TBC MPYA: Ushauri, Maoni na Mapendekezo ya ubora wa vipindi (Television Content)

Ukweli kwenye orodha ya channel ya kisimbuzi changu TBC niliifuta kabisa. Ni TV ya serikali lakin wanarusha habari za Mlango flani hivi.

Pia sahizi wana safari channel toka ianzishwe wanarudia vipindi vile as if wameweka mkanda Wa VHS, kama lengo ni kutangaza utalii basi kuweni wabunifu. Nashindwa kuelewa vijana wanafanya nini pale zaidi ya kutangaza Mpira.

Jifunzeni, elimikeni, badilikeni muendane na wakati. Onesheni ukongwe wenu sio mbaya mkajifunze AZAM MEDIA Kwa Tido
 
Mi napmba nijue, Ni lini mtaboresha mitambo yenu kwa wneo la kilolo milima ya udzungwa; ngangange, bomalangombe, masisiwe, udegenda na vijiji vingie ili tuwapate vizuri km mnavyojinadi kuwa niliondokewa ninyi ni bora!?
Umesahau idete, mbawe, mwatasi,masige,kibengu,mapanda
 
Ukweli kwenye orodha ya channel ya kisimbuzi changu TBC niliifuta kabisa. Ni TV ya serikali lakin wanarusha habari za Mlango flani hivi.

Pia sahizi wana safari channel toka ianzishwe wanarudia vipindi vile as if wameweka mkanda Wa VHS, kama lengo ni kutangaza utalii basi kuweni wabunifu. Nashindwa kuelewa vijana wanafanya nini pale zaidi ya kutangaza Mpira.

Jifunzeni, elimikeni, badilikeni muendane na wakati. Onesheni ukongwe wenu sio mbaya mkajifunze AZAM MEDIA Kwa Tido
Mimi TBC kwangu ndiyo bora kabisa kwani vipindi vya elimu navipata kwa ubora kabisaa
 
Tbc..acee naja Happ field next month. Tv programmer. Tv producer
Bila shaka naja na nondo mpya
 
Matangazo ya TBC1ya kipindi cha HADUBINI ya tarehe 13/04/2019 saa 2 usiku hayakuandaliwa vizuri kwa sababu sauti ya mtangazaji ilikuwa mbaya mno na ilikuwa haisikiki vizuri.Pamoja na kwamba kipindi kilikuwa kizuri sana kilichohusu nyumba ya ghorofa mbili iliotelekezwa na mzungu.Watu wengine wote waliokuwa wanazungumza sauti zao zilikuwa zinasikika vizuri.Tatiza la sauti mbaya na kutosikika vizuri liliendelea hadi mwisho wa kipindi kana kwamba fundi mitambo wa TBC 1 hakwepo na hakuona dosara hiyo iliokuwa wazi kabisa.Wahusika pia hawakuomba msamaha kwa Watanzania kutokana na tatizo hilo. Matatizo mengi ya TBC pengine hayafanyiwi maboresho kwa sababu pengine wahusika wanajua wao wanafanyakazi kwa ufanisi mkubwa wakati sio sawa.Kumekwepo na malalamiko mengi sana kuhusu chaneli mpya Tanzania Safari inayoonesha wanyama wetu na utamaduni wa makabila mbali mbali. Malalamiko hayo yanahusu kurudia rudia vipindi vile vile kwa muda mwingi.Yapo makabila mengi na utamaduni wao na iko mikanda mingi ya wanyama lakini TBC wameng'ang'ania ile ile kila siku.Kila siku tunaona wajukuu wa Mkwawa na kabila la Wahzabi na nyumbu. Hivi hakuna hata mtu mmoja wa TBC anaepitia maoni ya wadau mitandaoni ili waweze kuyafanyia maboresho?? Hakika watu wamechoka sana kuangalia marudio ya vipindi.Wahusika tuelezezeni kuna shida gani inawasibu na maandalizi ya vipindi vyenu.Sasa watu wamehamia chaneli zingine za wanyama ambazo nazo nyingi zinatoka mbuga za wanyama wa Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Napokea maoni mengi sana huko PM. Nakutana na kila aina ya maswali na jumbe za shauku ambazo watu wanahitaji kufanya kitu for TBC1.

Nasikitika kwamba nashindwa kuzijibu zote na kusemea chochote kwa sababu mimi sio mwajiriwa na wala sina mahusiano yoyote ya kikazi na TBC.

Niombe wote ambao mna maoni, ushauri, mapendekezo au mahitaji muyaweke hapa inatosha. Kwa bahati mbaya, huko PM sitoweza kusaidia chochote.

Miongoni mwa mawazo mazuri niliyopokea ni haya:

Habari,
Binafsi nimefurahiswa sana na maamuzi ambayo TBC inataka kuyachukua.

Kwanza kabisa;
Kumbukeni hiyo ni Station ya Taifa hivyo ina watazamaji wa kila namna, so kuzingatia maadili ni jambo la muhimu sana.

Pili;
Miaka hii wananchi wamegawanyika, Jambo litakalowateka na kuongeza watazamaji ktk station yenu ni kufanya mabadiliko ya kushangaa, Namaanisha.. Kwa kuwa imeshazoeleka kwa kurusha Events za CCM pia ianze kurusha na za vyama pinzani.

Je, mtalifanyaje hili..?
JIBU NI:
• Hakikisheni mnaongea na Uongozi wa vyama hivi kwanza, yaani mjadili na kujua ni tukio gani au mada gani mtakayokuwa mnairusha hewani na kama ina tatizo basi mliweke sawa kabla ya siku husika, hivyo mfanye malema uratibu wa vipindi vyenu mapema na iwe hivi hata kwa chama tawala pia.
Kwa kufanya hivi, hakika Mtarudisha matumaini kwa wananchi na kuanza kuwa watazamaji wakubwa wa vipindi vyenu.

• Pia, ongeeni na bunge mrudishe tena Bunge Live au baadhi ya mijadala na mingine itangazwe rasmi na bunge kuwa ni Siri Za Nchi hivyo haipaswi kurushwa live, naamini watanzania wote watalipokea vizuri na kufurahishwa na bunge,

Again, fanyeni uratibu wa vipindi mapema na setting za Camera pamoja na mitambo ya kurusha live mapema kabla ya bunge kuanza rasmi.

TATU;
Bei za kurusha matangazo kwenu ziwe kama bure kabisa, hii itawasaidia kuongezeka kwa wadhamini wa vipindi na kuwa station pekee hapa nchi yenye matangazo mengi especially kwa wajasiliamali wadogo wadogo na wawekezaji wa hapa nchini kwetu.

NNE:
Kumbukeni hicho ni chombo cha Burudani basi watangazaji wake wawe ni Vijana wenye Talent, Graphic za TBC ni mbaya sijawahi kuona, hivyo mnahitaji kuwaajiri vijana watakaokuwa wanaenda sambamba na Graphic za Wasafi Tv hali kadhalika na Clouds Tv ambazo zimekaa kisasa zaidi.

TANO;
Ombeni serikali iwekeze kwenu pesa ya kutosha, naamini hata serikali ikisema imetoa Billion kadhaa ili kuboresha Kituo Cha Habari Cha Taifa kiwe cha kisasa naamini hata wananchi wataunga mkono na kumpongeza JPM maana wamechoshwa mno na kituo hicho.
• Hivyo, Ajirini kwanza vijana kwa zaidi ya 90% then muweke kikao na kujadili mnahitaji vifaa gani vya kisasa, Camera zipi za kisasa, Magari ya matangazo na kufungua angalau branch 1 moja kwenye kila mkoa.

Waiteni hata wazungu wawafungie Mitambo hiyo the nitawapa Idea za Vipindi vitakavyokuwa bora zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TBC ya Mhando ilikuwa bora kuliko tv station zoote tz
Kwa kweli TBC mh, wiki iliopita tulilamika kuhusu mtangazajia wao wa habari za biashara Stanley, sasa hivi wamemtoa simuon tena, Habari za biashara zinasomwa direct, hatukumaanisha kumtoa ila awe serious na kazi yake na apewe IPAD ili awe wa kisasa zaidi ya kukunja makaratasi,sielewi wanafail wapi,hata mavazi yao kiujumla sasa sijui ni picha ndo zinawafanya wasiwe na mvuto?
 
Picha ni mbovu sana badilisheni ziwe za hd waigeni TV E na Clouds tv picha zao zinang'aa, kuacha kuegemea upande mmoja wa chama cha siasa kwa sasa waachieni ch. 10 wafanye kazi hiyo, vipindi ni vibovu sana wengi wetu tunapendelea movie na michezo mbalimbali rejea kipindi cha Jumba la Dhahabu, Channel zenu kupatikana bure kwa dish la ft 8 wakati channel zingine zinapatikana kwa dish ft 6, kushindwa kuhakikisha channel zenu zinaonyeshwa bure kwenye ving'amuzi vyote vya Tanzania.
 
Wameomba ushauri toeni ushauri mimapovu kede kede ya nini sasa.
Bolesheni ubora wa vipindi. Wapelekeni watangazaji kwenye mafunzo hata ya mwezi waendane na hali ya mtazamaji wa sasa.
 
Wameomba ushauri toeni ushauri mimapovu kede kede ya nini sasa.
Bolesheni ubora wa vipindi. Wapelekeni watangazaji kwenye mafunzo hata ya mwezi waendane na hali ya mtazamaji wa sasa.
Mafunzo ya mwezi kivipi? Unaweza fananisha viwango vya elimu vya TBC na chombo chochote nchini? Wao huajiri kujari sana elimu mnaotaka sauti muonekano nendeni TV za mitaani jua hiyo ni ya serikali kamwe haiwezi fanana na binafsi
 
Picha ni mbovu sana badilisheni ziwe za hd waigeni TV E na Clouds tv picha zao zinang'aa, kuacha kuegemea upande mmoja wa chama cha siasa kwa sasa waachieni ch. 10 wafanye kazi hiyo, vipindi ni vibovu sana wengi wetu tunapendelea movie na michezo mbalimbali rejea kipindi cha Jumba la Dhahabu, Channel zenu kupatikana bure kwa dish la ft 8 wakati channel zingine zinapatikana kwa dish ft 6, kushindwa kuhakikisha channel zenu zinaonyeshwa bure kwenye ving'amuzi vyote vya Tanzania.
Naam,ubora wa picha si mzuri kuonekana kwenye dish futi 8 hio aina ya satellite watumiayo,hilo la kuonekana ving'amuzi vyote mbona iko hivyo TBC 1na utalii,labda TBC 2 ndio ya kulipia je kisimbuzi gani TBC na utalii si za bure? Au sijakuelewa?
 
Daaa nyie hatakuwashaur hatujui wapi pa kuanzia......... Labda kwanza mungeibadir iyo T iwe Ccm Broadcasting Television CBT. Kifupi mnatuboa saana mpka kutoa ushaur tunaona uvivu
 
Wenzetu Kenya television yao ya taifa wanaonyesha michuano ya afcon wao wanakaz ya kusifia vjna wa Lumumba🤕🤕🤕🤕🤕🤕🤕
 
Mafunzo ya mwezi kivipi? Unaweza fananisha viwango vya elimu vya TBC na chombo chochote nchini? Wao huajiri kujari sana elimu mnaotaka sauti muonekano nendeni TV za mitaani jua hiyo ni ya serikali kamwe haiwezi fanana na binafsi
Kama mtaeshimu michango yetu ili mbadilike nina uwakika mtaboresha TBC. Ikiwa mnajibu kifedhuli kama hivi mjue ilo chombo kitakufa kwa midomo yenu michafu.
Mafunzo ya vitendo kwa vyombo vingine na msione aibu nendeni hata private television mkajifunze kwa kujitolea...
Kusoma sio mpaka muingie darasani..
 
Daaa nyie hatakuwashaur hatujui wapi pa kuanzia......... Labda kwanza mungeibadir iyo T iwe Ccm Broadcasting Television CBT. Kifupi mnatuboa saana mpka kutoa ushaur tunaona uvivu
Haiwezekani ccm wanayo yakwao chanelten,TBC 1 ya serikali toa mapendekezo kipi kifanyike acha kupotosha watu au kupoteza maana ya huu ukurasa
 
Back
Top Bottom