Uchaguzi 2020 Tazama hii video ya kivuko alichozuiwa kupanda ndugu Tundu Lissu kwa madai kuwa ni kibovu kikiwa Mwibara kisha soma ufafanuzi wa yaliyotokea

dikteta2020

JF-Expert Member
Aug 14, 2018
595
3,990
Kwenye video hapa chini kinaonekana kivuko ambacho kipo upande wa Mwibara. Kilitoka Ukerewe kwenda Mwibara ambapo kimemuacha ndugu Lissu akiwa Ukerewe kwenye mkutano. Yani Lissu amefika Ukerewe na kivuko kikatoka Ukerewe (Na tuliambiwa kuwa ni kibovu)

Tazama mbele ya kivuko yanaonekana magari. Magari haya ni pamoja na gari la Tundu Lissu (Prado nyeupe) na magari mengine ya msafara wa Lissu ambayo walitaka kuyavusha kwa kutumia kivuko hicho kutoka Mwibara kwenda Ukerewe. Sasa kwa kuwa waliambiwa kuwa kivuko ni kibovu, wakamua kuyaacha magari yao hapo (kama yanavyoonekana) kisha wakaenda zao Ukerewe kwa kutumia Mtumbwi.

Sasa ajabu kivuko kimetoka Ukerewe kimefika Mwibara hatimaye wameshindwa kushusha mizigo na mabasi waliyopaki ndani ya kivuko kwa kuwa magari ya msafara wa Lissu yaliachwa hapo na madereva wote wameenda Ukerewe pamoja na Lissu (Yame block njia).Sasa wanalazimika kusubiri hadi atoke Ukerewe ndipo waje watoe hayo magari ili kivuko kiweze kushusha mizigo na hayo mabasi.

Angalizo: Tundu Lissu aliambiwa kuwa kivuko ni kibovu na kwa leo kisingefanya kazi kabisa!

Swali, hapo nani kacheza kitoto?

 
Kwann Lisu afunge njia?? Haoni kuwa anawakwamisha watu! Inawezekana kweli kivuko kilikuwa kibovu lakini kimetengamaa baada ya kutengenezwa
Na hao watu wakiamua wawe Kama yeye unajua Nini kitatokea kwenye hayo Magari.Halafu eti huyu ndiye anaomba awe Rais, wakati vitu vidogo Kama hivi anashindwa kuonyesha uvumilivu wake na Busara zake.
 
Back
Top Bottom