TAZARA wanaweza kufanya safari ya Dar - Mbeya kwa masaa matatu tu, suala ni kuwa na mikakati mikubwa ya muda mrefu

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,141
18,769
Nawashangaa sana watu wa TAZARA. Wanakubali kufiwa na shirika mikononi na siku zote kuwa na mikakati midogo sana ya kuifufua kampuni (mediocre strategies). TAZARA wanahitaji kufikiria kikubwa - think big - ikiwa wanataka kuendelea kuwapo.

Kwa mfano, umbali wa reli ya TAZARA toka Dar hadi Mbeya ni km 860. Treni za kasi za kampuni ya DB ya Germany zinazosafiri kati ya nchi ya Germany, Ufaransa, Belgium na Uswisi, spidi yake ya wastani ni km 250/hr, lakini zinaweza kwenda hadi spidi ya 300km/hr.

Kwa hiyo ikiwa reli ya TAZARA ambayo ni "heavy gauge" ikiboreshwa kutumia umeme na kuondoa kona kali, TAZARA watakuwa na uwezo wa kufanya safari kati ya Dar es Salaam na Mbeya kwa muda wa saa 3, kutia ndani na kusimama vituo vikubwa vya Ifakara na Makambako.

Gharama ya maboresho hayo ya TAZARA kufikia kiwango hicho hayawezi kufikia gharama ya kujenga SGR kati ya Dar na Morogoro. Yatafanya soko la TAZARA likue sana. Na nikweli safari za ndege Dar - Mbeya zitakosa soko, lakini si ajabu. Pia TAZARA wakifanya hivyo itapunguza sana utitiri wa mabasi njia ya Dar-es-Salaam hadi Mbeya. Watu wa Dar - Iringa au Dar- Songea wanaweza kuwa wanapanda mabasi toka Makambako.

Inawezekana, suala ni mipango tu, labda ubia na wachina kwa mradi kama huu ili kuinusuru TAZARA ambayo bila mkakati mzito itakufa. Think big TAZARA, acheni mipango ya maboresho ya kipwagu na pwaguzi, haitawapeleka popote. TAZARA wanaweza pia kufikiria kuendeleza reli hii kwenda Kyela na Malawi toka pale Vyawa (Mbozi) - ukifikiria suala la kupatikana mafuta ndani ya ziwa Nyasa.


1552320034856.png
 
Nawashangaa sana watu wa TAZARA. Wanakubali kufiwa na shirika mikononi na siku zote kuwa na mikakati midogo sana ya kuifufua kampuni (mediocre strategies). TAZARA wanahitaji kufikiria kikubwa - think big - ikiwa wanataka kuendelea kuwapo.

Kwa mfano, umbali wa reli ya TAZARA toka Dar hadi Mbeya ni km 860. Treni za kasi za kampuni ya DB ya Germany zinazosafiri kati ya nchi ya Germany, Ufaransa, Belgium na Uswisi, spidi yake ya wastani ni km 250/hr, lakini zinaweza kwenda hadi spidi ya 300km/hr.

Kwa hiyo ikiwa reli ya TAZARA ambayo ni "heavy gauge" ikiboreshwa kutumia umeme na kuondoa kona kali, TAZARA watakuwa na uwezo wa kufanya safari kati ya Dar es Salaam na Mbeya kwa muda wa saa 3, kutia ndani na kusimama vituo vikubwa vya Ifakara na Makambako.

Gharama ya maboresho hayo ya TAZARA kufikia kiwango hicho hayawezi kufikia gharama ya kujenga SGR kati ya Dar na Morogoro. Yatafanya soko la TAZARA likue sana. Na nikweli safari za ndege Dar - Mbeya zitakosa soko, lakini si ajabu. Pia TAZARA wakifanya hivyo itapunguza sana utitiri wa mabasi njia ya Dar-es-Salaam hadi Mbeya. Watu wa Dar - Iringa au Dar- Songea wanaweza kuwa wanapanda mabasi toka Makambako.

Inawezekana, suala ni mipango tu, labda ubia na wachina kwa mradi kama huu ili kuinusuru TAZARA ambayo bila mkakati mzito itakufa. Think big TAZARA, acheni mipango ya maboresho ya kipwagu na pwaguzi, haitawapeleka popote. TAZARA wanaweza pia kufikiria kuendeleza reli hii kwenda Kyela na Malawi toka pale Vyawa (Mbozi) - ukifikiria suala la kupatikana mafuta ndani ya ziwa Nyasa.


View attachment 1043252
Hili swala juzi tu na jamaa mmoja hivi hapa Mby tulikuwa tuna liongelea

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndiyo tulivyo mkuu, wanasubiri mpaka JPM aseme, hawapeleki proposal wala nini, sisi ni kukariri, kuwa creative hapana...Ni shida...
 
hiyo reli ina kona nyingi sana na milima ya kutosha pamoja na mahandaki zaidi ya 18 ngumu kutumia saa 3 kutoka Dar kwenda Mbeya. Pia station moja kwenda nyingi ni mwendo wa dakika 20 - 30 - 45 si rahisi sana kwa muda huo uliotoa kufika mbeya
Mkuu, treni ya kwenda Mbeya haiwezi kusimama hivyo vituo vidogo vidogo. Haiwezekani kwa spidi ya 250km/hr. IKitoka Dar itasimama Ifakara, halafu Makambako, halafu Mbeya. Vituo vingine vitahudumiwa na ordinary train
 
Sio kazi Mkuu, mainjinia watajua. Unaangalia spidi ya juu ya treni, na kuangalia radius ya kona na "banking" ya reli inayotakiwa.
Kwani mainjinia si ndio walifanya hiyo kazi ya ujenzi mkuu?
Binafsi ninavyofahamu shida kubwa ni hali ya kijiografia ya maeneo ndio changamoto kubwa sana, nina imani hata wao walipenda iwe rahisi lakini ndio hivyo.
 
Kwani mainjinia si ndio walifanya hiyo kazi ya ujenzi mkuu?
Binafsi ninavyofahamu shida kubwa ni hali ya kijiografia ya maeneo ndio changamoto kubwa sana, nina imani hata wao walipenda iwe rahisi lakini ndio hivyo.
Hapana, kona ziliwekwa kulingaa na design speed ya reli. Kwa hiyo kama unabadilisha design spidi ya reli inabidi uondoe makali ya kona. Kumbuka hata kona za barabara zinatengenezwa kwa kufikiria design spidi - kitu kinachoitwa road banking

1552324115519.png
 
Kuwa zuzuzuzu ni mojawapo vya vigezo vya kuwa kiongozi....ushahidi upo hapa bongo viongozi wanajali tu mshahara na kiki na kufanya maamuzi ya kitoto....hivi vitu kuongeleka ni rahisi na hata kutendeka ni simple ila tatizo ni wa africa....yani we can't do most things hadi natamanigi bara liitwe africant
 
Hapana, kona ziliwekwa kulingaa na design speed ya reli. Kwa hiyo kama unabadilisha design spidi ya reli inabidi uondoe makali ya kona. Kumbuka hata kona za barabara zinatengenezwa kwa kufikiria design spidi - kitu kinachoitwa road banking

View attachment 1043315
Mkuu, jaribu kufanya uchunguzi mdogo wahoji madereva wa loco hasa za mizigo unaweza fahamu zaidi kuhusu hii reli.
 
Tatizo sio speed tu bali ni huduma bora na dhamira ya kweli mbali na siasa.

Kama huduma ingeimarishwa na kuwa bora watu wanasafiri tu kwa treni.
Mfano:pakiwa na mabehewa masafi ya first class na second yenye huduma bora za chakula ,vyoo na malazi kwa nini watu wasipande kwa ajili ya utalii pia.
Lakini huduma ni mbovu nani atahangaika kupoteza muda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom