao hata magoli huwa hawaoneshi sasa sijui ni habari ya wapi ya michezo, hata Channel Ten wako juu. TBC sijui wanafanyaje kazi maana sometimes kipindi kinaisha lkn huwezi jua kama kimeisha, kinakatishwa tu ghafla, muda kwao si kitu cha kujali saaana, aaagh TIDO onyesha ujuzi wako baba.
 
ITV gagulo
TBC sidiria...
Zote nguo za ndani.

Taarifa zao za habari utaona mashindano ya wafanyakazi wa mabenki, mara sijui kuvutana kamba, mara draft, mara sijui darts yaani upuuzi puuzi.

Lakini tofauti kubwa sana na star TV.
Hawa jamaa ukiangalia habari watakuonyesha habari za YANGA kamchambisha Azam.

Au utasikia ''na huko barani ulaya ktk ligi ya Serie A kiungo mshereheshaji anayeaminika kucheza soka la mbinguni Ronaldinho Gaucho the Saint jana aliisaidia klabu yake yenye mafanikio zaidi ulimwenguni ya AC Milan kuibuka na ushindi wa goli 3-0''.....halafu wanakupeleka uwanjani na kukuonyesha miujiza na chenga zenye upako toka kwa Dinho.

Hakika star TV wako juu kwa michezo.
Japo nao wakiamua kukufurulizia mashindano yao ya jimbo cup wanaboaga.
 
ITV na Radio one, kama mzee Mengi hatabadiri management zake, kwangu mimi naona anajiandalia kifo cha vituo hivyo.
nasema haya kwasababu, viongozi wake hawana ubunifu wakisasa, hawana mbinu za kukabiliana na changamoto za maisha ya kisasa.
ITV inaendeshwa vilevile kama miaka kumi iliyopitwa, kwa kuangalia mtiririko wa vipindi, uwasilishaji wake na hata haiba ya watangazaji wake.
Radio One, ndo kabisa, hata akifufuka leo mtu aliekufa mwaka 2000, ataweza kukupa ratiba nzima ya vipindi bila taabu.
hii ni ishara ya uongozi uliofulia, uongozi unaokopi na kupaste yaleyale.
ITV/Radio One KUGOMEA MECHI ZA SIMBA, hiki nacho ni kielelezo cha uongozi wenye fikra mgando, wanatumia majungu na fitina na hata mapenzi yao binafsi kuihukumu na kuinyonga SIMBA.
Kama hawakuwa na maslahi binafsi ni kwanini iwaume Simba kugomea Mechi zao kuonyeshwa ?
mbona imewauma sana ? mbona Star TV wanaendelea kama kawa na matangazo yao kuihusu Simba ?
Deo Rweyunga na Issack Gamba plus KitenGE Maulid, mmeumbuka ama Mmmeumbuliwa na Kaduguda, Fitina zenu hazitashinda.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom