Tee Bag
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 7,200
- 5,553
Nyie "Tibisii" nisikilizeni niwasaidie. Acheni kumuelekeza Mama Samia njia ya kupita. Hoja zenu kila siku ni "mama Samia avae viatu vya Magufuli, mama Samia apite njia ya Magufuli, mama Samia aendeleze yale aliyoacha Magufuli, mama Samia ajipime kwa viatu vya Magufuli, mama Samia alikua mwanafunzi mzuri wa Magufuli, mama Samia amalizie kazi aliyoacha Magufuli"
Muacheni MAMA afanye vile atakavyoona inafaa, ili mradi iwe kwa maslahi ya taifa letu. Yale mazuri aliyofanya Rais Magufuli tutayaenzi, lakini tusimlazimishe Mama Samia apite njia ileile ya Magufuli au afanye yaleyale.
Kumbukeni huyu sio msaidizi tena wa Magufuli. Huyu ni Rais wa nchi mwenye mamlaka kamili. Ana haki ya kuchagua njia yake anayoona inafaa kusaidia nchi. Msimlazimishe kuendeleza 'legacy' ya Magufuli. Ana haki ya kutengeneza 'legacy" yake kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo. Tumeelewana nadhani. Zindukeni kabla hamjazinduliwa!
Muacheni MAMA afanye vile atakavyoona inafaa, ili mradi iwe kwa maslahi ya taifa letu. Yale mazuri aliyofanya Rais Magufuli tutayaenzi, lakini tusimlazimishe Mama Samia apite njia ileile ya Magufuli au afanye yaleyale.
Kumbukeni huyu sio msaidizi tena wa Magufuli. Huyu ni Rais wa nchi mwenye mamlaka kamili. Ana haki ya kuchagua njia yake anayoona inafaa kusaidia nchi. Msimlazimishe kuendeleza 'legacy' ya Magufuli. Ana haki ya kutengeneza 'legacy" yake kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo. Tumeelewana nadhani. Zindukeni kabla hamjazinduliwa!