TBC badala ya kuitwa Televisheni ya Taifa, ni bora kuanzia sasa ikaitwa Televisheni ya Magufuli!

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
TBC ni Televisheni ya Taifa na inaendeshwa kwa kodi za wananchi wote, bila kujali itikadi zao za kisiasa

Kutokana na hali hiyo ni LAZIMA, TBC iendeshwe kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wanaifanya iendekee ku-survive

Kwa Televisheni yetu ya Taifa inavyoendeshwa, ni kama Mali binafsi ya Magufuli, Rais wa nchi hii.

Nitatoa mfano ninachomaanisha

Wakati awamu ya tano ilipoingia madarakani, walifuta kuonyesha Live, matangazo ya Bunge, kwa sababu za "kipuuzi" eti hawawezi kuonyesha Live matangazo hayo, kwa kuwa huo ni muda wa kazi na awamu hii imejitanabaisha kwa slogan yake HAPA KAZI TU

Kama kweli TBC ingekuwa Televisheni ya Taifa, ingesikiliza maoni ya watanzania namna wanavyotaka Televisheni hiyo ya Taifa, namna gani wanataka iendeshwe

Nakumbuka wakati yanafutwa matangazo hayo mubashara, wabunge wa upinzani na wananchi wenyewe walipa kodi inayoendesha Televisheni hiyo, walipinga vikali, kufuta matangazo hayo ya moja kwa moja

Hata hivyo tulichojionea baada ya kufutwa matangazo hayo, ni kila tukio linalotokea Ikulu, kuanzia kuapishwa kwa wateule wake, kukutana na vikundi mbalimbali vya kijamii, yakirushwa moja kwa moja mubashara na Televisheni hiyo na kitu kinachoshangaza ni kuwa matukio yote hayo yanatokea majira ya kufanya kazi, majira ambayo tuliambiwa watanzania kuwa majira ya kazi, kwa hiyo watanzania hatupaswi kuangalia Televisheni na badala yake tunatakiwa tuchape kazi, kwa kuwa slogan ya awamu ya tano ya serikali ni HAPA KAZI TUU!

Hata hivyo Bahati nzuri katika moja ya hotuba zake, Mheshimiwa Rais alikiri mwenyewe kuwa ni yeye aliyefuta matangazo hayo mubashara ya Bunge, kwa "kuwaagiza" wabunge wake wa CCM kwa kutumia uwingi wao kuyafuta matangazo hayo ya moja kwa moja!

Kitu kinachoniuma zaidi ni hili tukio la hivi sasa la michuano ya AFCON inayoendelea nchini Misri kipindi hiki, ambapo timu yetu ya Taifa imefuzu kwenye fainali hizo

Habari za uhakika ni kuwa timu zote zilizofuzu fainali ya michuano hiyo, Televisheni za nchi zao, zinaonyesha mubashara michuano hiyo, ikiwemo jirani zetu Kenya na kutufanya sisi kuwa ni nchi pekee, kati ya nchi zilizofuzu kwenye fainali hizo kutoonyesha michuano hiyo mubashara!

Ningependa kuwauliza manejimenti ya TBC, je Televisheni hiyo inaendeshwa kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wananchi, wanayoifanya Televisheni hiyo Iendelee ku-survive au ni kutokana na matakwa ya Mkuu wa nchi hii??
 
TBC ni Televisheni ya Taifa na inaendeshwa kwa kodi za wananchi wote, bila kujali itikadi zao za kisiasa

Kutokana na hali hiyo ni LAZIMA, TBC iendeshwe kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wanaifanya iendekee ku-survive

Kwa Televisheni yetu ya Taifa inavyoendeshwa, ni kama Mali binafsi ya Magufuli, Rais wa nchi hii.

Nitatoa mfano ninachomaanisha

Wakati awamu ya tano ilipoingia madarakani, walifuta kuonyesha Live, matangazo ya Bunge, kwa sababu za "kipuuzi" eti hawawezi kuonyesha Live matangazo hayo, kwa kuwa huo ni muda wa kazi na awamu hii imejitanabaisha kwa slogan yake HAPA KAZI TU

Kama kweli TBC ingekuwa Televisheni ya Taifa, ingesikiliza maoni ya watanzania namna wanavyotaka Televisheni hiyo ya Taifa, namna gani wanataka iendeshwe

Nakumbuka wakati yanafutwa matangazo hayo mubashara, wabunge wa upinzani na wananchi wenyewe walipa kodi inayoendesha Televisheni hiyo, walipinga vikali, kufuta matangazo hayo ya moja kwa moja

Hata hivyo tulichojionea baada ya kufutwa matangazo hayo, ni kila tukio linalotokea Ikulu, kuanzia kuapishwa kwa wateule wake, kukutana na vikundi mbalimbali vya kijamii, yakirushwa moja kwa moja mubashara na Televisheni hiyo na kitu kinachoshangaza ni kuwa matukio yote hayo yanatokea majira ya kufanya kazi, majira ambayo tuliambiwa watanzania kuwa majira ya kazi, kwa hiyo watanzania hatupaswi kuangalia Televisheni na badala yake tunatakiwa tuchape kazi, kwa kuwa slogan ya awamu ya tano ya serikali ni HAPA KAZI TUU!

Hata hivyo Bahati nzuri katika moja ya hotuba zake, Mheshimiwa Rais alikiri mwenyewe kuwa ni yeye aliyefuta matangazo hayo mubashara ya Bunge, kwa "kuwaagiza" wabunge wake wa CCM kwa kutumia uwingi wao kuyafuta matangazo hayo ya moja kwa moja!

Kitu kinachoniuma zaidi ni hili tukio la hivi sasa la michuano ya AFCON inayoendelea nchini Misri kipindi hiki, ambapo timu yetu ya Taifa imefuzu kwenye fainali hizo

Habari za uhakika ni kuwa timu zote zilizofuzu fainali ya michuano hiyo, Televisheni za nchi zao, zinaonyesha mubashara michuano hiyo, ikiwemo jirani zetu Kenya na kutufanya sisi kuwa ni nchi pekee, kati ya nchi zilizofuzu kwenye fainali hizo kutoonyesha michuano hiyo mubashara!

Ningependa kuwauliza manejimenti ya TBC, je Televisheni hiyo inaendeshwa kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wananchi, wanayoifanya Televisheni hiyo Iendelee ku-survive au ni kutokana na matakwa ya Mkuu wa nchi hii??
Habari kama hii kamwe huwezi kuikuta tbc
IMG_20190623_155557.jpeg
 
Jambo la kushangaza zaidi ni pale TBC wanapokata matangazo ya moja kwa moja yenye maslahi mapana kwa Taifa hili na kutupeleka Ikulu, kwenye shughuli za Rais

Mfano halisi ni hivi karibuni, wakati TBC ilipokata matangazo muhimu na yenye maslahi mapana kwa Taifa, ya mwelekeo wa Bajeti ya wizara ya Fedha, iliyokuwa ikisomwa asubuhi hiyo na kutupeleka Ikulu, ambako Rais alikuwa akikutana na wabunifu wa mkoa wa Njombe!
 
Awamu hii nimeinyooshea mikono..ni propaganda tu..hakuna professionalism..!!

Labda kuna mabadiliko baadae..tusife moyo!
 
TBC ni Televisheni ya Taifa na inaendeshwa kwa kodi za wananchi wote, bila kujali itikadi zao za kisiasa

Kutokana na hali hiyo ni LAZIMA, TBC iendeshwe kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wanaifanya iendekee ku-survive

Kwa Televisheni yetu ya Taifa inavyoendeshwa, ni kama Mali binafsi ya Magufuli, Rais wa nchi hii.

Nitatoa mfano ninachomaanisha

Wakati awamu ya tano ilipoingia madarakani, walifuta kuonyesha Live, matangazo ya Bunge, kwa sababu za "kipuuzi" eti hawawezi kuonyesha Live matangazo hayo, kwa kuwa huo ni muda wa kazi na awamu hii imejitanabaisha kwa slogan yake HAPA KAZI TU

Kama kweli TBC ingekuwa Televisheni ya Taifa, ingesikiliza maoni ya watanzania namna wanavyotaka Televisheni hiyo ya Taifa, namna gani wanataka iendeshwe

Nakumbuka wakati yanafutwa matangazo hayo mubashara, wabunge wa upinzani na wananchi wenyewe walipa kodi inayoendesha Televisheni hiyo, walipinga vikali, kufuta matangazo hayo ya moja kwa moja

Hata hivyo tulichojionea baada ya kufutwa matangazo hayo, ni kila tukio linalotokea Ikulu, kuanzia kuapishwa kwa wateule wake, kukutana na vikundi mbalimbali vya kijamii, yakirushwa moja kwa moja mubashara na Televisheni hiyo na kitu kinachoshangaza ni kuwa matukio yote hayo yanatokea majira ya kufanya kazi, majira ambayo tuliambiwa watanzania kuwa majira ya kazi, kwa hiyo watanzania hatupaswi kuangalia Televisheni na badala yake tunatakiwa tuchape kazi, kwa kuwa slogan ya awamu ya tano ya serikali ni HAPA KAZI TUU!

Hata hivyo Bahati nzuri katika moja ya hotuba zake, Mheshimiwa Rais alikiri mwenyewe kuwa ni yeye aliyefuta matangazo hayo mubashara ya Bunge, kwa "kuwaagiza" wabunge wake wa CCM kwa kutumia uwingi wao kuyafuta matangazo hayo ya moja kwa moja!

Kitu kinachoniuma zaidi ni hili tukio la hivi sasa la michuano ya AFCON inayoendelea nchini Misri kipindi hiki, ambapo timu yetu ya Taifa imefuzu kwenye fainali hizo

Habari za uhakika ni kuwa timu zote zilizofuzu fainali ya michuano hiyo, Televisheni za nchi zao, zinaonyesha mubashara michuano hiyo, ikiwemo jirani zetu Kenya na kutufanya sisi kuwa ni nchi pekee, kati ya nchi zilizofuzu kwenye fainali hizo kutoonyesha michuano hiyo mubashara!

Ningependa kuwauliza manejimenti ya TBC, je Televisheni hiyo inaendeshwa kwa matakwa ya walipa kodi wa nchi hii, ambao ndiyo wananchi, wanayoifanya Televisheni hiyo Iendelee ku-survive au ni kutokana na matakwa ya Mkuu wa nchi hii??
yule manager wa ile tv (tbc) ana shida sana!
 
Haina hadhi hata ya kuitwa TELEVISION, kwa vipindi gani walivyokua navyo, hata match za taifa stars haioneshi, television pekee ya taifa africa isioonesha match za timu ya taifa lake.

Bora ingeitwa "Channel Maalum Ya Kuunga Juhudi"
 
TBC imeshapoteza mvuto kabisa. Huu ujinga ndyo unautesa Star tv na radio yake RFM. Waliendekeza siasa. Sasa hii TBC utarun kwa hasara mpaka kifo chake.
 
Haina hadhi hata ya kuitwa TELEVISION, kwa vipindi gani walivyokua navyo, hata match za taifa stars haioneshi, television pekee ya taifa africa isioonesha match za timu ya taifa lake.

Bora ingeitwa "Channel Maalum Ya Kuunga Juhudi"
Hii hali haikuwahi tokea kwa marais waliopita.

Hili linajitokeza kwa mara ya kwanza katika utawala huu wa awamu ya tano
 
Kwani mkurugenzi wa hiyo magu tv anateuliwa na nani? Anayemlipa mcheza zumari ndo huchagua wimbo.
 
Kwani mkurugenzi wa hiyo magu tv anateuliwa na nani? Anayemlipa mcheza zumari ndo huchagua wimbo.
Pamoja na kuteuliwa na Rais, lakini jina la hiyo Televisheni inaitwa Televisheni ya Taifa na inaendeshwa kwa kodi ya wananchi, kwa hiyo wanapaswa waendeshe shughuli zao kwa weledi kwa ku-balance stories
 
Kipindi cha nyuma kabla ya awamu ya 5 michuano yote ya mpira haijalishi Tanzania imo au haimo TBC ilikua inaonyesha....sasa sijui kwann
 
Kipindi cha nyuma kabla ya awamu ya 5 michuano yote ya mpira haijalishi Tanzania imo au haimo TBC ilikua inaonyesha....sasa sijui kwann
Uongozi wa TBC umebaki kujipendekeza tu, kwa kila tukio linalotokea Ikulu linalomhusisha Mkulu,ni lazima walionyeshe Live!
 
Back
Top Bottom