Ndugu wana J-Forum napenda kuleta jamvini suala moja ambalo linanikera sana. Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu habari za kituo cha TV ya Taifa TBC imekuwa ikitoa habari kwa kupendelea chama cha mapinduzi kwa kurusha ktk taarifa za habari chaguzi zake mbalimbaali ndani ya chama sehemu mbalimbali za nchi. Kitu cha kushangaza ni kwamba Operesheni za vuguvugu la mabadiliko al maarufu kama M4C zinazoendeshwa na CHADEMA maeneo mbalimbali ya nchi au kampeni za udiwani ktk kata mbalimbali hazionyeshwi hata clip ya nusu dakika hiki ni kitu cha kushangaza sana. Je, kituo hiki ni cha CCM au ni cha Umma? Naomba kuwasilisha!!!!!