Tazama Protokali ilivyofelisha matamko mengi ya mawaziri hawa kutotekelezeka

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,252
21,345
Kutokana na kutozingatiwa chain-of-Command; matamko haya yalishindwa kutekelezeka kabisa!

Sababu hayakuwa na maelekezo ya kimaandishi kwenda kwa katibu wa wizara husika ili yatekelezwe;

Nitanukuu machache:
  1. Natangaza kuyavunja rasmi mabaraza ya ofisi za jiji Nchini -By Lukuvi
  2. Natangaza kufuta rasmi stika za usalama barabarani hazina tija- Lugola
  3. Natangaza rasmi hakuna kulipia nguzo za umeme zitatolewa bure nchi nzima- Kalemani
  4. Natangaza wagombea wote wa upinzani ambao majina yao yaliondolewa uchaguzi serikali ya mtaa yarudishwe- Jafo
Waandishi wa habari nao wamelala usingizi wa pono hata hawajisumbui kufatilia Utekelezwaji wa matamko hayo!
 
Daahh... Wanatuchezea akili zetu!! Maana sisi watanzania tunajua neno LA waziri ni kama sheria kumbe ni hewa!!? Kxtdkwysopfknlsrwuradosgpnsrwywin!!!!!!
 
Daahh... Wanatuchezea akili zetu!! Maana sisi watanzania tunajua neno LA waziri ni kama sheria kumbe ni hewa!!? Kxtdkwysopfknlsrwuradosgpnsrwywin!!!!!!
kwani hujawahi sikia kwamba wananukuliwa vibaya? Serikali inafanya kazi kwa maagizo ya kimaandishi ndiyo maana matamko yao huwa kama story tu za kijiweni
 
Haya mambo wangekuwa wanayasema baada ya kuwa wamewasiliana ndani,sasa baadaye anajikuta katamka ila halitekelezeki
 
Kuna Waziri alimwambia Mbunge wakiwa kantini kwamba "PM anatoa maagizo ya kisiasa yasiyotekelezeka". Basically hii ndio trend. Bahati nzuri makatibu wakuu wengi wa wizara wapo level headed na huwa hawawi fazed na hizo political drama za majukwaani
 
Kutokana na kutozingatiwa chain-of-Command; matamko haya yalishindwa kutekelezeka kabisa!

Sababu hayakuwa na maelekezo ya kimaandishi kwenda kwa katibu wa wizara husika ili yatekelezwe;

Nitanukuu machache:
  1. Natangaza kuyavunja rasmi mabaraza ya ofisi za jiji Nchini -By Lukuvi
  2. Natangaza kufuta rasmi stika za usalama barabarani hazina tija- Lugola
  3. Natangaza rasmi hakuna kulipia nguzo za umeme zitatolewa bure nchi nzima- Kalemani
  4. Natangaza wagombea wote wa upinzani ambao majina yao yaliondolewa uchaguzi serikali ya mtaa yarudishwe- Jafo
Waandishi wa habari nao wamelala usingizi wa pono hata hawajisumbui kufatilia Utekelezwaji wa matamko hayo!
Haha maelekezo bila baraka za malaika yule ni bure mkuu. Hii nchi ndipo ilipofikia na sijui huko tuendako
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom