Matangazo ya TBC1ya kipindi cha HADUBINI ya tarehe 13/04/2019 saa 2 usiku hayakuandaliwa vizuri kwa sababu sauti ya mtangazaji ilikuwa mbaya mno na ilikuwa haisikiki vizuri.Pamoja na kwamba kipindi kilikuwa kizuri sana kilichohusu nyumba ya ghorofa mbili iliotelekezwa na mzungu.Watu wengine wote waliokuwa wanazungumza sauti zao zilikuwa zinasikika vizuri.Tatiza la sauti mbaya na kutosikika vizuri liliendelea hadi mwisho wa kipindi kana kwamba fundi mitambo wa TBC 1 hakwepo na hakuona dosara hiyo iliokuwa wazi kabisa.Wahusika pia hawakuomba msamaha kwa Watanzania kutokana na tatizo hilo. Matatizo mengi ya TBC pengine hayafanyiwi maboresho kwa sababu pengine wahusika wanajua wao wanafanyakazi kwa ufanisi mkubwa wakati sio sawa.Kumekwepo na malalamiko mengi sana kuhusu chaneli mpya Tanzania Safari inayoonesha wanyama wetu na utamaduni wa makabila mbali mbali. Malalamiko hayo yanahusu kurudia rudia vipindi vile vile kwa muda mwingi.Yapo makabila mengi na utamaduni wao na iko mikanda mingi ya wanyama lakini TBC wameng'ang'ania ile ile kila siku.Kila siku tunaona wajukuu wa Mkwawa na kabila la Wahzabi na nyumbu. Hivi hakuna hata mtu mmoja wa TBC anaepitia maoni ya wadau mitandaoni ili waweze kuyafanyia maboresho?? Hakika watu wamechoka sana kuangalia marudio ya vipindi.Wahusika tuelezezeni kuna shida gani inawasibu na maandalizi ya vipindi vyenu.Sasa watu wamehamia chaneli zingine za wanyama ambazo nazo nyingi zinatoka mbuga za wanyama wa Tanzania.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app