TBC mnatia aibu hongera star Tv na Chanel 10

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,837
Toka jana umalizike uchaguzi wa serekali za mitaa na ccm kuanguka vibaya tbc wamekimbia jukumu lao la kutujuza kuhusu mchakato mzima wa uchaguzi Aibu kubwa
Hongereni chanel ten na star tv mliwatendea haki wananchi wa tanzania tupo yuma yenu milele
Natowa wito kwa wananchi wote na makampuni ya Tz iwe mwisho kupeleka matangazo yenu Tbc mnapata hasara tu,watz hawaangalii tena labda wanachama wa ccm pekee tena nina mashaka hata wao wameisusia ila wanaona aibu kuweka wazi.
 
heri hata hao chanel 10 na star tv wanatangza,maana bila kutangazwa ni dalili za kuchakachua
 
Halafu nyie waongo sana mnabaki kupambana na vyombo vya habari! hivi CCM imeanguka vibaya wapi?
 
Wapinzani wa tanzania ni waajabu sana kwa matokeo haya bado wana waza CCM itaondolewa Ikulu 2015!
 
Halafu nyie waongo sana mnabaki kupambana na vyombo vya habari! hivi CCM imeanguka vibaya wapi?

Eeeh inamaana wewe husikii?basi angalau uwe unaona basi kiongozi au mpaka ukawa waingie ikulu ndio ukubali?ok subiri siku zimebaki sio nyingi bado mwaka tu.
Ila nashukuru najuwa wewe ni mmoja wa watu ambao hawajaangalia tbc toka jana ila kwa aibu utabisha nakushauri uendelee kuwakazia washapoteza mwelekeo
 
Ndugu,
Kama Watanzania hawaangalii, wewe ulifahamu vipi kama hawaonyeshi kwa sababu ndani ya mantiki kulingana na andiko, utakuwa umeiangalia TBC kwa muda mrefu mpaka ukajenga hitimisho kama hawaonyeshi matangazo unayotaka yaonyeshe.

Kwani wewe siyo Mtanzania?. Kama wewe umeangalia, una uhakika gani na wengine hawaangalii?

Wewe hutaki wengine waangalie lakini wewe unaangalia!. This is fun!

By the way, inawesekana hata hufahamu mantiki ya hoja yako!

Ni ushauri tu!
 
Wapinzani wa tanzania ni waajabu sana kwa matokeo haya bado wana waza CCM itaondolewa Ikulu 2015!

We ulitaka matokeo yapi?ebu tuanzie 1995 mpaka jana we unaonaje?2015 bado mtakwepo magogoni?moyoni unajuwa mtaondoka ila utabisha kwa makusidi bado mwaka tu ccm itabaki kwenye vitabu kama kanu kenya
 
Ndugu,
Kama Watanzania hawaangalii, wewe ulifahamu vipi kama hawaonyeshi kwa sababu ndani ya mantiki kulingana na andiko, utakuwa umeiangalia TBC kwa muda mrefu mpaka ukajenga hitimisho kama hawaonyeshi matangazo unayotaka yaonyeshe.

Kwani wewe siyo Mtanzania?. Kama wewe umeangalia, una uhakika gani na wengine hawaangalii?

Wewe hutaki wengine waangalie lakini wewe unaangalia!. This is fun!

By the way, inawesekana hata hufahamu mantiki ya hoja yako!

Ni ushauri tu!

Mkuu hebu tupe tathmini yako , vipi kuhusu hii mbinu ya mapingamizi?
Inalipa sana?
Je mtaendelea kuitumia na mwakani au mwakani kuna mbinu nyingine ya uchakachuzi wa uchaguzi?
 
Ndugu,
Kama Watanzania hawaangalii, wewe ulifahamu vipi kama hawaonyeshi kwa sababu ndani ya mantiki kulingana na andiko, utakuwa umeiangalia TBC kwa muda mrefu mpaka ukajenga hitimisho kama hawaonyeshi matangazo unayotaka yaonyeshe.

Kwani wewe siyo Mtanzania?. Kama wewe umeangalia, una uhakika gani na wengine hawaangalii?

Wewe hutaki wengine waangalie lakini wewe unaangalia!. This is fun!

By the way, inawesekana hata hufahamu mantiki ya hoja yako!

Ni ushauri tu!

Leo nakupongeza hujaweka majidai uliyozoea, hiki kipigo kimekupa busara. Hongera sana , maumivu huanza taratibu mwisho huwa ugonjwa. Hata kansa au ebora inaanza hivyo hivyo , na mdharau mwiba huota tende.
 
Tbc ccm imebaki kuonyesha bunge tu, angalau kwa hili wamejitaidi. Nje ya hapo ni kuonyesha kwa sana mikutano ya ccm na kuipamba zaidi.
 
Halafu nyie waongo sana mnabaki kupambana na vyombo vya habari! hivi CCM imeanguka vibaya wapi?
kweli magamba mmepigwa ganzi kweli, sasa mitaa yote ambayo upinzani imechukuwa ilikuw ccm, kama huku kwetu kati ya mitaa tisa CHADEMA mitaa 7 na ccm 2, wewe unaonaje? Hiyo unaona ccm wameshinda mingi ni ya mapingamizi waliweka ili kuwakatisha tama wagombea wa ukawa na wananchi, ila aibu kwao, halafu ikumbukwe mwaka jana serikali za mtaa walishinda 90% sasa hawata pata hata 75% na hii ndiyo tunajivunia kwamba tumewaonyesha kuwa hatuwataki.
 
Back
Top Bottom