kende
JF-Expert Member
- Dec 2, 2013
- 3,527
- 1,664
Fella mchizi wangu... tena sana tu... long time kitambo hata Bongo Flavor haijaanza!! Lakini kibongo bongo, uki-mess na Fella; umeumia... bora u-mess na Ruge! Nakumbuka enzi za Wanaume Family, maskani madogo walikuwa wanamuogopa kama ukoma... wakianza kumng'ong'a basi ni lazima wafanye hivyo kimachale machale kwa imani kwamba Fella alikuwa anawaandea kwa bibi! Siku nimemuona Fella nyoko ni pale alipozinguana na mmoja wa washikaji wa Wanaume Family... kwa ku-show love, watu tukam-support yule mchizi akaenda studio, akagonga kopi kibao... nakumbuka tulihangaika sana kusambaza ile album radio stations...hata hivyo, haikupata airtime kabisa! Wambeya wakatupenyezea habari kwamba Fella kapita kufukia nyayo kila tulipopita... mchizi ambae tulimpa support ni very talented lakini amebaki historia!!
Hata hivyo, Fella sio mshamba kihivyo, sema inawezekana akinyuka pamba hazimtoi! Long time alikuwa na tabia ya kuvaa vijinzi vya kubana... ingekuwa siku hizi tungeita model... pata picha na ule mwili wake ingawaje enzi hizo hakuwa vile!!!
Bilashaka hapa unamzungumzia mtu wa kuitwa KAKA MAN