dikteta2020
JF-Expert Member
- Aug 14, 2018
- 595
- 3,990
Kwenye video hapa chini kinaonekana kivuko ambacho kipo upande wa Mwibara. Kilitoka Ukerewe kwenda Mwibara ambapo kimemuacha ndugu Lissu akiwa Ukerewe kwenye mkutano. Yani Lissu amefika Ukerewe na kivuko kikatoka Ukerewe (Na tuliambiwa kuwa ni kibovu)
Tazama mbele ya kivuko yanaonekana magari. Magari haya ni pamoja na gari la Tundu Lissu (Prado nyeupe) na magari mengine ya msafara wa Lissu ambayo walitaka kuyavusha kwa kutumia kivuko hicho kutoka Mwibara kwenda Ukerewe. Sasa kwa kuwa waliambiwa kuwa kivuko ni kibovu, wakamua kuyaacha magari yao hapo (kama yanavyoonekana) kisha wakaenda zao Ukerewe kwa kutumia Mtumbwi.
Sasa ajabu kivuko kimetoka Ukerewe kimefika Mwibara hatimaye wameshindwa kushusha mizigo na mabasi waliyopaki ndani ya kivuko kwa kuwa magari ya msafara wa Lissu yaliachwa hapo na madereva wote wameenda Ukerewe pamoja na Lissu (Yame block njia).Sasa wanalazimika kusubiri hadi atoke Ukerewe ndipo waje watoe hayo magari ili kivuko kiweze kushusha mizigo na hayo mabasi.
Angalizo: Tundu Lissu aliambiwa kuwa kivuko ni kibovu na kwa leo kisingefanya kazi kabisa!
Swali, hapo nani kacheza kitoto?
Tazama mbele ya kivuko yanaonekana magari. Magari haya ni pamoja na gari la Tundu Lissu (Prado nyeupe) na magari mengine ya msafara wa Lissu ambayo walitaka kuyavusha kwa kutumia kivuko hicho kutoka Mwibara kwenda Ukerewe. Sasa kwa kuwa waliambiwa kuwa kivuko ni kibovu, wakamua kuyaacha magari yao hapo (kama yanavyoonekana) kisha wakaenda zao Ukerewe kwa kutumia Mtumbwi.
Sasa ajabu kivuko kimetoka Ukerewe kimefika Mwibara hatimaye wameshindwa kushusha mizigo na mabasi waliyopaki ndani ya kivuko kwa kuwa magari ya msafara wa Lissu yaliachwa hapo na madereva wote wameenda Ukerewe pamoja na Lissu (Yame block njia).Sasa wanalazimika kusubiri hadi atoke Ukerewe ndipo waje watoe hayo magari ili kivuko kiweze kushusha mizigo na hayo mabasi.
Angalizo: Tundu Lissu aliambiwa kuwa kivuko ni kibovu na kwa leo kisingefanya kazi kabisa!
Swali, hapo nani kacheza kitoto?